Saudi Arabia yatangaza kujenga mji bila barabara

Saudi Arabia yatangaza kujenga mji bila barabara

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,677
Ujenzi huo utaanza miezi minne ya mwanzoni mwa mwaka huu wa 2021. Usafiri wote wa umma utakuwa chini. Mwanamfalme Salman ametangaza lengo lake la kuanzisha mradi wa ujenzi wa mji usiokuwa na barabara na usioruhusu magari na kutoa maelezo ya taarifa hiyo siku ya Jumapili.

Kwa mujibu wa mwana mfalme Mohammed bin Salman, alisema ifikapo 2050, watu bilioni moja watakuwa hawana makazi kutokana na hewa chafu ya kaboni. Ndio maana Saudi Arabia imepanga kujenga mji mpya ambao hautakuwa na magari.

Takwimu zinaonesha kuwa ni watu milioni moja tu ndio wataishi katika mji huo. Asilimia tisini ya idadi ya watu duniani inapata changamoto ya hewa chafu. "Kwanini dunia iruhusu watu milioni 7 kufariki kila mwaka kwasababu ya matokeo ya hewa chafu?"
"Watu wengine milioni 7 wafariki kutokana na ajali za barabarani."

Mji huu utajengwa ukiwa unazingatia hali rafiki kwa mazingira. Mji huo utakuwa na shule ,hospitali, bustani, na usafiri wa mwendo kasi wa chini. Ujenzi wa mji huo mpya kwa Saudi Arabia ni sehemu ya kuacha utegemezi wa rasilimali moja ya mafuta pekee.

BBC SWAHILI
 
Tutaona uvumbuzi wa Mwarabu! Mungu awanusuru hao wakazi watarajiwa na majanga ya moto au dharura za kiafya zenye kuhitaji magari ya dharura kutoa huduma husika.
 
Usikute sababu ni kuwakomoa wanawake ambao ndo wanalilia haki ya kuendesha magari huko kwao
Lengo ni kuvutia watalii na uwekezaji nje ya mafuta kama ilivyo kwa Emirates. Ndiyo maana kidogo kidogo wanalegeza sheria pia.
 
"Kwanini dunia iruhusu watu milioni 7 kufariki kila mwaka kwasababu ya matokeo ya hewa chafu?"
Lkn si magari mapya yanayotumia umeme badala ya mafuta yanalenga kudhibiti hewa chafu?
 
ajenge barabara kwa ajili ya magari yanayotumia umeme tu kama hataki hewa chafu
 
Usikute sababu ni kuwakomoa wanawake ambao ndo wanalilia haki ya kuendesha magari huko kwao
Mnashobokea jambo la Wanawake...ni watu waovu sana katika uso huu wa Dunia

Lengo kuu....ni kupata fursa ya kula kimasikhara

Ovyo kabisa
 
Wanatumia fedha za mahujaji wa makka na madina kujengea miji ya kifahari.

Biashara ya hijja na dini inalipa sana
 
Huo mji ni mkubwa kwa kweli na phase 1 imeisha na 2025 itakamilika maana wanasema ni x33 ya ukubwa wa NY
Mji mpya ndio habari ya mjini kama Chato vile [emoji1]
1. Vp soo la Kashoggi walimalizaje?

2. COVID imewakosesha jamaa mabilioni toka Kwa Watalii (wakiwemo ndugu zetu toka KISIJU).
 
Wanatumia fedha za mahujaji wa makka na madina kujengea miji ya kifahari.

Biashara ya hijja na dini inalipa sana
Utalii unaiendesha Singapore
Mafuta yanaiendesha Nigeria
Viwanda vinaiendesha China
Kaaba inaiendesha Saudi Arabia.
 
1. Vp soo la Kashoggi walimalizaje?
2. COVID imewakosesha jamaa mabilioni toka Kwa Watalii (wakiwemo ndugu zetu toka KISIJU).

1. Watano walihukumiwa kifo Dec 2019 na 3 walifungwa na wengine kufukuzwa kazi
2. Covid inakung’uta kila kona ya dunia
 
Back
Top Bottom