Samia tumaini jipya Tanzania: The Economist baada ya kumsakama sana Magufuli, sasa angalau lina matumaini na Samia, laanza naye vizuri

Samia tumaini jipya Tanzania: The Economist baada ya kumsakama sana Magufuli, sasa angalau lina matumaini na Samia, laanza naye vizuri

Utapangiwa utake usitake.Hatuishi mbinguni.ugonjwa huu ni hatari,ukikupata ndio utaujua au kuusahau moja kwa moja.Tatizo wewe hutaki kukubali ukweli.Ukimwi ukiupata ni wewe tu,lakini huyu corona anakumaliza wewe au mimi na familia zetu.Tuendelee kuchukua tahadhari.
Ukweli unaotaka niukubali ni upi?
Nimeona watu wangu wa karibu wakiugua corona na nimethibitisha kuwa mwafrika akichukua tahadhari hana sababu ya kuiogopa corona.

Kwahivyo lazima Africa iwe na njia zake za kukabili maambukizi ya corona tofauti na za wazungu.

Ndio msingi wa hoja yangu ya TUSIPANGIWE.
 
Tunawaza tofauti. Mimi nawaza maslahi ya nchi kwa ujumla wake.
Huwezi kufikiri uchumi kwa ujumla wake bila kufikiri sera za uchumi zinazotengenezwa na mtu
Kwa mfano, TRA, BoT , TIC na vyombo vyote vya uchumi husikiliza sera za aliyeko madarakani
Kwa nchi zilizoendelea , yes, kwa nchi masikini zisizoheshimu taasisi kama yetu huwezikutenga uchumi na mtu
Yaani, ni kitu gani au sera gani ineleta impact ya kiuchumi kwa watanzania kwa ujumla wao, wewe unawaza mtu.
Nimejibu hapio juu. Kwa kuongezea tu, tulikuwa na sera ya uchumi wa soko huria wakati wa Mwinyi, Mkapa na JK.
JPM akaja na sera za 'monopoly' kama tulivyoshuhudia sekta ya anga ambako ushindani uliondolewa.
Unawezaje kutenga uchumi na mtu?
Sheria ya mihimili kutoshtakiwa haina shida.
Siyo mihimili bali wakuu wa mihimili ambao ni wanadamu. Mihimili ni taasisi
Tatizo lako unawaza mtu binafsi badala ya mhimili.
Yes kama mtu huyo ana impact kwa mhimili. Miaka 5 tumeshuhudia mhimili '' uliojichimbia chini zaidi' ulivyo fanya ''redundancy'' kwa mihimili mingine. Hayo hayakutokea katika mfumo wa taasisi na taasisi bali impact ya mtu katika taasisi.
Haina shida mhimili wa uraisi kutoshtakiwa. Urais ni alama ya utaifa, kushtaki urais ni kujishtaki kama taifa. Rais, kama mtu, akiwa mbovu kuna solutions zake. Ya kwanza ni kuwa voted out of the office. Ya pili ni kumaliza muhula na kusepa zake.
Urais ni institution lakini kuna Rais ambaye ni kiongozi wa taasisi.
Rais anaweza kushtakiwa kwasababu yeye pekee si alama bali anabeba alama.

Kuondoka kwa Rais hakuifanyi taasisi kuondoka. Kwa mantiki hiyo Rais anashtakiwa tofauti na mawazo ya kijinga kwamba ni alama. Kote duniani Rais akienda nje ya misingi ya kazi anashtakiwa.

Kilichotokea wakati wa nyuma ni baada ya kubaini kuna mpinzani alishinda kesi hivyo serikali ikapeleka mswada haraka wa kumkinga Rais aliyepo na si Marais waliotangulia. Hii haikuwa sahihi.

Kutengeneza sheria za kujilinda ni dalili ya kuhisi uovu. Hivi unaogopaje mahakama kama wewe ni clean?


