Unatengeneza kila kitu kivipi? Nimetoa mfano wa software Leo fb waondoe social media zao (Whatsap, insta na fb) kwenye simu za huawei au zisiruhusiwe unadhani huawei ataweza kutengeneza social media zake ? Unafikiri kuna mtu atanunua huawei? Kuna vitu vingine lazima utegemee watu, kutengeneza display inaweza isiwe issue lakini je itakulipa? Investment inaweza kuwa kubwa huku unauza simu chache ukala hasara. Ni Kama lile suala la kuchenjua mchanga wa dhahabu Kama una kiasi kidogo huwezi kuweka smelta ni bora upeleke Kwa mtu mmoja afanye hiyo kazi . Ni suala la cost and benefits
Au tuseme Muuza chips akisema alime viazi, alime alizeti akamue mafuta, awe na kiwanda cha kutengeneza majiko, achome mkaa na afuge kuku, awe na kiwanda cha vijiko na uma na vijiti, alime nyanya na vitunguu, alime matangoKwa ajiri ya salad , awe na kiwanda cha chumvi n.k
Unafikiri atafanya biashara au atakuwa anapoteza muda ??