#COVID19 Sayansi inazidi kutokomeza Corona

Mh mkuu unajua kwamba huko kufungwa shule na kuzuia mikusanyiko kwenye michezo na sherehe ni hatua ambazo zilichukuliwa siku moja baada ya kupatikana kesi ya kwanza Tz ya mgonjwa wa corona?
 
Kila kitu tunajua sisi. Hayo mengine waachie wasiojua
 
Mh mkuu unajua kwamba huko kufungwa shule na kuzuia mikusanyiko kwenye michezo na sherehe ni hatua ambazo zilichukuliwa siku moja baada ya kupatikana kesi ya kwanza Tz ya mgonjwa wa corona?
Ile kwa mujibu wa serikali mkuu na uhakika corona ilikuwa imeshaingia muda mrefu, mwezi wa 11 watu wengi sana Dar walikuwa wanaumwa mafua ya ajabu na vifua sana tu ila corona haikuwa kihivyo katika media wengi walichukulia labda kuna upepo fulani unapita ilikuwa mafua na vifua vikali wakati inakuja kutangazwa ilikuwa imeshawapitia wengi sana kutokufahamu tu. turudi katika ile case ya kwanza tu kwa mujibu wao, mtu kawekwa quarantine, kapona huo ugonjwa kusambaa nchi nzima ulipita wapi? ndio maana jiulize mtu wa kwanza siku ya pili wakafunga kila kitu kweli tufunge sababu ya mtu mmoja? leo tunazika kila leo hawafungi. Yule hakuwa mtu wa kwanza ugonjwa ulianza Dar katika Nov na watu wa Dar mashahidi watu waliumwa sana miezi ile mpaka kufika wanafunga ugonjwa ulishafika kila kona ya nchi.
 
Issue sio hiyo case ya kwanza ya mgonjwa wa corona bali ni wewe kudai kwamba kulikuwa na vifo vingi mtaani na wagonjwa wengi mahospitalini,na kwamba hali hiyo ilikuja kupungua baada ya kufungwa mashule na hizo kumbi za starehe pamoja na michezo. Nachojua mimi mwaka juzi 2019 mwishoni ni kweli kulikuwa na mafua makali na vifua hata mimi niliumwa mafua makali sana,ila kuhusu vifo hakukuwa na wingi wa vifo kiasi cha kusema hadi palipozuiliwa mikusanyiko ndio vilipungua. Na pia hata ukiangalia takwimu za corona kipindi kile hali ilikuwa inaonesha kwamba maambukizi yanazidi kila siku hata huko baadaye serikali kuja kuanza kusema sijui corona inapungua ilikuwa ni kisiasa zaidi na ndio maana iliacha kutoa takwimu za corona kwa kila siku.
 
Mimi na wewe hatutofautiani sana katika hili, tatizo kubwa sana sio la kwetu hapa tutabaki na dhana kipi kilifanyika na kusaidia. Tatizo kubwa uwazi na uwazi ni serikali sababu ndio wana madaraka takukusanya takwimu. kwa bahati mbaya serikali hawakuwa wawazi issue ilishakuwa tatizo kabla nadhani muda ule vifo vingi tulifika peak sasa wakati tunatangaza mgonjwa wa kwanza na kuchukuwa hatua za kufunga ukweli ilikuwa ni peak, kosa lilifanyika siasa zikaingia tukapoteza mweleko na watumishi wakawa waoga kureport tatizo, dunia ika tuonya kuna second wave itakuja lazima tuchukuwe tahadhari. EA wakiwa wawazi na data zikawekwa tutajuwa je hii second wave imetupiga sana sisi TZ au hata wao hapo tutajuwa kama hatua zilisaidia au zinasaidia.
 
Tukizungumzia mwaka jana mie sioni kilichofanyika hata cha kuhisi tu ambacho ndio tutasena pengine hicho ndiyo kilisaidia kupunguza,maana kama nilivyosema kwamba tuliacha mapema sana kuzingatia njia za kujiking na corona na hivyo hata zile jitihada za watu kujiepusha na mikusanyiko zilipotea na hivyo watu wakawa wanakusanyana kama kawaida biashara ya barakoa ikadoda nayo.
 
Lakini tulionywa second wave inakuja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…