 
Mtihani pekee mkubwa kwako ni kuukubali ukweli kuhusu Corona and do the right thing. Kwenye hili nimewahi kushauri mahali na hapa nashauri tena, "Kwavile Magufuli alikuwa hapendi kupangiwa na hatukumpangia, nawaombeni members humu, tusimpangie Samia". Samia Suluhu yuko vizuri sana, anajua nini cha kufanya, tumwache afanye vile anaona inafaa, please let's give her space ".
Mimi nimeona ni-'copy' tu haya:

Mosi, kukupa pole wewe binafsi, kama kimya kile kilikuwa kinatokana na kazi maalum, badala ya uteuzi wa waziwazi, au hata kama kulikuwa bado kuna subira za matumaini ya uteuzi chini ya Magufuli, bahati mbaya sana hilo halikuwa.

Pili - ndiyo, watu wasianze kujipendekeza kwa Samia na kumpa sifa hata kwenye mambo ambayo bado hajayafanya. Hii ni kutaka kujionyesha na kujipitishapitisha tu uonekane machoni au usikike masikioni mwake au kwa wapambe wake.

Tabia hii siyo nzuri hata kidogo, na ilikuwa moja ya tabia zilizomharibia Magufuli. Kupenda sifa kuliko uhalisia wake.

Msitafute kumsukumizia Samia naye aingie huko. Mwache achape kazi za waTanzania ajuavyo inafaa.

Kama ni lawama zitakuwa ni zake, kwa vitendo vyake, msianze kuchochea kwa ushangiliaji wa kkinafiki.
 
Yes kama mtu huyo ana impact kwa mhimili. Miaka 5 tumeshuhudia mhimili '' uliojichimbia chini zaidi' ulivyo fanya ''redundancy'' kwa mihimili mingine
Na kiuhakika zaidi, haukuwa "mhimili uliojichimbia chini zaidi", ni mtu binafsi mwenye mabavu zaidi aliyekuwa anauendesha mhimili huo peke yake, mbali na kuiendesha mihimili mingine alivyopenda.

Utawala wa namna ile haujapata kutokea na sidhani kuwa utatokea tena katika miaka ya hivi karibuni.
 
Waliokua wanatuma makala the economist wanafahamika.

Rais asikubali kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa.

Sifa hizo zina malengo ya kujaribu kulegeza misimamo iliyokata mirija ya kinyonyaji.

Namshauri Rais alinde masilahi ya Nchi asikubali kuyumbishwa na mabeberu.
 
Samora Machel alisema vizuri sana hapa kuhusu kusifiwa na wazungu:

IMG-20210325-WA0007.jpg
 
Naona dawa zimekusaidia kidogo mkuu, pia huyu mama hatafanya chochote cha ajabu sababu ya mfumo mbovu wa CCM pamoja na katiba yetu ikichangizwa na NEC ya ajabu ya Mahera, tatizo la nchi yetu hatuna mfumo imara isipokuwa tunategemea watu imara kama vile tuna mkataba na MUNGU, mwendazake watu walimchukia sababu ya tabia zake za kujiona yeye ni MUNGU mtu na nchi ilikuwa mali yake binafsi, ndiyo maana wapambe wake akina Bashiru leo wamevuna aibu kubwa sn. Tutengeneze mfumo imara na siyo mtu imara.
Mfumo imara siyo mtu mmoja, ajiimarishe awe mbinafsi na imara!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Wanabodi,

Kwa vile hili ndio bandiko langu la kwanza kwa mwaka huu, kwanza tutakiane heri ya mwaka mpya.

Pili tupeana pole sana kwa msiba mkubwa wa kumpoteza JPM.

Tatu, nitoe pongezi kwa President Samia kuwa rais wa JMT, kuongoza awamu ya Sita, hongera sana Mama Samia, umeanza vizuri kwa kuonyesha kuwa japo una nia ya kuyaenzi mazuri yote ya mtangulizi wako, umeonyesha kila mtu ana size yake ya viatu, sio vema kuvaa viatu vya mtu yoyote, bali viatu vyako vya size yako. Magufuli anazikwa na viatu vyake, huku ametuachia only mazuri yake ambayo ndio yanabebeka, na kwasababu he was a human being, lets carry only his good luggages, but not his baggages zake on his human side.

