Sengerema: Viongozi wapigwa chini kwa kukusanya mchango wa ujenzi wa zahanati kwa lazima

Sengerema: Viongozi wapigwa chini kwa kukusanya mchango wa ujenzi wa zahanati kwa lazima

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Ummy Mwalimu amewasimamisha kazi Mtendaji wa kijiji cha Nyamililo Wilayani Sengerema Mariamu Mgunda, pamoja na mwenyekiti wa Kijiji hicho Mateso Shibayi na kuwaweka ndani kwa kosa la kuchangisha kwa nguvu fedha za ujenzi wa jengo la Zahanati.

mtendaji%20na%20mwenzake.jpg

Mariamu Mgunda ambaye ni mtendaji wa kijiji cha Nyamlilio wilayani Sengerema Mkoa wa Mwanza pamoja na mwenyekiti Mateso Shibayi.

Agizo hilo amelitoa akiwa ziarani mkoani humo, baada ya wananchi kulalamikia mambo wanayofanyiwa na viongozi hao ikiwamo kukamata mifugo kwa kushindwa kutoa mchango.

Baada ya malalamiko hayo, Ummy ameagiza watendaji wote wa vijiji na kata nchi nzima wasichangishe fedha kwa wananchi bila kibali kutoka kwa mkuu wa wilaya husikia.

Akijibu malalamiko hayo, mtendaji Mariamu Mugunda amesema michango hiyo walikubalina na wananchi kupitia vikao vyote vya kijiji hicho na hajaenda kinyume na utaratibu.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Robert Gabriey amesema atafanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo na atakayebainika atafikishwa Mahakamani
 
Tuchangie ila sio kwa nguvu...mpaka inafikia kukamata mali na mifugo sio sawa kabisa.

Serekali yenyewe inalalamika haina hela sembuse wananchi?
 
Tuliambiwa zahanati zitajengwa kwa tozo ya uzalendo, eboo!
 
Mbona hujaandika kuwa viongozi hao wa kijiji walichangisha pesa za kukamilisha ejenzi wa Zahanati wakati Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI ilikuwa imeshapeleka pesa za kukamilisha ujenzi wa Zahanati hiyo, kiasi cha Tsh milioni 50?
Taarifa yako imeakaa kinafiki sana!
 
Yani huu ndiyo upuuzi ambao watu wenye akili timamu hatuutaki.Haiwezekani wanakijiji wanyanyaswe hivyo hadi aje waziri kutoka Dodoma ndio awaokoe.Mkuu wa wilaya alikuwa wap? mtendaji wa kata hakulijua? Mkuu wa mkoa hakulijua? Kwa hiyo Ummy asingekwenda huko ina maana wananchi wangeendelea kunyanyaswa? Waliotakiwa kuwajibishwa siyo hao bali Wakubwa zao.
 
Yani huu ndiyo upuuzi ambao watu wenye akili timamu hatuutaki.Haiwezekani wanakijiji wanyanyaswe hivyo hadi aje waziri kutoka Dodoma ndio awaokoe.Mkuu wa wilaya alikuwa wap? mtendaji wa kata hakulijua? Mkuu wa mkoa hakulijua? Kwa hiyo Ummy asingekwenda huko ina maana wananchi wangeendelea kunyanyaswa? Waliotakiwa kuwajibishwa siyo hao bali Wakubwa zao.
Iko hivi, hao wote uliowataja ndio huwaambia hao watendaji kwamba serikali imeshaleta hela kwahiyo watendaji ndo watajua wanamaliziaje hizo miradi ( Kwa kigezo cha asilimia za wananchi) . ( Option inayobaki ni Kwa watendaji na wenyeviti Kuwabana wananchi).
Ila Sasa inapotokea kwenye ziara ya mkubwa Kama hivyo Nani anakubali kuaibika mwananchi Kama huyo anapolalamika sababu hiyo michango hata ningekuwa Mimi kutoa ni inshu. Nguvu hutumika kukusanya. Zigo humuangukia Mtumishi wa chini Kama Mtendaji.

Wengine wote wataruka lakini wanajua fika nini kinaendelea na wakati mwingine ni maagizo Yao. Ndio maana huwa nasema watumishi wa chini wasikubali kutekeleza maagizo ya mdomo( Siku hizi maarufu Kama matamko) zaidi ya maandishi, Bora uonekane Una kiburi Ila taka maandishi Kwanza. Hasa hasa huko Local G.
 
Back
Top Bottom