Sasa Watanzania wanangojea kuona Wabunge wa kuteuliwa na Rais wakiapishwa haraka haraka na Ndugai kama akina Mdee

Sasa Watanzania wanangojea kuona Wabunge wa kuteuliwa na Rais wakiapishwa haraka haraka na Ndugai kama akina Mdee

Nimeipenda hiyo Mkuu Nchi iko mikononi mwa MBWA, na Nchi yoyote iliyo mikononi mwa MBWA haiwezi kupiga hatua zozote za Kimaendeleo.
Hahahaaa! Hautaliona hilo. Nyerere alisema kuwa hawezi kutoa nchi kwa mbwa - 1995. Bila Nyerere kujua, nchi tayari imeingia kwenye mikono ya mbwa.

Ni mbwa pekee wanaoweza kuteka wagombea pinzani ili wao wapite bila kupingwa. Ni mbwa pekee wanaoweza sema ruhusa TLP na UDP kusapoti CCM lakini haramu CHADEMA kusapoti ACT kwenye uchaguzi.

Ni mbwa pekee wanaoweza kufoji utaratibu wa kuteua wabunge wa viti maalum wakihusisha Bunge, mahakama na serikali halafu ikawa kama vile hakuna baya lililotendeka.

Ni mbwa pekee wanaoweza kuwawekea vikwazo wagombea wa vyama ambavyo vipo kikatiba ili wasifanye uchaguzi ambao upo kikatiba kwa kuwanyima usafiri ama kuzua usafiri wao wenyewe ili wasifanye kampeni.

Ni mbwa pekee wanaoweza kuchapisha makaratasi ya kura, weka tiki kwa CCM wakiwa majumbani na mahotelini, halafu kuyaingiza kwenye vituo chini ya ulinzi wa jeshi la polisi. Halafu jioni wakaacha kuhesabu kura kwenye hayo makaratasi. Badala yake wakasoma matokeo yaliyotoka kwa Mahera!

Ni mbwa pekee wanaweza kuvunja katiba yetu watakavyo na kusiwe na consequences.
 
2.trilion ndizo zinazowazuzua
CCM walizunguka nchi nzima kuutangazia uma kwamba wapinzani wanakwamisha maendeleo na ndiomaana wakakwapua majimbo yote hili bungeni wawe pekeyao chakushangaza leo hii tena wanawalazimisha wapinzani kwenda bungeni kwa nguvu amakweli hii dunia ina maajabu yake. Kuna nini Kwan
 
Tukio la karne na kihistoria la Spika wa Bunge la Tanzania (Job Ndugai) kuwaapisha chap chap wakina Halima Mdee na wenzake 18 nje ya ukumbi wa Bunge bila kuwepo kwa Wabunge wengine, wala kikao rasmi cha Bunge au kusimikwa kwa Siwa kumezusha mjadala wa kisiasa na Kikatiba.

Mtihani huo sasa umehamia upande wa pili wa kumtaka Spika Ndugai kuwaapisha chap chap Wabunge wapya wawili wa kuteuliwa na Rais ili wakaanze kutumikia mara moja majukumu ya Kibunge.

Safari hii, sijui wataapishiwa wapi?

Sote tunasubiri kuona na kujifunza mapya kutoka kwa Ndugai.
Tinatawaliwa kishenzi kabisa.
 
Mbona Spika mara baada ya kuwaapisha akina Mdee (Rejea clip ipo you tube) alielezea vizuri tu...kikatiba na kikanuni za Bunge utaratibu wa kuapa jinsi ulivyo. Kwamba kanuni mpya ya bunge baada ya kurekebishwa bunge lenyewe inamruhusu Spika kumwapisha m_mbunge Mahali popote atakapopachagua Spika mwenyewe Ili mbunge huyo aanze Kazi mapema pasipo kungojea kuapishwa mbele ya wabunge wengine wakati wa kikao cha bunge.

