Sare ya Real Madrid vs Real Mallocra jana ni somo tosha kwetu mashabiki wa Simba tulioipenda timu miaka hivi karibuni

Sare ya Real Madrid vs Real Mallocra jana ni somo tosha kwetu mashabiki wa Simba tulioipenda timu miaka hivi karibuni

Leonel Ateba Mbinda

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2023
Posts
644
Reaction score
2,695
Jana nilicheki mechi baina ya Real Mallorca vs Real Madrid, gemu iliisha kwa sare ya bao 1 -1, mpira mwingi ulipigwa na Real Mallorca jana na almanusura Madrid walie dakika za mwisho, Real Madrid ndio mabingwa wa soka duniani, ndio timu yenye mafanikio makubwa namba duniani, timu yenye makombe yasiyohesabika duniani.

Madrid imesheheni wachezaji wa hatari kabisa, kule mbele kuna watu wabaya mno.Jana Vini, Mbappe, Rodrigo walihangaika mnooo lakini wapi, Mallorca walipambana nao bila kujali majina.

Lakini kubwa zaidi na hoja yangu mimi ni Madrid kusare na timu ndogo kama Mallorca, sare ya jana haikuwashtua mashabiki wala kocha wala uongozi, sare katika mchezo wa kwanza ni jambo la kawaida hasa ukizingatia kuwa ndio kwanza mechi ya kwanza kwao.

Lakini pia wenzetu wanaamini sare ni sehemu ya mchezo, Madrid wamepambana sana lakini matokeo yakawa vile vile moja moja, walishambulia sana lango la Mallorca na Mallorca hawakuwa wanyonge kivile, waliwapelekea moto Madrid mwanzo mwisho.Huo ndio mpira.

Kwenu mashabiki wa Simba, timu yetu inapotoka sare au kufungwa ni sehemu ya mchezo, nafikiria jana Simba angesare au kufungwa sijui ingekuwaje leo Jumatatu, kama wewe unaona football iko upande wa ushindi tafadhali geuka kama Hamissa Mobetto au Meja Kunta au Nabii Meja nenda Yanga ambao wao wanaamini kushinda kila gemu ndio mpango mzima.

Kama Madrid anatoka sare na kibonde wewe nani uwe unashinda kila siku.
 
1979Magufuli umeandika andiko bora kabisa. Hakika wewe ni mzalendo mwenye nchi.

Jamaa wa mtaa wa pili ni mpaka waelezwe na Mzee Manara au Kikwete ndiyo wataelewa ulichoandika.
 
Jana nilicheki mechi baina ya Real Mallorca vs Real Madrid, gemu iliisha kwa sare ya bao 1 -1, mpira mwingi ulipigwa na Real Mallorca jana na almanusura Madrid walie dakika za mwisho, Real Madrid ndio mabingwa wa soka duniani, ndio timu yenye mafanikio makubwa namba duniani, timu yenye makombe yasiyohesabika duniani.

Madrid imesheheni wachezaji wa hatari kabisa, kule mbele kuna watu wabaya mno.Jana Vini, Mbappe, Rodrigo walihangaika mnooo lakini wapi, Mallorca walipambana nao bila kujali majina.

Lakini kubwa zaidi na hoja yangu mimi ni Madrid kusare na timu ndogo kama Mallorca, sare ya jana haikuwashtua mashabiki wala kocha wala uongozi, sare katika mchezo wa kwanza ni jambo la kawaida hasa ukizingatia kuwa ndio kwanza mechi ya kwanza kwao.

Lakini pia wenzetu wanaamini sare ni sehemu ya mchezo, Madrid wamepambana sana lakini matokeo yakawa vile vile moja moja, walishambulia sana lango la Mallorca na Mallorca hawakuwa wanyonge kivile, waliwapelekea moto Madrid mwanzo mwisho.Huo ndio mpira.

Kwenu mashabiki wa Simba, timu yetu inapotoka sare au kufungwa ni sehemu ya mchezo, nafikiria jana Simba angesare au kufungwa sijui ingekuwaje leo Jumatatu, kama wewe unaona football iko upande wa ushindi tafadhali geuka kama Hamissa Mobetto au Meja Kunta au Nabii Meja nenda Yanga ambao wao wanaamini kushinda kila gemu ndio mpango mzima.

