Sare za JWTZ zamuweka kijana matatani

Sare za JWTZ zamuweka kijana matatani

ankai

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2017
Posts
3,282
Reaction score
4,251
Mkazi wa morogoro Abubakari Mbaya (22) anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani pwani kwa tuhuma za kukutwa amevaa sare z jeshi la wananchi Tanzania JWTZ wakati yeye akiwa si askari wa jeshi ilo.

Kijana huyo alikamatwa juzi jioni na askari halisi baada ya kutiliwa shaka eneo la kwa Mathiasi mjini Kibaha.

Kamanda wa polisi mkoa wa pwani Wankyo Nyige alisema kijana uyo alikuwa anasafiri na basi la Abood kutoka Morogoro kuelekea Dar esalaam akiwa amevalia sare izo za jeshi.

Kwa mujibu wa kamanda kijana baada ya kukamatwa alikiri kuwa kuwa ni kweli yeye si askari wa jeshi la wananchi na pia izo sare alizokuwa amevaa ni za babu yake ambaye alikuwa ni askari wa jeshi lakini kwa sasa ameahafariki .

Kijana aliweka wazi kuwa amekuwa akivaa sare izo za jeshi kutokana na mapenzi makubwa sana aliyonayo juu ya kazi iyo ya kulitumikia taifa kupitia jeshi la wananchi lakini amejaribu kila mbinu angalau aweze kupata nafasi ya kulitumikia jeshi ilo lakini kwake imekuwa ngumu sana.

Aliongeza kuwa tangia akiwa mdogo enzi za babu yake akiwa hai amekuwa akivaa izo umsare na muda mwingine alikuwa akimwibia babu yake.

Kijana hakusita kufikisha kilio chake kwa Mh Raisi waTanzania kwamba anamuomba kama itampendeza basi ampe nafasi ya kujiunga na jeshi la wananchi kwani anapenda kulitumikia taifa kwa moyo mmoja na ni kazi ya ndoto zake ambayo amekuwa akiiota siku zote za maisha yake.

Hata Kamanda alisema baada ya kijana kuhojiwa na uchunguzi kukamilika atafikishwa mahakamani ili akajibu tuhuma zinazo mkabili za kutumia sare za chombo cha ulinzi ili hali yeye si muhusika.

Maoni yangu kamanda haoni kama uyu kijana ni mzalendo wa hali ya juu kwa taifa lake kwanini wasimsaidie kukamilisha ndoto zake ili aje kuwa mtumishi mwenye kuipenda na uzalendo uliotukuka juu ya nchi yake kuliko kumfikisha mahakamani ili akafungwe?

IMG_20181030_120634.jpg
 
Inawezekana akawa kweli ni mzalendo, lakini sio sababu ya yeye kuvunja sheria....alitakiwa apigane kufa kupona kwa njia sahihi, kama kuingia jkt n.k....ili aweze kutimiza ndoto zake.
 
Asitafute huruma!
Mara nyingi askari akifariki au hata kustaafu au kuacha kazi kwa utaratibu vifaa vyake vyote vya kijeshi vinarudishwa jeshini.
Aseme vizuri hizo nguo alikuwa anazifanyia kazi gani?!
😡😡😡😡😡😡😡😡😡
 
Kuwa na huruma kwa ntoto wa mwezio.The dream comes true apelekwe tu Bulombora akachimbe chokaa
Asitafute huruma!
Mara nyingi askari akifariki au hata kustaafu au kuacha kazi kwa utaratibu vifaa vyake vyote vya kijeshi vinarudishwa jeshini.
Aseme vizuri hizo nguo alikuwa anazifanyia kazi gani?!
😡😡😡😡😡😡😡😡😡
 
Kuwa na huruma kwa ntoto wa mwezio.The dream comes true apelekwe tu Bulombora akachimbe chokaa
Weee ulisoma SUA nina hakika unajua vizuri tabia za vijana wa mkoa wa Morogoro walivyo wezi.
Bora tu wamkazanie aseme vizuri kuhusu hizo nguo, si ajabu kuna na wenzie wanazo.
 
Asitafute huruma!
Mara nyingi askari akifariki au hata kustaafu au kuacha kazi kwa utaratibu vifaa vyake vyote vya kijeshi vinarudishwa jeshini.
Aseme vizuri hizo nguo alikuwa anazifanyia kazi gani?!
😡😡😡😡😡😡😡😡😡
Hapa jirani na home kuna chalii yangu baba yake amefariki mjeshi mstaafu na hizo gwanda hawajarudisha mpaka leo zipo tu lkn hazivaliwi

Mbona kawaida wapo wengi hawarudishi vifaa wakistaafu
 
wamgongeshe tu,unaweza kukuta jamaa alikuwa anawaonea sana wenzake uko mitaa yao
 
Hapa jirani na home kuna chalii yangu baba yake amefariki mjeshi mstaafu na hizo gwanda hawajarudisha mpaka leo zipo tu lkn hazivaliwi

Mbona kawaida wapo wengi hawarudishi vifaa wakistaafu
Kiuitaratibu ilitakiwa jeshi lenyewe ndio wavifate au wavidai, ni kweli raia walio wengi wanakuwa hawajui kuwa hivyo vitu ni mali ya jeshi husika.
 
Asitafute huruma!
Mara nyingi askari akifariki au hata kustaafu au kuacha kazi kwa utaratibu vifaa vyake vyote vya kijeshi vinarudishwa jeshini.
Aseme vizuri hizo nguo alikuwa anazifanyia kazi gani?!
😡😡😡😡😡😡😡😡😡
Rahisi tu kufahamu mkuu km kweli za babu yake au la, maana zina identification. Code
 
Weee ulisoma SUA nina hakika unajua vizuri tabia za vijana wa mkoa wa Morogoro walivyo wezi.
Bora tu wamkazanie aseme vizuri kuhusu hizo nguo, si ajabu kuna na wenzie wanazo.
Haaaaaaaaa SUA????????????
 
Back
Top Bottom