Gamba la Nyoka
JF-Expert Member
- May 1, 2007
- 7,036
- 9,331
Issue sio ubaguzi ni uwezeshaji.
. Kwenu nyie wakina Mkono, Tenga, IMMA ni bora mara kumi ya Issa Shivji kwa sababu tu ni wazawa!
FM,
Hapa ndipo unapotosha mjadala,hatujasema kuwa watanzania wenye asili ya uhindini wabaguliwe, kinachotakiwa ni kuwawezesha watanzania wazawa ili nao waweze kufanikiwa ingawa hawawezi kuwa wote, kama ilivyo sio watanzania waasia wote wenye hali nzuri.Lakini ni ukweli usiopingika kuwa watanzania weusi wengi ndio wana hali mbaya kiuchumi na kimaendeleo.Najua wapo weusi wachache wamefanikiwa sasa hiyo isiwe kigezo kuwa mbona mengi amefanikiwa na yeye atahitaji kuwa empowered.Hapa tunazungumzia kundi kubwa la watu walio nyuma sana kimaendeleo na kiuchumi.Na kwa kufanya hivyo haitakuwa na maana kuwa tunawabagua waliofanikiwa, lengo litakuwa kuwawezesha hawa wanyonge ili waweze kupiga hatua pasipo kuathiri hao waliofanikiwa.
Na labda nikukumbushe kuwa hao akina rakesh rajani, Prof. Issa shivji tayari wao ni watu waliofanikiwa wako kundi moja na akina mzee mengi na wengineo, kwahiyo hawahitaji kuwa empowered.
Suala la Mkono, IMMA, Tenga kuwa bora kuliko akina Shivji ni mawazo yako na mtazamo wako tu lakini hakuna mahali popote tumesema hivyo.
Na hata hivyo hao wote ni watu ambao wamefanikiwa iwe ni kwa njia ya haki au kwa haramu(kitunambacho hatukijadili hapa), maana najua wabongo wengi tuna bifu na utajiri wa mkono na ufisadi wa deep green ikihusishwa na IMMA.
Hivi fundi nikuulize swali, mbona hampigi kelele kupinga akina mama kupewa upendeleo kwa kupewa viti maalum vya ubunge na udiwani?mbona hampigi kelele kupinga akina mama kupewa upendeleo ili waweze kusomea kozi za uhandisi na sayansi vyuo vikuu baada ya kuonekana kuna uhaba wa wataalam wanawake kwenye nyanja hiyo???na ni kwa nini basi mgeuze suala muhimu la kuwawezesha wazawa maskini kuwa ni ubaguzi???mnataka waendelee kuwa maskini milele.Kama wewe umefanikiwa haina maana kuwa lazima na wengine wahangaike kama wewe ili wafanikiwe, watu wametofautiana uwezo, ndio sababu hata marehemu JKN alianzisha utaratibu wa kiweka viwango tofauti vya ufaulu kwenda shule za sekondari ili kuwainua wale walio kuwa nyuma kielimu, na ndipo na sie tuliokuwa tunachunga ng'ombe huko porini serengeti tukapata nafasi za kusoma hadi hivi leo tumeweza kujua kubofya kwenye key board na tukasomeka.
FM,
Hii sera hata mie kwa USA naona imepitwa na Wakati. Tumemuona Powel, Rice na sasa Obama. Ila siyo siri, imeinua wengi sana USA. Unaweza kukataa au kukubali ila huo ndiyo ukweli kama ulivyoandika hapo nimeweka rangi. Hata Tanzania inaweza kuwekwa kwa miaka kadhaa na baadaye ife. Kuna vitu vingine huwa vya mpito na lazima kifanyike kwa muda, na baadaye wakishaamka kundi la matajiri wafanya biashara, mpango unakufa. Hata Tanzania leo shule unalipia. Shida kubwa kwa Watz kwa sasa ni kutokujua kufanya biashara. Wenzetu Wahindi na Waarabu uongo mbaya, hawajambo. Jamani kuwaamsha Weusi kadhaa hiyo ni UBAGUZI? Wacheni hiyo.
Kwanza mwajua ubaguzi ninini? Mmeshauona ubaguzi lakini au mwasikia? Mnafikiri sisi tunasema Mhindi apigwe na Black skinhead? Akae nyuma ya basi, asiruhusiwe kusoma na sisi, tumtenge hadi AKOME!!!! Mhhh, mwaenda mbali nyie watu? Ukitaka kukamua jipu, huu ndiyo ubaguzi positive.