President Samia umeonyeshwa uwezo kwanza ni kwa kulibwaga hilo zigo ulilolikuta hapo mlangoni kwako Ikulu. Pia asante kutuletea a real diplomat pale MFA na sio yule Mwalimu wangu Orator mzuri tuu, pale hapahitaji oration ni diplomacy. Mtihani pekee mkubwa kwako ni kuukubali ukweli kuhusu Corona and do the right thing. Kwenye hili nimewahi kushauri mahali na hapa nashauri tena, "Kwavile Magufuli alikuwa hapendi kupangiwa na hatukumpangia, nawaombeni members humu, tusimpangie Samia". Samia Suluhu yuko vizuri sana, anajua nini cha kufanya, tumwache afanye vile anaona inafaa, please let's give her space ".

Kabla sikaanza, naomba kutoa angalizo muhimu. Kwa vile sasa Samia ndie rais, kuna watu sasa ndio wataanza kujipendekeza kwa Samia, hivyo kila mtu atakayeandika jambo lolote zuri kumhusu Samia akaonekana ana jipendekeza. Naomba usome bandiko hili uone nilisema nini kumhusu Samia na ni lini!.



Baada ya hayo sasa nije kwenye topic hii.
Kwanza mimi ni muumini wa kitu kinachoitwa karma, everything that happens, it happens for a reason, hivyo lolote likitokea, hakuna ubaya kulitafakari bila kumuuliza Mungu sababu, Mungu ana sababu zake kumchukua Magufuli na pia ana sababu zake kumleta Samia, we don't question God's authority.

Japo kifo cha rais Magufuli ni kazi ya Mungu, lakini pia kuna vitu vya kibinaadamu vimechangia, kama heshima kwa marehemu, naomba nisivitaje, lakini kama kuna kitu unakijua kumhusu Magufuli na kinaweza kuwa kimechangia, na sasa unakiona kinaanzishwa mdogo mdogo kuelekezwa kwa Samia, ukiweza kukizuia, kizuie, mimi sina uwezo wa kukizuia, ila nina uwezo tuu wa kukisema ili wenye uwezo wazuie, wakiona hakuna haja ya kuzuia ni kupuuzia tuu, let it be, mimi kwa upande wangu nitakuwa nimetimiza wajibu wangu, to inform.

Siku zote nimekuwa nikihubiri humu, kauli huumba, hakuna kitu kina nguvu humu duniani kama kauli. Pia nikasema uongo ukisemwa sana na kuachwa kujirudia rudia bila kukanushwa, huwa na mtindo sio wa kuonekana kama ukweli, bali kauli hizo za uongo kuumba huo uongo in reality na kuufanya ukatokea kweli.

Moja ya majarida makubwa kabisa ya kimataifa ya kibeberu, The Economist, kwa miaka yote mitano limekuwa likiandika makala za uongo mwingi na ukweli kidogo za kumsakama rais Magufuli. Uongo huu umekuwa ukirudiwa rudiwa bila kukanushwa, na matokeo yake ukaja kugeuka ukweli, sasa Magufuli hatunaye tena, sasa tuna Samia, jarida hili sasa linajipanga kuanza na Samia!. Jee Tanzania tuendelee kuacha uongo ukisemwa kuhusu taifa letu na viongozi wetu hatu lini?!. Hivi ni hatuna uwezo wa kukanusha, au ni tunapuuza kwa hoja kuwa wasomaji wao hawatuhusu, sisi wanaotuhusu ni Watanzania tuu?!. Sasa tunaishi kwenye global world, ulimwengu wa kiganjani, uongo ukisemwa popote unaingizwa kwenye social media, kila mtu anausoma, mkisingiziwa uongo, msipo kanusha, uongo huo unaonekana ndio ukweli. Tanzania ya Samia must do something on this.