Kama Madrid anatoka sare na kibonde wewe nani uwe unashinda kila siku.
Ni kweli lazima mashabiki wa uheshim mpira, Mbona wengine wapo Simba na Madrid lakini Matokeo ya kule Ulaya hayawashangazi ila uku kwenye Ligi wanapatwa na mshtuko.

Mimi nawashauri mashabiki wa Simba wajiondoe katika Hali ya kutaka kujifananisha na Yanga au Azam.
Hawawezi kuamini lakini kwa jinsi timu Yao ilivyo cheza kwa wastan wa mechi Nne zilizo pita lazima dirisha Dogo wafumue Tena timu.
Ili Simba waweze kushikiria nafasi ya tatu msimu huu inabidi Tff wa dhalirike kwa kufanya uhuni ili Simba waipate nafasi iyo.

Timu imekua ya hovyo kuliko matarajio ya wengi na kwaina ya baadhi yawachezaji wapya ukiacha Debora wengi wanauwezo wakaida na wanapatikana hapa Nchini Tena kwa bei chee kabisa.

Kama Kikosi Cha Simba kinathamani ya Bilion 7 basi Kuna shida kubwa pale Msimbazi.
 
Sasa mechi moja una determine timu kimeo atleast mechi 10 ndo unajua uelekeo wa timu
 
Kwahiyo kama madrid anatoa sare na sisi wana lunyasi tupite humo humo sio? Sawa mkuu

Mpira dakika 90+ ni matokeo matatu, USHINDI, SARE na KUPOTEZA. Kibaya ni kuwa na matokeo yasiyoridhisha mfululizo.
Jamaa ana hoja iliyojificha. Liverpool mara ya mwisho kuchukua kombe la ligi Kuu Uingereza ilikuwa ni msimu wa 2019/2020 na walichukua kombe hilo baada ya kukaa miaka 30 bila ya kuchukua kombe lolote la ligi.

Yaani Liverpool walichukua kombe la ligi mara ya mwisho msimu wa 1989/1990 ndiyo wakaja kuchukua tena msimu wa 2019/2020. Miaka 30 ilipita bila ya Liverpool kuchukua kombe la ligi.

Lakini mashabiki wa Liverpool ndiyo mashabiki bora kabisa kuliko mashabiki wa timu yoyote ile kwenye ligi ya uingereza.

Jee mashabiki wa Simba ama Yanga wanaweza kuendelea kuzishabikia timu zao zikikaa miaka 30 bila ya kuchukua kombe lolote la ligi?

Mfano mwingine ni wa timu ya Manchester City. Hawa jamaa msimu wa 1997/1998 walishuka daraja mpaka daraja la tatu la uingereza. Yapo Madaraja kumi.

Lakini mashabiki wa Man City walibaki kuwa mashabiki wa Man City Wala hawakutangatanga na leo hii wanafurahia kwa pamoja mafanikio ya timu yao.

Kuna la kujifunza kwenye hoja ya jamaa.
 
Shida sio matokeo kuwa mazuri ama kuwa mabaya ni nature ya ligi, Madrid anaweza akafungwa au akasare na wapinzani wake wakubwa Barca na Atletico wakasare au kufungwa vilevike, Kule taaluma ndio inaendesha ligi na sio mkato mkato ya nje ya uwanja , Tuje hapa Bongo sasa Simba akifungwa kudodisha pointi kutegemea Yanga afungwe inabidi kuroga sana au mshindane kwenye kutoa bahasha na N.K na kinyume chake.
Mazingira ndio yanaibua hisia za watu kutaka matokeo muda wote kwasasababu wanazujua figisu
 
Jana nilicheki mechi baina ya Real Mallorca vs Real Madrid, gemu iliisha kwa sare ya bao 1 -1, mpira mwingi ulipigwa na Real Mallorca jana na almanusura Madrid walie dakika za mwisho, Real Madrid ndio mabingwa wa soka duniani, ndio timu yenye mafanikio makubwa namba duniani, timu yenye makombe yasiyohesabika duniani.