. Kwenu nyie wakina Mkono, Tenga, IMMA ni bora mara kumi ya Issa Shivji kwa sababu tu ni wazawa!
FM,
Hapa ndipo unapotosha mjadala,hatujasema kuwa watanzania wenye asili ya uhindini wabaguliwe, kinachotakiwa ni kuwawezesha watanzania wazawa ili nao waweze kufanikiwa ingawa hawawezi kuwa wote, kama ilivyo sio watanzania waasia wote wenye hali nzuri.Lakini ni ukweli usiopingika kuwa watanzania weusi wengi ndio wana hali mbaya kiuchumi na kimaendeleo.Najua wapo weusi wachache wamefanikiwa sasa hiyo isiwe kigezo kuwa mbona mengi amefanikiwa na yeye atahitaji kuwa empowered.Hapa tunazungumzia kundi kubwa la watu walio nyuma sana kimaendeleo na kiuchumi.Na kwa kufanya hivyo haitakuwa na maana kuwa tunawabagua waliofanikiwa, lengo litakuwa kuwawezesha hawa wanyonge ili waweze kupiga hatua pasipo kuathiri hao waliofanikiwa.
Na labda nikukumbushe kuwa hao akina rakesh rajani, Prof. Issa shivji tayari wao ni watu waliofanikiwa wako kundi moja na akina mzee mengi na wengineo, kwahiyo hawahitaji kuwa empowered.
Suala la Mkono, IMMA, Tenga kuwa bora kuliko akina Shivji ni mawazo yako na mtazamo wako tu lakini hakuna mahali popote tumesema hivyo.
Na hata hivyo hao wote ni watu ambao wamefanikiwa iwe ni kwa njia ya haki au kwa haramu(kitunambacho hatukijadili hapa), maana najua wabongo wengi tuna bifu na utajiri wa mkono na ufisadi wa deep green ikihusishwa na IMMA.
Hivi fundi nikuulize swali, mbona hampigi kelele kupinga akina mama kupewa upendeleo kwa kupewa viti maalum vya ubunge na udiwani?mbona hampigi kelele kupinga akina mama kupewa upendeleo ili waweze kusomea kozi za uhandisi na sayansi vyuo vikuu baada ya kuonekana kuna uhaba wa wataalam wanawake kwenye nyanja hiyo???na ni kwa nini basi mgeuze suala muhimu la kuwawezesha wazawa maskini kuwa ni ubaguzi???mnataka waendelee kuwa maskini milele.Kama wewe umefanikiwa haina maana kuwa lazima na wengine wahangaike kama wewe ili wafanikiwe, watu wametofautiana uwezo, ndio sababu hata marehemu JKN alianzisha utaratibu wa kiweka viwango tofauti vya ufaulu kwenda shule za sekondari ili kuwainua wale walio kuwa nyuma kielimu, na ndipo na sie tuliokuwa tunachunga ng'ombe huko porini serengeti tukapata nafasi za kusoma hadi hivi leo tumeweza kujua kubofya kwenye key board na tukasomeka.
Sipotoshi bali natamka mnachokataa kutamka.
Hauwezi kulinganisha upendeleo wanaopewa wanawake na huu mnaoudai. Wanawake katika jamii wanayimwa haki kutokana na tamaduni (jamii kuona wao hawako sawa na wanaume). Wanawake hawana uwakilishi unaolingana na wingi wao katika sehemu zote za maamuzi ya nchi. Kuanzia serikali, mahakama n.k. Wanawake wananyimwa haki na baadhi yetu hata ya kumchagua wanaemtaka kwa kuambiwa ni lazima wafuate mfano wa mume wao. Wangapi katika jamii yetu wanaona ni kupoteza pesa kusomesha mwananmke? Ni wangapi katika jamii yetu tunaona ni halali kumfanyisha kazi za kitwana binti kwa kisingizio cha kumfundisha wajibu wake atakapokuwa wakati wavulana tunawaachia wafanye watakalo? Na hao hao wanawake wakizeeka na kupata Alzheimer, hatuchelei kuwatenga na wakati mwingine hata kuwauwa kwa kusingizia ni wanga! Zote hizi na nyingine nyingi tu ndizo zinazotoa ulazima wa mwanamke na yule mwenye ulemavu kupewa upendeleo. Mpaka hapo sisi ( wanaume wasio na ulemavu) tulio na nguvu katika jamii tutakapowaona kuwa kweli wanastahili haki sawa na sisi, upendeleo itabidi uendelee.