Katika toleo lake la wiki inayoanzia April 3, The Economist limeibuka na makala hii kuihusu Tanzania ya Samia. Katika toleo hili this time angalau limeanza kwa kuonyesha Tumaini Jipya Tanzania: The Economist Baada ya Kumsakama Sana Rais Magufuli, Sasa Angalau Lina Matumaini na Rais Samia!, Laanza Nae Vizuri kwa kumtaka aachane na makosa ya Magufuli kwenye kudeal na Covid!. Yakwepa kuzungumzia chianzo cha kifo kilichotangazwa rasmi, waisingizia...

20210403_map502.jpg

Hoping for change​

Tanzania’s new president surely can’t be worse than the old one​


Uongo humu ni upi na una madhara gani, endelea kuandamana nami.

Paskali
Mabeberu watukome na wamkome vilivyo mama yetu! Hili gazeti La The Economist likome!! Hamu na tarajio kubwa la mabeberu ni kutuingiza kwenye utumwa wa Corona!! Tanzania ni nchi pekee duniani ambayo imegoma kuwekwa kwenye utumwa wa Corona!! Wazungu na ujanja wao wote wako kwenye kongwa la utumwa wa Corona!! Majirani zetu pia wako kwenye utumwa wa Corona! Kuingia kwenye utumwa wa Corona ni hiari! Lakini ukiingia humo si hiari tena kutoka!! Chonde chonde mama yetu, tafadhali usikubali kutuingiza kwenye utumwa huu wa corona!! Corona is over-rated!! Kila anayekufa wanalazimisha kuwa amekufa na corona ilí kuuhadaa ulimwengu kuwa corona ni ugonjwa hatari Sana!! Siyo kweli!! Hata walio na corona wakifa si kwamba wameuliwa na corona!! Mabeberu wanalazimisha kuwa ukiwa na corona halafu ukafa ni corona imekuua wakati si lazima iwe hivyo!! Tanzania tuko vizuri na wanajua hivyo! Hata Uingereza wametangaza kuwa kuanzia June wataachana na lockdown milele japo maambukizi bado wanayo mengi tu!! Wameamua Jambo hilo wakati Magufuli aliliamua toka awali, lakini bado wanasema Magufuli alifanya kosa! Lakini hawasemi Uingereza inafanya kosa!
Mpango wa chanjo wa covax hauna maana yoyote! Lengo ni kutuweka katika utumwa wa Corona tu!! Chini ya mpango wa covax ni asilimia 20 tu ya watu watakaochanjwa!! Hii ni asilimia ndogo Sana na haisaidii kufikia kuikinga jamii yaani kufikia herd immunity. Herd immunity inaanzia walau kuchanja asilimia 60.
Mabeberu wameshaishiwa rasilimsli za asili! Wameona corona ni biashara ya kudumu!! Wanakukopesha pesa ya kupima corona halafu unailipa kwa riba!! Watukome!!
Mask ina msaada kidogo Sana wa kumkinga mtu kutokuambukizwa!! Ingekuwa na msaada mkubwa basi maambukizi mapya yangeshakoma kwenye nchi ambazo watu wake wanashinda na barakoa!! Lakini huko huko ndo kila siku wanatangaza maambukizi mapya kwa maelfu!! Watukome!! Mama yetu mpendwa tafadhali usituingize kwenye utumwa huu wa corona!! Ila nikupongeze mama, mabeberu tayari umeshawakatisha tamaa!! Walitamani Sana wakuone unashinda na barakoa!! Nikupongeze mama mpaka hapo!! Wasikutishe!! Wasikufanye mtumwa!! Wewe ni Rais huru!!
 
1. Hayati JPM alihakikisha anasimama Imara ktk kulinda Rasilimali zetu haswa Madini alifanya hivyo kwa kubadilisha sheria mbali mbali na serikali ikaanza kunufaika kwa kiasi kikubwa, hatua hii haikuwa rahisi hata kidogo, mabeneru ambao ndio wanyonyaji wakuu kupitia makampuni yao hawakufurahiswa na hatu hizo.
choko choko na chuki ziliibuka.

