Sasa ndio mtaamini nani mmiliki wa wasafi tv na redio

Hii issue ya coconut niliwaza pia,
 
SCANAD ni kampuni inayojihusisha na nini
marketing communication &digital marketing kwa ujumla

ila ndani yake kuna vitu vingi kama kumanage strategy za kampuni mteja, creative development, design, digital and IPO communication planning

ndio curent wana mkataba na tigo wa kutengeneza matangazo yao..matangazo yote ya tigo ukiyaona ujue ni hawa jamaa ndio wamehusika
 
Hili bara letu ni tatizo mkuu tena ni tatizo kubwa
 
92% kwa 8%?? Huyo Diamond ana akili kweli?
Alikua hana wanasheria wakanegotiate deal zuri??

Ina mana faida ya 100m yeye anapata 8 mwenzie 92??

Garbage
Haiwezi kuwa ratio ya hivyo, Diamond sio mbumbumbu hivyo japo ana form4 tu ila ni mjanja sana ndio maana hata wafanyabiashara wengi wameona ni potential candidate, inshort ana influence kubwa sana kwenye media za Tanzania na anakubalika mno! Kwa jinsi nilivyoona kwenye moja ya taarifa ratio ni ile ya 50 : 48 : 2 ambapo Diamond anakula hio 48%
 
Labda ivo inamake sense na ni fair
 
Safi sana dada yangu mwenyewe napataga wakati mgumu sana kwa brand ya Diamond kuwa na 2% ukiangalia kwa jinsi anavyojielewa na mameneja wake wanaomzunguka kama Sallam ambae anasema hawezi kumsindikiza mtu kwenye utajiri. Nakumbuka interview moja ya diamond kipindi kidogo aliulizwa kuhusu kuuza account yake instagram akasema labda kwa 1 billion ndio atauza alafu aje auze brand ya wasafi kwa 2% huu ni uzwazwa na ukiangalia nguvu anayotumia kuibarand wasafi media ni kubwa kuliko kawaida.
 
92% kwa 8%?? Huyo Diamond ana akili kweli?
Alikua hana wanasheria wakanegotiate deal zuri??

Ina mana faida ya 100m yeye anapata 8 mwenzie 92??

Garbage
Ulisha wahi kufanya biashara ya share?

Yaani mtaji wa kuanzisha project tuseme ni 50 Milion, mm nitoe milion 48 na ww utoe milion 2 halafu uje umiliki hisa 49 na mm nimiliki hisa 51? Hapa hata haitaji mwanasheria kama project ni wazo la kusanga na yy kma katoa hela nyingi, lazma Kusanga awe na hisa nyingi
 
Haiingii akilini kabisaa pale labda Wamegawana 50 na kusagaa...!!
Na ni zaidi ya 50 sababu kama pesa ya ku establish media anayo kama brand anayo sasa kusaga ana kipi cha kumzidi diamond mpaka yeye ndio awe top kwa wasafi media? Diamond ana kila kitu cha kuweza kusimamisha media yake pasi na kutegemea nguvu ya mtu. Media kaweza kusimamisha Dialo na dj majizo tena media kubwa tu atashindwaje Diamond? Tusikaushane uzazi bhana huyo kusaga nafikiri ndie anatembelea nyota ya diamond kama ushauri nk na asilimia atakuwa na chache tu.
 
sio kusanga mkuu ni kusaga.maana mwisho utasema kudanga
 
We unatoa capital yeye anatoa brand kubwa so haiwezi kua 92/8%


Kama ni hivyo huyo mmiliki si angeiita KUSAGA FM au KUSAGA TV?? Kama hela yake ilikua ina matter?
 
Kabisa Mond kwa sasa ni Brand kubwaa sanaa...! wasafi ni yeyee asilimia kubwaa tv na radio...Pia hizo perfume..karanga zote anamiliki kwa asilimia kubwa sana
 
Mkuu hivi unajua walio nyuma ya Diamond kumfikisha hapo alipo Kusanga yupo? Walio mfanikishia mafanikio ya diamond pana mikono ya watu wengi wengi sana, Hadi Kikwete yupo, brand ya diamond imekuzwa na watu wengi sana + juhudi zake mwenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…