Amandla.......
Quote: FM
1. Sera zote zilizowekwa baada ya uhuru zilikuwa na nia ya kumwinua mtanzania mweusi bila ya kumtenga mwingine.
2. Shule zilizokuwa zikiwabagua zilitaifishwa na watu wote kupewa nafasi ya kusoma BURE. Biashara zilizokuwa zikimilikiwa kwa kiasi kikubwa na wasio weusi, zilitaifishwa, na watu weusi kuwekwa kuziendesha.
3. Maghorofa yaliyokuwa yakimilikiwa na watu wasio weusi yalitaifishwa na watu weusi kupewa kipaumbele katika kupanga humo. Yote haya yalifanywa bila ya kuwa na sera ya uzawa maana ilijulikana ukimlenga mtanzania wa kawaida, sehemu kubwa mno itakuwa ni weusi.
4. Sasa mtuambie, ni kipi kigeni ambacho sera yenu ya kibaguzi itafanya ambacho hakijajaribiwa kama sio kuhalalisha ubaguzi dhidi ya mtanzania mwenzetu?
Wadau ,wachangiaji wengi hapa wanalinganisha uzawa na ubaguzi, versus uwezeshaji wa waTanzania.Nafikiriri hii argument ukiichukua namna hii in three dimensions si rahisi kupata jibu la matatizo yetu waTanzania.
Ubaguzi utabaki kuwa ubaguzi dhambi ambayo tumeikana siku nyingi.
Hata hivyo suala la uwezeshaji wa watanzania litabaki kuwa pale pale.Hatuna mjomba wa kutuendeleza,kama tulijaribu tukashindwa ni vema tuka analyse tulishindwa wapi na tundelee wapi katika kuwawezesha watanzania.
Admitting to failure and doing nothing anbout it is much worse, nikama kukubali kurudi utumwani kwa sababu ati umeshindwa kujiendesha .We must try, we may fail, but we must try again.
Sera ya uzawa kwa maana ya kuwapendelea weusi ni sera ya Kirundi ya miaka ya nyuma hukooo....ambayo iliwapendlea Watusi katika masuala ya elimu na biashara na kuwaacha Wahutu wakiwa watumishi wasiokuwa na hadhi.Hii ni aina ya ubaguzi ambayo Simba alitaka ifuatwe.
Simba aliona jinsi ilivyowainua Watusi wa huko kwao na akadhani itakuwa na matokeo mazuri hapa Tanzania.Ubaguzi wa aina yoyote ni ubaguzi tu.Ukianza kuwabagua watu kwa rangi zao au pua zao utakuwa unazalisha chuki.Baada ya vita na maafa Burundi iliachana na sera hiyo na sasa Warundi wote wana fursa ya kujiendeleza bila ubaguzi.
"Hata kama rangi ya ngozi yako ni nyeusi lakini una mawazo ya kikaburu, basi hatutokuonea haya!, kwani wewe ni kaburu tu!"-Mwalimu Nyerere alitamka haya baada ya Simba and Company kutaka kuleta sera za uzawa...
Badala ya kulalama dhidi ya wenzetu, tujifunze kutoka kwao. Wakati tunalalamika kuwa hatuna uwezo wa kujikwamua, tunaendelea kuendekeza michango isiyo na manufaa kwa jamii. Kama tungetumia muda na resources tunazoweka kwenye harusi, kitchen party, kuvunja vikao, kubarikiwa watoto, misiba ( si kuuguza) n.k. tungekuwa mbali. Tuko tayari kukaa na kuingia gharama ya vikao vya mwaka mzima ili kuhakikisha kuwa mwanetu anaoa au kuolewa kwa mbwembwe! Mapesa yote tunayokusanya tunapelekea kuhakikisha kuwa waalikwa na wasio alikwa wanakunywa na kusaza. Ni mara chache sana sehemu ya michango hiyo imepelekwa katika kuwawezesha mahurusi katika maisha yao mapya. Tukijitahidi ni kafriji lakini hata siku moja hatusemi hizi ni ada ya shule ili ujiendeleza, mtaji wa kununua/kupanga sehemu ya kufanyia biashara. Hapana, sisi ni kunywa na kula tu! Mara ngapi tumeweka vikao vya kuwatafutia ada watoto wetu? Mara ngapi tumekaa vikao vya kuchangia tiba ya mwenzetu? Hata hapo tukikaa kuchangia tiba, michango yake hata siku moja hailingani na ile ya kwenye harusi!
