~^^~ Sambusa ni tamu bwana! ~^^~


funza ninasimama, sambusa kuzitizama
macho yanipima, kwa kudunda kwa mtima
mate yaniwama, mdomoni yamekwama
Napata hamu nasema, sambusa nikitizama
 
Nyingine ni za kichina
Zilizotuna kwa sana
Na zipo za Amerikana
Azipikazo Shaquana!
Sambusa ni tamu bwana, hasa zisizonana!
 
Nyingine ni za kichina
Zilizotuna kwa sana
Na zipo za Amerikana
Azipikazo Shaquana!
Sambusa ni tamu bwana, hasa zisizonana!

Mimi napenda pie
Ile pootang pie
Usidhani nazumgumzia papai
Hizo sambusa zako hazioni ndani
Utamu wake kama sukari
Mdomo wangu umebaki wazi

Ijaribu siku moja
Hakika itakunogea
Ikikudatisha
Usije kudhani ni kashata
Ukaja kuichanganya na ufuta
 
Duh! Mkjj nimekubali wee ni Malenga kinoma.
WoS nawe unatisha!
-----
Tuache utani watani
Sambusa ni tamu jamani
Nani asiyeitamani?
Si haramu asilani
Nzi kufia kidondani

Kitumbua tusisahau
Vipi laini za simu?
Voda na Tigo wadau?
Ukipewa huishi hamu
Utataka kula kila siku
 
Mie pia naafiki, kwamba sambusa ni tamu hazishindi bata mchafu kama niliyemla nyumbani kwa binamu ambaye alikolea pilipili, limau na chumvi bla kuzidi hata kidogo hahahahahah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…