Sasa ni rasmi Rais wa TFF, Jamal Malinzi amehusika na upangaji matokeo

Hivi hili sakata ni kwanini Takukuru hawajaingia katika uchunguzi? Ama mpaka wapate maelekezo kutoka Ikulu? ama wao wa deal na issue za serikali tu na haya ya vyama vya michezo na mengineyo hayawahusu?
Ni ajabu sana details zote za viashiria vya rushwa vipo lakini hawa jamaa wa Takukuru wapo kimya.
 
Simpendi jamal mainziii kwa moyo wangu wote kaua kabisa kampira ketu kadogo tulikobaki nacho
 
Kwani uchaguzi ujao ni lini? Subiri na tayarisha pesa kwa ajili ya mikakati ya uchaguzi huo ili uingie wewe mkuu, maana majungu ni mengi hata ukikaa wewe.

Sina Muda Wa Kujibizana Na FOOLS Ila Kwa Wanaojua NINACHOKIPIGANIA Hapa Watanielewa. Au Huyo Malinzi Ni Babako Hivyo Unaogopa NISIMTUMBUE Zaidi? Sasa Kwa TAARIFA Yako Nina Mengineyo Mengi Zaidi Ya Haya Ila Nasubiria Nione Katika Hiyo 72 Hours ULTIMATUM Ya Kumtaka AJIUZURU Kisha Ndipo Utajua Kuwa Sipo Humu KUFANYA Masihara. Simpingi Malinzi Kama Malinzi Bali Napinga UPUUZI Wake Anavyoendesha SOKA La Tanzania. Na Kuna Breaking News Nyingine Imenifikia Sasa Hivi Unataka Niiweke Hapa ILI Uniheshimu Zaidi? Namsaidia Rais Wangu Dkt. Magufuli Katika Suala Lake Zima La " Anti - Corruption Drive " Katika Nyanja Zote Nchini Tanzania.
 
Nimeipata hiyo clip sehemu na nitaiweka muda si mrefu.

Mkuu Nitashukuru Kama UTAWAWEKEA Hapa Ili Watu WANIHUKUMU Kama Nina Chuki Binafsi Na Rais Wa TFF Jamal Malinzi au Nina HOJA Ya Msingi. Ila Kwa Ambaye Hajaipata Hadi Sasa Vuteni Subira Nafanya MKAKATI Niwawekeeni Ile CLIP Nyingine Ya Mchongo Mzima Ulikoanzia Ikianza Na Yule Kiongozi Wa Mashindano Wa TFF Bwana Chacha, Viongozi Wa TFF Mkoa Hadi Yule Jamaa Wa TFF Aliyesema WAZI WAZI Kuwa Alikuwa Ametumwa Na Rais Wa TFF Jamal Malinzi Kwenda Kuzugumza Na Viongozi Wa Timu Tajiri Ya Geita Gold FC Wiki Moja Kabla Ya Mechi Yao Ili Wafanye Vizuri Na Wapande Ligi Kuu. Kuna Mtu Mmoja Ambaye Kwa Sasa Sitamtaja Jina Ambaye Nitamwomba Mheshimiwa Waziri Nape Nnauye Na Rais Dkt. Magufuli Ikiwezekana Wampe TUZO Ya USHUJAA Kwani Huyu Jamaa Japo Ni Mmoja Wa Viongozi Wa TFF Lakini Aliweza Kufanya UDUKUZI Wa Hizi TAARIFA Zote Huku AKIWAREKODI Na Pia Akirekodi Mawasiliano Mengine Bila Hata Ya Hao WAJUMBE Kumshtukia. Niseme Tena Kuwa KWA USHAHIDI ULIOPO RAIS WA TFF JAMAL MALINZI HASTAHILI TENA KUWA RAIS WA TFF NA AWAJIBIKE KABLA YA HIZO SAA 72 NILIZOMPA KWANI MZIGO NILIONAO WA KASHFA ZAKE ZINGINE NI MKUBWA KULIKO HATA HUU WA SASA. Nipo Katika MAPAMBANO Na SITACHOKA!
 
Aluta Continua!
 
Jamal Malinzi njoo utufafanulie upya.

Nakuhakikishia Mkuu Kuwa HAWEZI KUJA KWANI ANAJUA KUWA KWA MABOMU MENGINE YANAYOMUHUSU NILIYONAYO HATOTHUBUTU KUTIA MGUU HUMU. Tumemvumilia Vya Kutosha Na Sasa TUMEMCHOKA! Na Asisahau KUTUOMBA MSAMAHA WANA MTANDAO WOTE WA JAMII FORUMS KWA KUTUDHIHAKI SIKU ILE AKIWA ANAFANYA PRESS CONFERENCE YAKE.
 
Hatimae Malinzi ameumbuka kunakotukuka. Sports HQ na E sports kupitia Efm hakika ni habari ya mjini.

Kama HUKUSIKILIZA Leo Sports Headquarters Ya E FM Radio Basi UMEKOSA MENGI Ila SIRI ZOTE Na UHUSIKAJI WA MOJA KWA MOJA WA RAIS JAMAL MALINZI Umejidhihiri Na Hana Sehemu Ya KUJITETEA Zaidi Tu Atusaidie Na ATUPISHE HATUMTAKI Vinginevyo Watu TUTAFUNGA ZAIDI Kisha Wenye MACHUNGU Na Mpira Wao " WACHAFUE KABISA HALI YA HEWA Na KINUKE ".
 
Katika watu wanaoliaribu soka la Tanzania ni huyu rais Wa sasa Wa ttf Na watu wake bila kujiuzuru huyu tusahau kusonga mbele katika soka letu madudu mengi yamefanywa katika uongozi wake akeweka pesa mbele mpira umekuwa Wa kuhonga sasa
 
Me naona aondoke , binafsi namkumbuka tenga ....huyu malinzi kaja tff kuvaa suti tu.
 
Viongozi wa Polisi Tabora wamesema wanakwenda kukata rufaa lakini pia,Malinzi akae akijua hiyo nafasi ataiona chungu mpaka ataiachia. Jamal Malinzi binafsi namshauri sana kuachia hiyo nafasi mambo yamekuwa mabaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…