Samatta kwenda Aston Villa : Haki za Kimbangulile FC zizingatiwe

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Nakumbuka kwamba Timu ya Kimbangulile FC ya Mbagala ndiyo iliyomlea Mbwana Samatta hadi kufikia kuonwa na vilabu vikubwa , na kuna wakati iliambulia mgawo kwenye mauzo ya Mbwana , sina kumbukumbu kama ni kule TP Mazembe au KRC GENK .

Ninaamini kama kuna mgawo wowote wa kisheria basi Kimbangulile FC haitasahaulika
 
Sheria inasema asilimia 5 ya mauzo itagawanywa kwa timu alizopitia kwa maana ya hizo timu za Afrika ikiwemo Tp mazembe,simba,Lyon na hiyo uliyosema kama ndiko alikotokea. Hiyo 5% ya mauzo ndio waragawana hao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee mbona sheria ziko wazi, timu alizochezea zote kuanzia miaka 12 hadi 23 wana mgao wao
 
Kabla ya Kimbangulile FC alikua akichezea Zakhiem United, nao watataka chao pia.
 
Ki msingi Samatta mwenyewe hashindwi kutoa mshahara wake japo hata wa Siku 1 au hata Wiki 1 akawapa Kimbangulile FC. Yeye hatopoteza Sana lakini upande wa Kimbangulile utakua umefaidika Sana.
 
Hao Kimbangulile ni wa Juzi tu! Samatta alianza kukipiga pale Sukamahela FC

Natarajia na wao watapata Mgao wao kwenye hiyo asilimia 5
 
usipotoshe hii sheria inatumika kwa wachezaji waliokulia academy... na ni academy iliyohusika kumkuza mchezaji ndiyo wanapata hii kitu
Sheria inasema asilimia 5 ya mauzo itagawanywa kwa timu alizopitia kwa maana ya hizo timu za Afrika ikiwemo Tp mazembe,simba,Lyon na hiyo uliyosema kama ndiko alikotokea. Hiyo 5% ya mauzo ndio waragawana hao

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…