2. Urafiki wa Mabeberu/wanyonyaji kwa nchi za kiafrika unakuwepo tu pale mirija yao inapo kuwa salama, lkn mirija ikikatwa lazima watakuchukia na watapambana kukuchafua.
kamwe usitetereke hapo ndipo kipimo cha uzalendo wako kinafanyika.

3. Tanzania hatutaki Diplomasia yakuwa wapole na kukubali kunyonywa rasilimali zetu huku wakitupumbaza kwa kutusifia sifa kemkem, hapana!! kamwe tusikubali kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa.
lazima tuwe wakali inapo bidi.

Wizara ya Mambo ya nje kwa sasa imepata mwana Diplomasia nguli, Mama Mulamula, sasa tunaamini tumepata, msemaji, mkanushaji na msawazishaji wa kimataifa

4.Tunamuomba Mama Samia ktk kusimamia Rasilimali na Maslahi ya watanzania ni bora uchukiwe na wanyonyaji/mabeberu kwa ajili ya watanzania.

Endapo wasaidizi wa Mhe. Rais kuanzia na; PM, Mawaziri, makatibu wakuu, ma Rasi, Ma Dasi, Wakurugenzi, watendaji wa vijiji na kata pamoja na watendaji na viongozi wote wa Idara za Serikali watafanya kazi zao kwa bidii, uadilifu na kujituma usiku na mchana basi kwa kufanya hivyo sio tu watakuwa wamemsaidia kupeleka maendeleo ya wana chi mbele bali pia watakuwa wame changia kulinda afya ya Mhe. Rais na kinyume chake watakuwa wamechangia kuzorotesha afya yake.
tufanye kazi kwa bidii na kwa kutumia maarifa, tuache wizi, rushhwa na ubadhirifu wa mali za umma.
 
U
Utapangiwa utake usitake. Hatuishi mbinguni, ugonjwa huu ni hatari. Ukikupata ndio utaujua au kuusahau moja kwa moja. Tatizo wewe hutaki kukubali ukweli. Ukimwi ukiupata ni wewe tu lakini huyu corona anakumaliza wewe au mimi na familia zetu. Tuendelee kuchukua tahadhari.
Ugonjwa huu siyo hatari kama inavyodaiwa! Kati ya wanaopata corona, ni asilimia ndogo Sana wanaofariki.
Magonjwa mengine asilimia kubwa ya wanaougua hufariki eg kansa!
 
1. Hayati JPM alihakikisha anasimama Imara ktk kulinda Rasilimali zetu haswa Madini alifanya hivyo kwa kubadilisha sheria mbali mbali na serikali ikaanza kunufaika kwa kiasi kikubwa, hatua hii haikuwa rahisi hata kidogo, mabeneru ambao ndio wanyonyaji wakuu kupitia makampuni yao hawakufurahiswa na hatu hizo.
choko choko na chuki ziliibuka.

2. Urafiki wa Mabeberu/wanyonyaji kwa nchi za kiafrika unakuwepo tu pale mirija yao inapo kuwa salama, lkn mirija ikikatwa lazima watakuchukia na watapambana kukuchafua.
kamwe usitetereke hapo ndipo kipimo cha uzalendo wako kinafanyika.

3. Tanzania hatutaki Diplomasia yakuwa wapole na kukubali kunyonywa rasilimali zetu huku wakitupumbaza kwa kutusifia sifa kemkem, hapana!! kamwe tusikubali kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa.
lazima tuwe wakali inapo bidi.

Wizara ya Mambo ya nje kwa sasa imepata mwana Diplomasia nguli, Mama Mulamula, sasa tunaamini tumepata, msemaji, mkanushaji na msawazishaji wa kimataifa

4.Tunamuomba Mama Samia ktk kusimamia Rasilimali na Maslahi ya watanzania ni bora uchukiwe na wanyonyaji/mabeberu kwa ajili ya watanzania.

