Samweli Sitta anafaa kuwa Mwenyekiti wa Bunge la Katiba

Samweli Sitta anafaa kuwa Mwenyekiti wa Bunge la Katiba

Baada ya kutangazwa kwa wajumbe 201 wa bunge maalum la katiba napendekeza wabunge hao wamchague Mh, Sitta kuwa Mwenyekiti kwa kuwa alionesha kulimudu vyema bunge la JMT haswa katika mambo yenye maslahi ya taifa.

Natoa rai yangu kwa wajumbe wote 600 wasije chagua watu watakaopokea maelekezo kutoka serikalini. Katiba hii ni yetu na inahitaji mtu anayeona mbali na wala haongozwi na chama wala serikali.

Karibuni nanyi mpendekeze. Ni mdahalo wa wazi utakaowaongoza wajumbe kupata Mwenyekiti mwenye uwezo wa kulimudu bunge vyema, tusije pata watu kama akina Ndugai waliotawaliwa na usdhabiki na Jaziba.

NB tungepata mtu asiye na chama ingekuwa bora ila sidhani kama watakubali kumchagua mtu asiye na chama chochote cha siasa. hasa nje ya CCM

umetumwa na nape au mwakyembe?
 
tuwaachie wajumbe wachague wenyewe mwenyekiti wao.
 
Mawazo yetu yanaweza kuwa dira ya kuwaongoza.
Pia si kila mtu anaweza kuwa mkiti tu kwa kuwa anaongea pointi, La hawa wanaoongea kama akina Tundu , Mtikila na wengine ni vyema wasiwe m/viti kwa kuwa wao tutawategemea katika kutoa michango.
Mtikila si alisema anaenda mahakani kupinga mchakato mzima
 
pa pa pa pa pa makofi hayo, nimependa sana mapendekezo haya. Jiwe walilokataa washi litakuwa jiwe kuu la pembeni.

hii id imekuja kasi sana,post zako zote zipo kishabik sana,hivi kuna siku ambayo umewahi kuandika chochote kinachoweza kumsaidia mtanzania? tumia elimu yako kujikomboa na kuwakomboa wengine,acha ushabiki wa kisiasa.
 
Ninashauri spika wa bunge hilo atokane na majaji wastaafu.
 
Baada ya kutangazwa kwa wajumbe 201 wa bunge maalum la katiba napendekeza wabunge hao wamchague Mh, Sitta kuwa Mwenyekiti kwa kuwa alionesha kulimudu vyema bunge la JMT haswa katika mambo yenye maslahi ya taifa.

Natoa rai yangu kwa wajumbe wote 600 wasije chagua watu watakaopokea maelekezo kutoka serikalini. Katiba hii ni yetu na inahitaji mtu anayeona mbali na wala haongozwi na chama wala serikali.

Karibuni nanyi mpendekeze. Ni mdahalo wa wazi utakaowaongoza wajumbe kupata Mwenyekiti mwenye uwezo wa kulimudu bunge vyema, tusije pata watu kama akina Ndugai waliotawaliwa na usdhabiki na Jaziba.

NB tungepata mtu asiye na chama ingekuwa bora ila sidhani kama watakubali kumchagua mtu asiye na chama chochote cha siasa. hasa nje ya CCM

Usipende kukariri kijana, Sita wa kipindi kile siye yule wa leo....
 
Kwani akichaguliwa sitta je,kwa kipindi hicho chote atakachokuwa bungeni shughuli zake za uwaziri wa afrika mashariki zitaendeshwa na nani?
 
Jamii nzima ina matarajio makubwa na uongozi wa Samuel Sutta katika bunge maaluum la Katiba hasa kutokana na historia yake wakati wa Bunge la Tisa akiwa Spika.
 
Bado hajachaguliwa. Hata hivo dalili zote zinaonyesha ndiye atakayechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum. Uchaguzi ni kesho saa kumi jioni.
 
Kesho anaingizwa kazini Rasmi.Huyo ni tunu ya Taifa
 
Mimi siamini kama samwel sitta ndio mtu pekee anayestahili kuwa m/kiti wa tume ya katiba.Wapo wengi ila hawapewi fursa,mfano Mahalu
 
Jamii nzima ina matarajio makubwa na uongozi wa Samuel Sutta katika bunge maaluum la Katiba hasa kutokana na historia yake wakati wa Bunge la Tisa akiwa Spika.

Huyu ni CCM usitegemee fairness katika maamuzi yake.
 
Back
Top Bottom