Kimsingi...Mbunge anaapa mbele ya Spika na si ndani ya ukumbi wa bunge au wakati wa kikao cha bunge au mbele ya wabunge.
Uwe unaakili basi kidogo ni kwamba kanuni inatokana na sheria Mama, na sheria Mama iliyozaa sheria nyingine ni KATIBA

Kwa mantiki hiyo basi KATIBA haiwezi kuifuta KANUNI bali KANUNI inatakiwa kuifuta KATIBA

Mnatuletea utawala wa kihuni kumbukeni na matokeo ya utawala wa kihuni ni kutuletea maendeleo ya kihuni, msije kumtafuta mchawi aliyewaloga wakati sasa hivi mnajiwangia wenyewe
 
Mbona Spika mara baada ya kuwaapisha akina Mdee (Rejea clip ipo you tube) alielezea vizuri tu...kikatiba na kikanuni za Bunge utaratibu wa kuapa jinsi ulivyo. Kwamba kanuni mpya ya bunge baada ya kurekebishwa bunge lenyewe inamruhusu Spika kumwapisha m_mbunge Mahali popote atakapopachagua Spika mwenyewe Ili mbunge huyo aanze Kazi mapema pasipo kungojea kuapishwa mbele ya wabunge wengine wakati wa kikao cha bunge.

Kimsingi...Mbunge anaapa mbele ya Spika na si ndani ya ukumbi wa bunge au wakati wa kikao cha bunge au mbele ya wabunge.
Sawa mkuu ndo maana watu wanasubiri na hawa wabunge wawili wateule wa Rais waapishwe haraka ili waendelee kutimiza majukumu ya kibunge kama ilivyo kwa wale 19 wa viti maalumu.
 
Tukio la karne na kihistoria la Spika wa Bunge la Tanzania (Job Ndugai) kuwaapisha chap chap wakina Halima Mdee na wenzake 18 nje ya ukumbi wa Bunge bila kuwepo kwa Wabunge wengine, wala kikao rasmi cha Bunge au kusimikwa kwa Siwa kumezusha mjadala wa kisiasa na Kikatiba.

Mtihani huo sasa umehamia upande wa pili wa kumtaka Spika Ndugai kuwaapisha chap chap Wabunge wapya wawili wa kuteuliwa na Rais ili wakaanze kutumikia mara moja majukumu ya Kibunge.

Safari hii, sijui wataapishiwa wapi?

Sote tunasubiri kuona na kujifunza mapya kutoka kwa Ndugai.
Wataapishwa getini maana parking kumejaa
 
Uwe unaakili basi kidogo ni kwamba kanuni inatokana na sheria Mama, na sheria Mama iliyozaa sheria nyingine ni KATIBA

Kwa mantiki hiyo basi KATIBA haiwezi kuifuta KANUNI bali KANUNI inatakiwa kuifuta KATIBA

Mnatuletea utawala wa kihuni kumbukeni na matokeo ya utawala wa kihuni ni kutuletea maendeleo ya kihuni, msije kumtafuta mchawi aliyewaloga wakati sasa hivi mnajiwangia wenyewe
Kabla sijakujibu naomba wewe mwenyewe uisome post yako taratibu na bila Jazba kisha utajitambua kuwa una hasira na haraka na papara.

Hata hivyo Mimi nimegundua ulichotaka kusema na nakujibu kama ifuatavyo.

Kwanza ni kweli kabisa kanuni yeyote Ile au sheria yeyote Ile ndani ya JMT haitakiwi ipingane na katiba ambayo ndiyo sheria mama.

Pili kama Kanuni ya Bunge iliyonukuliwa na Ndugai ingekuwa na shida.. yaani kuwa kinyume/ kupingana na Katiba ya JMT.. .Mahakama yetu tukufu isingekaa kimnya KWA uvunjifu huo wa Katiba kwani moja ya jukumu la mahakama ni hilo.

Mwisho ukiyakataa haya basi wewe wajifanya mjuzi na maridadi wa Sheria*Katiba na kanuni za Bunge kuliko wabunge wote wa JMT walioridhia kanuni hiyo ipite na pia wewe ni mtafsiri mzuri wa Katiba kuliko mahakama zetu.