Endapo wasaidizi wa Mhe. Rais kuanzia na; PM, Mawaziri, makatibu wakuu, ma Rasi, Ma Dasi, Wakurugenzi, watendaji wa vijiji na kata pamoja na watendaji na viongozi wote wa Idara za Serikali watafanya kazi zao kwa bidii, uadilifu na kujituma usiku na mchana basi kwa kufanya hivyo sio tu watakuwa wamemsaidia kupeleka maendeleo ya wana chi mbele bali pia watakuwa wame changia kulinda afya ya Mhe. Rais na kinyume chake watakuwa wamechangia kuzorotesha afya yake.
tufanye kazi kwa bidii na kwa kutumia maarifa, tuache wizi, rushhwa na ubadhirifu wa mali za umma.
Post nzuri sana! Ubarikiwe!
 
Huo ni mtazamo wa Gazetti la The Economist, hata raia wanaojielewa ninaamini wana mtazamo huo huo pia.

Katika kitu natamani ndugu mwandishi, siku moja uje kuanzisha thread kuichambua REPORT YA CAG ya mwaka huu bila kuwa biased kwa kusaka uteuzi. Bwana mkubwa hayupo nasi tena. Cha kusikitisha bungeni hayupo Zitto wa kuichambua vizuri hio report.

Key points;

1) ATCL kuendeshwa kwa hasara ya Billion 60 tokea 2016 - 2021.

Au ndio tuseme CAG pengine ana mhujumu Marehemu Rais Magufuli alietuaminisha kwa nguvu kubwa sana kwamba shirika linafanya kazi kwa faida, kufikia hatua shirika kupewa tuzo ya usafiri bora wa mwaka kuliko Turkey Airlines na serikali kupewa Hundi Ya Gawio La Faida na shirika???

Na je, Rais Magufuli angekua hai, angepewa hii hii report ya CAG yenye kulikosoa shirika la ATCL na TTCL, au kuna report nyingine iliopo kwenye makabati yenye mahesabu yaliopikwa ndio angepewa kumtukuza na kutuficha raia???

2) Matumizi ya hela nyingi zilizokua zinapelekwa Wizara Ya TAMISEMI na kutokujulikana matumizi yake, kufikia Rais Samia kumsimanga Waziri Selemani Jafo wazi wazi mbele ya vyombo vya habari, na kumtaka awasilishe mahesabu ya Wizara yake ndani ya muda mfupi, ila kabla hata ya Waziri Jafo ya kuwasilisha hayo mahesabu alioamrishwa na Rais, Rais akaamua kumhamisha Wizara baada ya Siku Mbili (Pengine baada ya kujua kwamba mahesabu hayo akipelekewa hata ridhika nayo kabisa).

3) TPA kukoroga mambo kwenye matumizi ya hela (Kwa viashiria vya ufisadi uliokithiri) mpaka kufikia hatua Rais Samia kumsimamisha kazi Mkurugenzi TPA na TAKUKURU kumshikilia na kufanya upelelezi wa Mabillioni kupotea kwenye account za TPA (Za BOT na NMB).

4) Matumizi ya hela HAZINA kuchotwa hovyo na wachache kwa kigezo cha matumizi (Matumizi yasio na mashiko wala sababu wala kujulikana). Kupelekea Rais Samia kumpa maelekezo CAG afanye ukaguzi upya wa matumizi ya hela zilizotoka hazina kuanzia January 2021 - March 2021.

5) Mikopo mingi sana kuchukuliwa na serikali kimya kimya bila kupitia bungeni, mikopo hio ya kimya kimya mingine bila hata kupitia katika Account za serikali na hela kuwa deposited kwenye Account za contractors na wauzaji wa ndege. Kitu kilicho sababishia serikali kuwa na deni zaidi kwa ukubwa ndani ya miaka 5 kuliko miaka 10 ya Kikwete.

Rais Samia kifupi, ana mashaka makubwa na matumizi ya hazina kuanzia mwaka huu kuanza (Ni aibu kwa watendaji kumfanya Rais awe ana mashaka na taasisi zao) na ana mashaka makubwa hasa na TPA.

