Salome Mgaya (Mama Kibonge) akamatwa kwa ukwepaji Kodi za Mabilioni ya fedha Bandarini

Salome Mgaya (Mama Kibonge) akamatwa kwa ukwepaji Kodi za Mabilioni ya fedha Bandarini

ChanjoSugu

Member
Joined
Oct 22, 2021
Posts
14
Reaction score
33
Leo tarehe 13 Oktoba 2022, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekamata shehena ya mizigo ya vitenge ya marobota 290 katika kontena mbili yenye thamani zaidi ya tsh. Billioni 5 iliyopitishwa kwa magendo katika bandari zetu.

Mfanyabiashara mwenye shehena hiyo alitorokea Dubai majuma matatu yaliyopita, huku TRA wakiweka doria na ulinzi mkali sana.

Mfanyabiashara huyo wa Kariakoo, mtaa wa Aggrey, Bi. Salome Mgaya, maarufu kama 'Mama Kibonge' au 'Mkinga' amekuwa akifanya jambo lolote bila kuguswa na yoyote pindi anapoingiza mizigo yake nchini kwa njia za magendo. Muda mwingine amekuwa anawatishia watumishi wa Bandari au TRA kuhamishwa au kufukuzwa kazi.

TRA wameendesha Operesheni Maalum chini ya Waziri wa Fedha Mwigulu Madelu Nchemba na kuweza kumdhibiti Mama Kibonge.

Mama Kibonge amekuwa akidaiwa kutamba kwa zaidi ya miaka kadhaa bila kukamatwa na kuguswa na mamlaka nchini Tanzania.

Kwa wasiofahamu na wanaomtetea Mama Kibonge kukamatwa kwa Mizigo yake hawajui kuwa, wanamtetea mkwepaji kodi, fiisadi na haramia wa Mapato ya Nchi yetu.

IMG-20221013-WA0271.jpg
 
Mama bonge...hajawah shindwa vita...na hii vita anapigwa na boss wa simba na mamluki kibao..kuna kaumafia fulan hivi kwenye hii biashara ya vitenge....kuna mmoja anataka kuwa supplyer na ni billionea na mzawa lakin kiwanda chake hakikidhi uhitaji wa bidhaa kwa hao wahitaji.,,na hapa ndio vita ilipoanzia tokea enz za Magu....

NB bil 5 kwa mama bonge...aah jaman mbona wanamchafua...pesa ya mandaz kabisa hyo...
 
Kariakoo biashara mingi ni za kimafyaaa sanaaa, kwa anayeanza hutoweza jua wenzio wamepita wapi hadi walipo sasa, ..... saa saba usikuu mama Kibonge yuko macho ... anafwatilia marobota ya vitenge ..

mastermind bado hajadabwa
 
Back
Top Bottom