KING MIDAS
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 8,589
- 16,936
Taarifa mbaya sana hii kwa Malaria 2 , Lucas Mwashambwa, MamaSamia2025 , ChawaWaMama na mapepo wengine wanaofanana na haoMwakilishi sauti ya watanzania (club house) - Kaswahili Juma Kaswahili, amesema kuwa wanamuunga mkono Tundu Lissu tokea siku ya kwanza alipochaguliwa kuwa mwenyekiti wa CHADEMA, hivyo wanaangalia utaratibu jinsi wanavyoweza kuchanga Tsh Bilioni 1 ili zimsaidie Lissu katika kukijenga Chama nchini.
View attachment 3237760
Na zitachangwa haraka na mapema kuliko wanavyofikiri...Hata Bil 10 tutachanga tu kwa ajili ya kulikomboa taifa letu dhidi ya mkoloni mweusi CCM
Fikra zako zinaanzia kwenye paji lako la uso na kuishia kisogoni pako...Hawa ndugu wana ndoto mbaya sana ambazo ni za mdomoni tu!!Hawa jamaa huko nje wana maisha magumu lakini wanamdanganya mwenzao na kumfariji faraja za hovyo.Washindwe milioni 30 halafu waweze bilion!!Labda kwa miujiza
Hekima ya mtu hupinwa kwa maneno na matendo!!.Sio kila viatu size yenu!!Fikra zako zinaanzia kwenye paji lako la uso na kuishia kisogoni pako...
Hata hujui kuwa, kilichokuwa kinasubiriwa ni milango iliyozuia baraka ya ukombozi kufunguka tu kwa TL kuwa mwenyekiti na tayari imefunguka...
Kama hujawahi kusikia na kuona kuwa mwamba (jiwe) linaweza kutiririsha maji safi ya kunywa na kumwagilia mashamba na kunywesha ardhi na mifugo, sasa UTAONA KWA MACHO YAKO...
Pesa zingine zitatoka huko huko kwa wana CCM na viongozi wa serikali yao...
Ndugu, Mwache Mungu aitwe Mungu maana njia zake, sio zako wewe mwanadamu na mawazo yake, kamwe sio kama yenu nyie wanadamu...!
Kama huamini kuwa hilo litakuwa, kaa hivyo hivyo hivyo na kutokuamini kwako lakini Mungu atabaki kuwa wa kuaminiwa daima na milele yote..!