Gombea ujaji...basi katika mahakama ya ICC..
 
Kabla sijakujibu naomba wewe mwenyewe uisome post yako taratibu na bila Jazba kisha utajitambua kuwa una hasira na haraka na papara.

Hata hivyo Mimi nimegundua ulichotaka kusema na nakujibu kama ifuatavyo.

Kwanza ni kweli kabisa kanuni yeyote Ile au sheria yeyote Ile ndani ya JMT haitakiwi ipingane na katiba ambayo ndiyo sheria mama.

Pili kama Kanuni ya Bunge iliyonukuliwa na Ndugai ingekuwa na shida.. yaani kuwa kinyume/ kupingana na Katiba ya JMT.. .Mahakama yetu tukufu isingekaa kimnya KWA uvunjifu huo wa Katiba kwani moja ya jukumu la mahakama ni hilo.

Mwisho ukiyakataa haya basi wewe wajifanya mjuzi na maridadi wa Sheria*Katiba na kanuni za Bunge kuliko wabunge wote wa JMT walioridhia kanuni hiyo ipite na pia wewe ni mtafsiri mzuri wa Katiba kuliko mahakama zetu.

Gombea ujaji...basi katika mahakama ya ICC..
Kuna mahakama tena au bunge?
 
Tukio la karne na kihistoria la Spika wa Bunge la Tanzania (Job Ndugai) kuwaapisha chap chap wakina Halima Mdee na wenzake 18 nje ya ukumbi wa Bunge bila kuwepo kwa Wabunge wengine, wala kikao rasmi cha Bunge au kusimikwa kwa Siwa kumezusha mjadala wa kisiasa na Kikatiba.

Mtihani huo sasa umehamia upande wa pili wa kumtaka Spika Ndugai kuwaapisha chap chap Wabunge wapya wawili wa kuteuliwa na Rais ili wakaanze kutumikia mara moja majukumu ya Kibunge.

Safari hii, sijui wataapishiwa wapi?

Sote tunasubiri kuona na kujifunza mapya kutoka kwa Ndugai.
Edeeddewew
 
Hahahaaa! Hautaliona hilo. Nyerere alisema kuwa hawezi kutoa nchi kwa mbwa - 1995. Bila Nyerere kujua, nchi tayari imeingia kwenye mikono ya mbwa.

Ni mbwa pekee wanaoweza kuteka wagombea pinzani ili wao wapite bila kupingwa. Ni mbwa pekee wanaoweza sema ruhusa TLP na UDP kusapoti CCM lakini haramu CHADEMA kusapoti ACT kwenye uchaguzi.

Ni mbwa pekee wanaoweza kufoji utaratibu wa kuteua wabunge wa viti maalum wakihusisha Bunge, mahakama na serikali halafu ikawa kama vile hakuna baya lililotendeka.

Ni mbwa pekee wanaoweza kuwawekea vikwazo wagombea wa vyama ambavyo vipo kikatiba ili wasifanye uchaguzi ambao upo kikatiba kwa kuwanyima usafiri ama kuzua usafiri wao wenyewe ili wasifanye kampeni.

Ni mbwa pekee wanaoweza kuchapisha makaratasi ya kura, weka tiki kwa CCM wakiwa majumbani na mahotelini, halafu kuyaingiza kwenye vituo chini ya ulinzi wa jeshi la polisi. Halafu jioni wakaacha kuhesabu kura kwenye hayo makaratasi. Badala yake wakasoma matokeo yaliyotoka kwa Mahera!

Ni mbwa pekee wanaweza kuvunja katiba yetu watakavyo na kusiwe na consequences.
Mnara wa BABELI waanza kuyumba tayari kwa kuanguka. Mungu hadhihakiwi.
 
Hahahaaa! Hautaliona hilo. Nyerere alisema kuwa hawezi kutoa nchi kwa mbwa - 1995. Bila Nyerere kujua, nchi tayari imeingia kwenye mikono ya mbwa.

Ni mbwa pekee wanaoweza kuteka wagombea pinzani ili wao wapite bila kupingwa. Ni mbwa pekee wanaoweza sema ruhusa TLP na UDP kusapoti CCM lakini haramu CHADEMA kusapoti ACT kwenye uchaguzi.

