Sekondari za Vipaji maalum takribani miaka 40 tangu kuanzishwa kwake umaalum wake uko kwenye nini? Hatuoni ubunifu wowote

Tatizo la nchi yetu ni siasa kuingilia utaalamu,,kwa style hiyo kila kitu lazima kitaharibika.
Nchi kama German imepiga hatua kimaendeleo,kwa kuweka kipaumbele katika sayansi kwa kiwango cha juu, maana mwanasayansi huwa amenyooka mda wote hana blablaa,nyeupe ni nyeupe tu,uwezi sema ni nyeusi.
 


Tatizo sio shule bali waliozianzisha ndio ambao akili zao zinatia mashaka .
Huwezi kuanzisha vipaji maalumu bila kulenga ugunduzi na teknolojia .
Tulitegemea pawe na shule za Vipaji maalumu zenye Maabara na workshop za ufundi na masuala ya ugunduzi na vipaji maalumu katika ubunifu na Computer.

Cha ajabu shule hizi ni za kukariri tu hesabu na sio vipaji vya ugunduzi . Wengi wao hawawezi hata kuchunga mwiko au hata kutengeneza jiko la mkaa achilia mbali Kutengeneza masufuria kama wazee wetu wa zamani .
Hata kufinyanga chungu hawawezi lakini wanauwezo wa kukariri na kupata alama A zote.

Shule za Vipaji maalumu zilitakiwa ziwe ni vipaji vya kuzaliwa na sio kukariri kama Koran tu.
Walitakiwa wapimwe kwa ujuzi usio wa kawaida na uelewa wa kuzaliwa kabla hata ya kuingia kwenye mitihani. Mfano mtoto mwenye uwezo wa kufanya hesabu ngumu kwa kichwa bila kuandika n.k.
Lakini hii ya ufaulu wa A haitatuletea Wagunduzi hata wa baiskeli achilia mbali Cherehani za Kidigitali.
 
Hata uchawa ni kipaji mkuu. Huoni wanavyozidi kuwa wavunifu?
 
Naelewa point yako.
 
Na sisi tuige mambo mazuri
 
Tuna sekondari nyingi kama
1. Ilboru Arusha
2. Msalato Girls Morogoro
3.Mzumbe Boys Morogoro
4.Kibaha Boys Pwani
5. Tabora girls na Tabora Boys.
Mkuu umeandika kwa uchungu sana aisee! Hizi sio shule za vipaji maalumu bali ni shule kwa ajili ya wanafunzi waliofanya vizuri. Kufaulu vizuri sio kipaji bali ni uamuzi wa mwanafunzi binafsi.......hata kilaza akiamua kukariri atafaulu vizuri. Kipaji ni kama vile kipaji cha kucheza mpira, kupiga gitaa, kuvumbua teknolojia mpya, n.k. Kufaulu vizuri masomo sio kipaji. Huo ni uwongooooooooooooo!
 
Mimi o-level nimesoma azania, miaka ile ukisikia azaboy ujue hicho kichwa cha moto, na nina washkaji zangu wamepiga kibaha na mzumbe. Hawa wanafunzi wanaotoka shule za vipaji maalumu wale finest wengi wao huwa wanapata scholarship za kwenda nje, kutokana na uchumi wa bongo wa tia maji tia maji huwa wanaamua kufanya kazi na kuishi uko uko.

Kuna wengine huwa wanachukuliwa na mashirika ya kimataifa ndio maana hapa bongo huwa wanabaki wachache sana kiasi kwamba hatuoni impact yao. Halafu watu waliosoma wana ustaarabu fulani hivi kiasi kwamba hata akiwa anafanya mambo makubwa anakua humble tofauti na ambao hawajasoma wanakuaga na show-offs nyingi sana kwaiyo ni rahisi kuonekana. Ndio maana hawa wanaotoka vipaji maalumu wengi hatujui wako wapi na wanafanya nini.

Lakini wapo na wanafanya vizuri tu nina washkaji zangu nimesoma nao azania kuna mmoja daktari anaishi newcastle, uingereza. Mwingine lecturer wa compyuta sayansi anafundisha chuo ujerumani, mifano ipo mingi wengi wapo nje na kwenye mashirika ya kimataifa
 
Asante kwa maelezo ya kina Ndugu Natafuta Ajira.
Umetaja Lecturer na Daktari hata huku wapo.

Mada hii ilikuwa inajielekeza zaidi kwenye ubunifu ili kuendana na hadi ya Neno "Kipaji Maalum"
 
TPaul nakubaliana na wewe. Kufaulu vizuri ni utashi wa Mwanafunzi na mazingira kidogo wezeshi.
 
Huko umeenda chini kabisa je umewahi kujiuliza SUA imekusaidia nini licha ya kuwa ni chuo kikubwa na cha muda mrefu hadi sasa? Je umenufaika nacho nini?
 
Waliosoma hizo shule wengi wao sasa hivi wanaonyesha vipaji vya uchawa Pro max
 
Duh!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…