Tulikua tunaaminishwa katika utawala ya 2015 - 2021 kulikua hakuna ufisadi kabisa, na mafisadi walikomeshwa kisawasawa sambamba na kutothubutu kuifisadi nchi. Raia walifurahi na kushangilia sana kwa hilo kwani mpambanaji wa mafisadi hatimae alipatikana kuwatetea wanyonge.

Ila katika hali ya kushangaza, na haya yaliotokea hivi karibuni kuna sintofahamu na imani imeanza kubadilika kabisa, kwamba ufisadi ulikuwepo ila "VITISHO VYA KUOGOPA KUIKOSOA NA KUIHOJI SERIKALI YA AWAMU YA 5" ndio sababu ya raia kuaminishwa kwamba hakuna ufisadi na mengineyo, ila sasa raia wanaanza kuamini ufisadi ulikuwepo kama awamu zilizopita (Na wengine wakiamini ufisadi umezidi awamu zilizopita - tuvute subira).

Na sisi wengine tunaamini, waliokua wanapata taarifa za ufisadi (Hasa waandishi wa habari wa kipelelezi) walikua wakiogopa sana kuweka wazi taarifa hizo, kwa kuhofia kupotezwa kama kina Azory Gwanda au kupewa kesi za uhujumu uchumi. Kasoro waandishi mliokua mnasaka uteuzi kwa kusifia hata yasio sifika.

NOTE THAT: baada ya awamu ya 6 kuingia madarakani, ndani ya week moja tu baadhi ya magazeti (Mfano Raia Mwema) wameanza kuisaidia serikali kutoa taarifa za ufisadi unaofanyika katika taasisi za serikali, kama hela zilizotolewa hazina kuanzia January 2021 mpaka March 2021 kwa kuweka wazi mpaka Account Number za benki na kiasi cha pesa zilizokua zikitolewa bila maelezo.

Issue ya Makontena Ya Makinikia, imeanza kuchukua taswira mpya, leak zimeanza kusambaa kwamba tume ya Prof fulani baada ya kufanya uchunguzi, ili baini kwenye makontena ya mchanga ule katika kila kontena la 20Ft kulikua na 0.7% ya dhahabu na sio 7.0% kama walivyolazimishwa kuandika kwenye report na Marehemu Boss Kazi baada ya kuona alikurupuka kwenye maamuzi (For the sake of political sympathy and legal consequences).

Acacia, mtoto wa ndani ya ndoa ya Barrick alikua akilipia kodi ya 0.7% ya dhahabu katika kila kontena la 20Ft kama ilivyotakiwa kisheria, na baada ya Boss Kazi kukurupuka na kufanya maamuzi bila kujiridhisha kwa kuunda tume ya uchunguzi aliamua kuyazuia makontena yale, report ilivyotoka ya tume ilibidi data kugeuzwa na kupikwa kuwa 7.0% ya dhahabu katika kila kontena badala ya 0.7%, Acacia ndio wakakutwa wanakwepa kodi.

Tulisubiri sana, zile NOAH moja kwa kila Raia kutoka kwa Acacia, ila kimya kilitanda mpaka umauti ukamfika alietupa ahadi ile. Tuliogopa ku hoji kipindi cha uhai wake, kwani tulimzoea kwamba hapendi kubanwa kwenye kona kwa hoja zenye mashiko. Pia tulimzoea alivokua akimaanisha pindi anaongea kwa kutumia maneno kuhusiana na serikali ya awamu ya tano SERIKALI YANGU, MIMI NINATAKA, tofauti na Mama anavyotumia maneno hayo na jinsi alivyoyabadilisha SERIKALI YETU, SISI TUNATAKA.
Si tuliaminishwa na tukaamini ATCL inaendeshwa kwa faida hata wakati kulikuwa hakuna wageni wengi kutokana na international flights kusitisha safari zao kutokana na corona na kwamba hata idadi ya watalii ilikuwa bado iko juu?
 
Back
Top Bottom