Sensa 2022: Zoezi linavyoendelea na yanayojiri

Sensa 2022: Zoezi linavyoendelea na yanayojiri

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Tarehe 23 Agosti ni siku rasmi ya kuanza zoezi la kuhesabu idadi ya Watu waliopo ndani ya mipaka ya nchi yetu. Zoezi hili limeandaliwa kwa umakini mkubwa tena kwa muda mrefu hivyo kutoa nafasi ya kufanya majaribio mbalimbali na kutatua changamoto na hata kuweka utaratibu mzuri wa kuliendesha zoezi hili la Sensa ya watu na makazi kisasa zaidi.

Serikali imewekeza bajeti kubwa kwenye eneo hili na kizuri zaidi ni kutoa nafasi ya ajira za muda kwenye zoezi hili ambapo makarani walipata mafunzo muhimu ili kufanikisha zoezi hili.

Zoezi limeanza na tumeambiwa na waandaaji kwamba litachukua siku saba mfululizo tangu kuanza kwake. Hivyo kinachoendelea mtaani sasa ni ukusanyaji wa taarifa za watu na makazi kwenye maeneo mbalimbali. Lakini kama tufahamuvyo, kila jambo linalopangwa na wanadamu lina pande mbili yaani mafanikio na changamoto.

lengo la uzi huu ni kuisaidia Serikali kusikia kutoka kwa wananchi endapo kuna changamoto zozote wanazokumbana nazo kwenye hili zoezi. Ninaamini kwamba watendaji mbalimbali wanapitia humu na inawezekana kupitia thread hii wakapata kufahamu nini kinajiri na hatua za haraka kurekebisha kasoro hizo zikachukuliwa.

Ninawasilisha changamoto moja kutoka Kata ya Toangoma wilaya ya Temeke niliyoipata usiku huu kupitia kwa rafiki aliyepo eneo hilo.
  1. Wakazi wa eneo la NSSF Estate wanalalamikia kwamba karani wa zoezi hilo ambaye ni mkazi mwenzao amewakabidhi vijana wa mtaani wasio na mafunzo wala vitambulisho kusambaza karatasi za kukusanya dodoso la wakazi kila nyumba ya eneo hilo
  2. Karani huyo hajatoa maelekezo namna ya ujazaji wa form hizo za kukusanya taarifa binafsi za mkazi
  3. Kuna uwezekano taarifa zitakazotoka eneo hilo zisiwe sahihi kama serikali inavyotarajia
Naamini wahusika wameelewa na wanaweza kutatua ama kufuatilia taarifa hizi kwa usahihi wake
 
Saa nane na dakika 12 usiku 24 August 2022 mimi na watu wa nyumba yangu tuko kwenye mkesha na thermos yetu ya kahawa tukiwangoja makarani wa sensa tupugie nao picha tutupie kwenye uzi wa Mshana Jr
Nawasubiri
IMG_20220824_025932_687.jpg
 
Mimi nimeshiriki sensa tatu nafikiri, lakini sensa hii ni ya ubabaishaji tu na si vinginevyo.

Sensa kama sensa ni zoezi la kuhesabu watu na linafanyika tangu enzi za Manabii, hata Yesu alizaliwa siku ya sensa wakati mama yake na Yoseph wamerudi kwao kwenda kuhesabiwa.

Mimi ninavyojuwa tuna ofisini ya takwimu ipo siku zote hii ndio ingehusika na kazi ya kukusanya hizo takwimu zao lakini siyo kulazimisha kufanya sensa ya watu na takwimu Kwa wakati mmoja, kaya moja kupata details zake sio chini ya nusu saa.

Hawa vijana wasiokuwa na ajira ndio wangepewa hizi kazi za kukusanya takwimu ili kuounguza tatizo la ajira na sensa huwa inafanyika siku moja tu, malengo ya sensa huwa ni kupata idadi ya watu, rika na jinsia au ulemavu tu, kama sensa wanaingiza na mambo ya takwimu ni Kwa nini kipengele cha dini hawakitaki?
 
Mimi nimeshiriki sensa tatu nafikiri, lakini sensa hii ni ya ubabaishaji tu na si vinginevyo.

Sensa kama sensa ni zoezi la kuhesabu watu na linafanyika tangu enzi za Manabii, hata Yesu alizaliwa siku ya sensa wakati mama take na Yoseph wamerudi kwao kwenda kuhesabiwa...

Sensa inapewa promo kichizi
 
Tarehe 23 Agosti ni siku rasmi ya kuanza zoezi la kuhesabu idadi ya Watu waliopo ndani ya mipaka ya nchi yetu. Zoezi hili limeandaliwa ...
Bilashaka hawakufanya Bure,huenda nao Kwa mbaaali wameonja kachembe la Ile keki ya taifa🏃
 
Mimi nimeshiriki sensa tatu nafikiri, lakini sensa hii ni ya ubabaishaji tu na si vinginevyo.

Sensa kama sensa ni zoezi la kuhesabu watu na linafanyika tangu enzi za Manabii, hata Yesu alizaliwa siku ya sensa wakati mama take na Yoseph wamerudi kwao kwenda kuhesabiwa...
Inastaajabisha, hoja aliyoitoa Mwl nayo ilikuwa dhaifu ni kama kulikuwa na hofu nyuma yake, suala la dini kwenye mipango ya maendeleo lina tija
 
Baadhi ya watz walivyo serious na sensa Yan mpaka nmeshangaa, Yan ety mtu kabisa unaacha kufanya kazi /biashara yako ety kisa sensa.
 
Sidhani kama wanapewa taarifa zote kwa usahihi!!
Tanzania bado sana
 
Miaka kumi ijayo wenyeviti wa mitaa wafanye zoezi hili la kuhesabu watu na makazi wanaweza kufanya vizuri zaidi.
 
Back
Top Bottom