Ni mbwa pekee wanaoweza kufoji utaratibu wa kuteua wabunge wa viti maalum wakihusisha Bunge, mahakama na serikali halafu ikawa kama vile hakuna baya lililotendeka.

Ni mbwa pekee wanaoweza kuwawekea vikwazo wagombea wa vyama ambavyo vipo kikatiba ili wasifanye uchaguzi ambao upo kikatiba kwa kuwanyima usafiri ama kuzua usafiri wao wenyewe ili wasifanye kampeni.

Ni mbwa pekee wanaoweza kuchapisha makaratasi ya kura, weka tiki kwa CCM wakiwa majumbani na mahotelini, halafu kuyaingiza kwenye vituo chini ya ulinzi wa jeshi la polisi. Halafu jioni wakaacha kuhesabu kura kwenye hayo makaratasi. Badala yake wakasoma matokeo yaliyotoka kwa Mahera!

Ni mbwa pekee wanaweza kuvunja katiba yetu watakavyo na kusiwe na consequences.
UJOBILE Malafyale - YOU HAVE SAID
 
Mbona Spika mara baada ya kuwaapisha akina Mdee (Rejea clip ipo you tube) alielezea vizuri tu...kikatiba na kikanuni za Bunge utaratibu wa kuapa jinsi ulivyo. Kwamba kanuni mpya ya bunge baada ya kurekebishwa bunge lenyewe inamruhusu Spika kumwapisha m_mbunge Mahali popote atakapopachagua Spika mwenyewe Ili mbunge huyo aanze Kazi mapema pasipo kungojea kuapishwa mbele ya wabunge wengine wakati wa kikao cha bunge.

Kimsingi...Mbunge anaapa mbele ya Spika na si ndani ya ukumbi wa bunge au wakati wa kikao cha bunge au mbele ya wabunge.
Kanuni hazitakiwi kukinzana na Katiba, ikitokea utata wowote basi Katiba ndio hutawala.
 
Kabla sijakujibu naomba wewe mwenyewe uisome post yako taratibu na bila Jazba kisha utajitambua kuwa una hasira na haraka na papara.

Hata hivyo Mimi nimegundua ulichotaka kusema na nakujibu kama ifuatavyo.

Kwanza ni kweli kabisa kanuni yeyote Ile au sheria yeyote Ile ndani ya JMT haitakiwi ipingane na katiba ambayo ndiyo sheria mama.

Pili kama Kanuni ya Bunge iliyonukuliwa na Ndugai ingekuwa na shida.. yaani kuwa kinyume/ kupingana na Katiba ya JMT.. .Mahakama yetu tukufu isingekaa kimnya KWA uvunjifu huo wa Katiba kwani moja ya jukumu la mahakama ni hilo.

Mwisho ukiyakataa haya basi wewe wajifanya mjuzi na maridadi wa Sheria*Katiba na kanuni za Bunge kuliko wabunge wote wa JMT walioridhia kanuni hiyo ipite na pia wewe ni mtafsiri mzuri wa Katiba kuliko mahakama zetu.

Gombea ujaji...basi katika mahakama ya ICC..
Pole ndugu, lakini nawe waonyesha jazba,hasira.
Tulia kidogo ili kwanza utambue kuwa Tz ni yetu wote.
Siku hizi kuna maeneo mengi tu yanavurugwa ambayo Wasomi, wataalamu wetu wanayanyamazia au kujifanya hawayaoni ili tu kufurahisha wakubwa na kulinda matumbo yao.
Wakati wa kuanza kuyarebisha ni SASA. AMEN
 
Kuna mahakama tena au bunge?
Mahakama si bunge. Kazi ya Bunge ni kutunga sheria ndani ya JMT. Lakini kazi mojawapo ya mahakama ni kuhakikisha kuwa Bunge halitungi sheria iliyo kinyume au inayokinzana na Katiba ya JMT.
Umeelewa??
 
Back
Top Bottom