SAUTI ya Watanzania na Maandamano ya Bila Kikomo - There is more Than one Way to Skin a Cat....

Mjinga wewe,

Hakuna chombo chenye uwezo wa kuua raia ml 60!!

Wauzie wajinga wenzio huo uoga.

Kudai HAKI imeruhusiwa kikatiba, polisi Hana ruhusa kuua raia yeyote.
nimekukanya vya kutosha jeuri yako utakula ukiwa hujiwezi na huna msaada
 
Maandamano tuwaachie TEC walioanduka waraka coz wao ndio wanajua wanafaidika vipi na hii nchi!!!

Sisi wa mtaani tubaki tukitafuta mkate wetu!
 
Kuhamasisha kondoo wapiganie haki zao ni kitu ngumu sana aloo!
 
Kwa Tanzania ninavyoijua unaweza kukuta wewe ni usalam@ umetumwa
 
Kwa Tanzania ninavyoijua unaweza kukuta wewe ni usalam@ umetumwa
Ni haki yangu vilevile na kama nipo kwenye ajira basi well and good (sababu nawajibika) ila kunipinga kwa hoja ni bora kuliko kwa shutuma...., na Ushauri ni Ushauri ambao mwingine anaweza kusema isiwe hivi na iwe vile.....,

In my humble upinion hatari hata ya Mtanzania mwenzangu mmoja kupata kovu (siwezi kuita huo ni ushindi iwapo kama ingewezekana kufanikisha bila hayo makovu)..., na mbaya zaidi walamba asali wana media (hence propaganda machines) kwahio huenda hata ile message nzuri ikawa diluted na propaganda na kusingiziwa ugaidi....., that's my two cents....
 
Hawa jamaa washauriwe au walazimishwe waachane kabisa na huo mpango wao wa kuhamasisha maandamano yasiyo na kikomo nchi nzima. Wala hakuna haja ya kuhamasisha wananchi kuvaa hizo T-shirts kama ulivyopendekeza. Sababu ni kama ifuatavyo:

- Kama lengo la hayo maandamano ni kufikisha ujumbe kwa serikali kwamba wanapinga huo mkataba wa DP World, mbona ujumbe huyo ulishafika kitambo serikalini?

- Kama lengo la hayo maandamano ni kuilazimisha serikali ijiondoe kwenye huo mkataba wa DP World, hilo haliwezekani na ni kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za utawala wa nchi. Hawana ubavu wa kuilazimisha serikali kwa jambo lo lote lile. Ni bunge tu ndilo lina ubavu huo lakini nalo utaratibu wake ni mugumu kwani linabidi lipige kura ya kutokuwa na imani na raisi. Kura hizo zikipita kwa theluthi mbili za bunge, raisi atalivunja hilo bunge na uchaguzi mkuu wa rais na wabunge utafanyika ambao kura za wananchi ndizo zitakazoamua.

- Vivyo hivyo pia kwa hawa waliokomalia kulazimisha katiba mpya. Tunawashauri wakomalie suala la wao kushika dola kupitia uchaguzi mkuu wa 2025. Wakifanikiwa kushika dola basi hiyo katiba mpya wanayoitaka wataileta wenyewe. Ni rahisi tu kuzingatia sheria na kanuni za nchi. Usipozingatia mkong'oto ukiupata usimulaumu mtu.

- Huyo Mwabukusi afuatilie tu hiyo rufaa ya hiyo kesi yao ya mkataba wa DP-WORLD huko Mahakama ya rufaa. Aachane na mambo ya uanaharakati.

- Huyo Mzee Dr Slaa atulie, ale pensheni yake ya ubalozi na atunze heshima yake. Kama anapenda kufanya siasa aanzishe chama chake cha siasa au ajiunge na mojawapo ya vyama vya siasa tulivyo navyo. Tunamshauri ajiunge na ACT wazalendo kama alivyofanya Maalim Sefu (RIP) walipomuzengua. Tunampenda sana Dr Slaa na tungalifurahi kumuona akiwa mgombea wa kiti cha uraisi 2025 kupitia chama cha ACT. Hapo mnyukano wa uchaguzi wa 2025 utakuwa umenoga wakipambana Mama Dr Salmia, Dr Slaa, Prof Lipumba na Dr Mbowe!
 
Wataanza lini kuandamana?
 
Ushauri wako hauna mashiko
 
Lengo ni kuonyesha kutoridhika kukubaliana na huo Mkataba / Makubaliano..., Hata mimi sikubaliani nao hata kila Watanzania wote wakikubali, naweza nikawepo / nikabaki mwenyewe ninakataa...., hivyo suggestion yangu ni kuonyesha kutoridhika..., Hata kama siwezi kuzima ukali wa joto la jua haimaanishi nitaacha kuwasha feni au kuongea kwamba jua leo ni kali
 
Akili nyepesi za harakati huwa zinatumiwa vilivyo na wanasiasa kwa manufaa yao. Huko USA walitengeneza fulana za kupinga kuuzwa bandari bila ya kuwa na uelewa wa kina wa kitu gani kinachokusudiwa kufanyika hapo TPA.

Zilipoanza kusambazwa barua za tender ya bandari kutafuta mwendeshaji mwenye uwezo baada ya kuwa IGA ilishapitishwa bungeni ndio baadhi ya hao wanaharakati wakaanza kugundua kuwa wanatumiwa na wapigaji wanaofaidika na uendeshaji wa bandari wenye mianya ya kuendeleza ufisadi!.

Kuna masuala mengi inabidi kwanza upate uelewa wa kina kuyahusu ndio uyapinge. Bandari ni fursa pana sana ya kiuchumi, kama mzalendo wa nchi hii anao ukaribu na makampuni ya kimataifa yenye uwezo wa kuendesha shughuli ya TPA hii ni fursa nzuri ya kutengeneza pesa kama alivyofanya Nazir Karamagi kwa mkataba wa TICTS miaka ile.

Unakula pesa yako ya malipo ya kazi ukiwa mwakilishi wa kampuni hapa nchini, unazeeka ukivuta kiko na kucheza golf pale Lugalo na Gymkhana. Unazeeka ukivuta pesa ya malipo yanayoingia kwenye kampuni yako iliyopewa tender ya uendeshaji wa TPA pale bandarini Dar, Bagamoyo au Tanga.
 
Kwamba huu Mkataba / Makubaliano ni Kosher..., Yaani hayana Dosari na kila anayepinga kapewa Mlungula na aliyekuwepo Kabla ?

Kama ndivyo kwanini tusiache na hawa wanaoona hii issue haipo vizuri na wao waeleze upande wao kama ilivyo haki yao kama walipa Kodi / Wananchi..., Kama vile CCM walivyokodi watu na kupita kwenye viwanja vya mipira wakitoa so called Elimu...,

I do Might not agree with what you have to say, but I'll defend to the death your right to say it.​
 
kwa hali tuliyofikia, kuandamana ni muhimu, maoni ya wananchi hayasikilizwi kabisa. Rejea katiba mpya ya wananchi inavyozungushwa, tume kadhaa zimechagiza mabadiliko ya sheria zetu, nani anafumba macho na kuziba masikio??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…