Sasa ni dhahiri, super power ni moja tu hapa duniani

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Israel bila Marekani, si kitu huko Mashariki ya Kati.

Taiwan bila Marekani, si kitu mbele ya China.

Korea Kusini bila Marekani, si kitu mbele ya Kim Jong Un.

Na Ukraine bila msaada wa Marekani, si kitu mbele ya Urusi ya Putin.

Jana Rais Trump kachomoa misaada ya kijeshi ya Marekani kwenda Ukraine, leo Volodymyr Zelenskyy kasema sasa yuko tayari kusitisha mapigano na kufikia muafaka wa kumaliza vita na Urusi na kwamba anasikitika kwa kilichotokea Ijumaa ya wiki iliyopita pale ikulu ya Marekani.

Ukweli wa mambo ni kwamba Marekani ndiyo kiongozi wa dunia. Marekani ndo inayoiendesha dunia.

Muungano wa Ulaya, ulio na jumla ya nchi 27, umeshindwa kuipiga tafu Ukraine bila msaada wa Marekani.

Viongozi wa Ulaya sasa hivi wana matumbo joto wakihofia tetesi kuwa huenda Marekani ikajitoa kwenye jumuiya ya NATO.

Ulaya imeonyesha udhaifu wa kiwango cha hali ya juu sana kwa kuwa tegemezi ya Marekani.

Bila jeshi la Marekani, nchi zote za EU hazifui dafu mbele ya Urusi [kijeshi].

Msioipenda Marekani, poleni sana maana hii hali na hadhi vitaendelea kuwepo kwa muda mrefu sana.
 
Walijisahau kawaamsha. Mambo yanabadilika sasa wameelewa kuwa waache kuwa bendera fuata upepo
 
Waziri mkuu wa Canada dogo Justin Trudeau alisema Trump akiweka tozo na Sisi tunaweka, Leo naona jasho linamtika anawahaidi wananchi wake kuwa wajiandae na Hali ngumu ya maisha, ila anatafuta namna ya kumaliza vita hii ya miuchumi haraka iwezekanavyo!
 
Jamaa anaitekeleza sera yake ya Make America Great Again(MAGA) kwa vitendo.
 
ILA ISRAEL NI WATU WENGINE NDUGU FIKIRIA WANAJESHI 5 WA ISRAEL WANAPAMBANA NA MAKOMANDO 50 WA HAMAS LAKINI HAWAWAKIMBII CHECK CONGO WANAJESHI 1000 WANAWA KIMBIA M23 HAMSINI AU SYRIA SO HAWO KATIKA MAMBO YA KIJESHI WASHAJITOA KABISA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