Madrid imesheheni wachezaji wa hatari kabisa, kule mbele kuna watu wabaya mno.Jana Vini, Mbappe, Rodrigo walihangaika mnooo lakini wapi, Mallorca walipambana nao bila kujali majina.

Lakini kubwa zaidi na hoja yangu mimi ni Madrid kusare na timu ndogo kama Mallorca, sare ya jana haikuwashtua mashabiki wala kocha wala uongozi, sare katika mchezo wa kwanza ni jambo la kawaida hasa ukizingatia kuwa ndio kwanza mechi ya kwanza kwao.

Lakini pia wenzetu wanaamini sare ni sehemu ya mchezo, Madrid wamepambana sana lakini matokeo yakawa vile vile moja moja, walishambulia sana lango la Mallorca na Mallorca hawakuwa wanyonge kivile, waliwapelekea moto Madrid mwanzo mwisho.Huo ndio mpira.

Kwenu mashabiki wa Simba, timu yetu inapotoka sare au kufungwa ni sehemu ya mchezo, nafikiria jana Simba angesare au kufungwa sijui ingekuwaje leo Jumatatu, kama wewe unaona football iko upande wa ushindi tafadhali geuka kama Hamissa Mobetto au Meja Kunta au Nabii Meja nenda Yanga ambao wao wanaamini kushinda kila gemu ndio mpango mzima.

Kama Madrid anatoka sare na kibonde wewe nani uwe unashinda kila siku.
Usitusingizie YANGA, sisi sio mbumbumbu kama nyie makolo!sisi tunaamini katika matokeo matatu ya mpira!na hata siku moja YANGA akifungwa husikii kelele!tunahuzunika, tunasonga mbele!
 
Jamaa ana hoja iliyojificha. Liverpool mara ya mwisho kuchukua kombe la ligi Kuu Uingereza ilikuwa ni msimu wa 2019/2020 na walichukua kombe hilo baada ya kukaa miaka 30 bila ya kuchukua kombe lolote la ligi.

Yaani Liverpool walichukua kombe la ligi mara ya mwisho msimu wa 1989/1990 ndiyo wakaja kuchukua tena msimu wa 2019/2020. Miaka 30 ilipita bila ya Liverpool kuchukua kombe la ligi.

Lakini mashabiki wa Liverpool ndiyo mashabiki bora kabisa kuliko mashabiki wa timu yoyote ile kwenye ligi ya uingereza.

Jee mashabiki wa Simba ama Yanga wanaweza kuendelea kuzishabikia timu zao zikikaa miaka 30 bila ya kuchukua kombe lolote la ligi?

Mfano mwingine ni wa timu ya Manchester City. Hawa jamaa msimu wa 1997/1998 walishuka daraja mpaka daraja la tatu la uingereza. Yapo Madaraja kumi.

Lakini mashabiki wa Man City walibaki kuwa mashabiki wa Man City Wala hawakutangatanga na leo hii wanafurahia kwa pamoja mafanikio ya timu yao.

Kuna la kujifunza kwenye hoja ya jamaa.
Kama hoja yake ni hiyo sawa mkuu. Binafsi yanga na arsenal hata ziporomoke vipi bado nitabaki kuwa shabiki mwenye imani na timu.
 
Kama hoja yake ni hiyo sawa mkuu. Binafsi yanga na arsenal hata ziporomoke vipi bado nitabaki kuwa shabiki mwenye imani na timu.
Yeah. Ndiyo hoja yake.

Huwezi kusema eti unahama timu kwa kuwa haichukui makombe. Huo ni ushabiki kapuku, unakuwa huna ulijualo kwenye Mpira.
 
Nilichogundua Jana, Madrid wakikutana na Yanga, Yanga anajipigia tu kama Makolo....😃
 
Unakumbuka Malloca wakati anachezea Etoo, Kila Madrid wakikutana wanafungwa.
Huwa Kuna timu zikikutana hata Wana ubora namna gani Mara nyingi wanafungwa, kwa matokeo hayo sioni Cha ajabu.
 
Back
Top Bottom