Sasa tuzungumze kimichezo, Nawapongeza sana Simba, Yanga tuna la kujifunza kwa Simba hili liko wazi atakayebishe ana matatizo kichwani

Sasa tuzungumze kimichezo, Nawapongeza sana Simba, Yanga tuna la kujifunza kwa Simba hili liko wazi atakayebishe ana matatizo kichwani

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2010
Posts
60,050
Reaction score
104,466
Kipute cha robo fainali kati ya Simba na Orlando kimekwisha na Orlando amesonga mbele kwa kutupa faraja wana Yanga kuzima kelele, tambo na kejerli za Simba.

Tuongee ukweli tu ni kwamba mashabiki wa Simba hamna cha kuidai timu yenu kwa kutolewa robo fainali ni hatua nzuri timu imefika, nawapongeza sana kwa dhati kabisa, huwa tunaombea tu Simba ifungwe kwa sababu ya kelele na tambo tu za mashabiki wao.

Turudi kwa Yanga sasa, itakuwa ni fedhea kubwa kwa Yanga kuwa mabingwa wa nchi na kutolewa round ya kwanza tu hapo ndipo ulipo msingi wa hoja yangu.

Kama vile tunavyowakejeri Simba waje kupata tuition Yanga ya upigaji penati na sisi yanga tunapaswa kupata tuition tena nzito ya jinsi ya kuutumia uwanja wa nyumbani, siri yote ya mafanikio ya Simba iko hapo.

Haya mashindano ya Africa yalivyo kiuhalisia ni kwamba kila mtu ashinde mechi zake na hapa ndipo tuition ya Simba inapohitajika yale mazingaombwe yao pale kwa Mkapa Yanga hatuwezi kuyatumia?

Na kwakuwa mpira wa Africa umeonesha wazi kila mtu anashinda kwake basi tuwe na forward za ukweli kina Mayele watatu ili mechi za nyumbani unamaliza shughuri nyumbani kwa goli tano away unakwenda kuwachosha tu wapinzani wako.

Hongereni sana Simba kwa kuweza kuutumia vyema uwanja wa Mkapa kwa mbinu zozote zile, ziwe chafu au halali haijarishi cha msingi ni ushindi.
 
Uhasama ni uhasama tu kucheza kwao vizuri kikubwa wametoka kelele zao hua nyingi bora wametoka
Simba hawakufika hatua hiyo kwamba walikuwa ma timu bora kuliko Asec, haya mashindano siri yake ipo kwenye hesabu ya mechi za nyumbani tena unatakiwa kupiga mtu goli nyingi.

Tunao muda wa kuhakikisha next season Watanzania tunakwenda pamoja ikiwezekana robo fainali ya club bingwa mnakutana na derby ya Simba na Yanga.

Tunapaswa kuelekea huko sasa, sidhani kama Walibya ni bora zaidi yetu na wameingiza timu mbili robo fainali ili zicheze zenyewe.
 
Tunapaswa kuelekea huko sasa, sidhani kama Walibya ni bora zaidi yetu na wameingiza timu mbili robo fainali ili zicheze zenyewe.
Tunapaswa kufika huku kwa kweli, japo hili linahitaji maandalizi makubwa.
 
Huwezi sema una mafanikio kama hujachukua kombe
Ndio tuwekeze sasa tuache tambo zisizokuwa na mashiko.

Angola wamedhamiria mwaka huu na wameinvest kwenye timu yao usishangae kombe likienda Angola.
 

Ndio tuwekeze sasa tuache tambo zisizokuwa na mashiko.

Angola wamedhamiria mwaka huu na wameinvest kwenye timu yao usishangae kombe likienda Angola.
Ile timu Petro Luanda matajiri wale...wana visima vya mafuta😀😀😀.......kama hujui hata Simba huko Championi league amekushindwa......kaangukia kwa walioshindwa Confederation cup
 
Back
Top Bottom