Mara ngapi sisi tulionazo tumejenga madarasa au kuezeka shule zilizo jirani yetu? wa ngapi katika sisi tulioenda katika vituo vya watoto yatima na ku-adopt mmoja wao? Ni wangapi, huko tunakotoka tumefanya juhudi za kuleta tofauti katika maisha yao? Wangapi, tukiwa likizo, tunajitolea kutoa ushauri, kufundisha, kujenga bure kwa wale tuliowazidi?
Wenzetu yote haya (kupeana mitaji n.k.) wanafanya kwa jamii yao. Kwa nini tusiwaige badala ya kutaka serikali yetu wote iwatilie kauzibe?
Uwezo wa kujikomboa tunao na wala hatuhitaji upendeleo. Tunachohitaji ni kufungua macho na kuanza kujiamini katika tunachokifanya. Ni hicho tu.
Amandla......
Badala ya kulalama dhidi ya wenzetu, tujifunze kutoka kwao. Wakati tunalalamika kuwa hatuna uwezo wa kujikwamua, tunaendelea kuendekeza michango isiyo na manufaa kwa jamii. Kama tungetumia muda na resources tunazoweka kwenye harusi, kitchen party, kuvunja vikao, kubarikiwa watoto, misiba ( si kuuguza) n.k. tungekuwa mbali. Tuko tayari kukaa na kuingia gharama ya vikao vya mwaka mzima ili kuhakikisha kuwa mwanetu anaoa au kuolewa kwa mbwembwe! Mapesa yote tunayokusanya tunapelekea kuhakikisha kuwa waalikwa na wasio alikwa wanakunywa na kusaza. Ni mara chache sana sehemu ya michango hiyo imepelekwa katika kuwawezesha mahurusi katika maisha yao mapya. Tukijitahidi ni kafriji lakini hata siku moja hatusemi hizi ni ada ya shule ili ujiendeleza, mtaji wa kununua/kupanga sehemu ya kufanyia biashara. Hapana, sisi ni kunywa na kula tu! Mara ngapi tumeweka vikao vya kuwatafutia ada watoto wetu? Mara ngapi tumekaa vikao vya kuchangia tiba ya mwenzetu? Hata hapo tukikaa kuchangia tiba, michango yake hata siku moja hailingani na ile ya kwenye harusi!
Mara ngapi sisi tulionazo tumejenga madarasa au kuezeka shule zilizo jirani yetu? wa ngapi katika sisi tulioenda katika vituo vya watoto yatima na ku-adopt mmoja wao? Ni wangapi, huko tunakotoka tumefanya juhudi za kuleta tofauti katika maisha yao? Wangapi, tukiwa likizo, tunajitolea kutoa ushauri, kufundisha, kujenga bure kwa wale tuliowazidi?
Wenzetu yote haya (kupeana mitaji n.k.) wanafanya kwa jamii yao. Kwa nini tusiwaige badala ya kutaka serikali yetu wote iwatilie kauzibe?
Uwezo wa kujikomboa tunao na wala hatuhitaji upendeleo. Tunachohitaji ni kufungua macho na kuanza kujiamini katika tunachokifanya. Ni hicho tu.
Amandla......
Fundi,
hapo ndipo nasema unajaribu kupotosha mjadala.Hatujasema popote kwamba hao waliofanikiwa wawekewe kauzibe hata kidogo, wataendelea kujipambanua kama kawaida. Halafu unajadili hii mada kama vile hakuna wazawa ambao ni weusi na wana hali bora, badala yake unajaribu kulazimisha kuwa tunawabagua weupe.
Hivi fundi unataka kutuambia kuwa hao wazungu unaotaka tujifunze kutoka kwao hawaoi na kuolewa?unataka kutuambia kwamba tatizo la watanzania ni elimu?hawajasoma?unataka kutuambia kuwa hao wote waliofanikiwa kiuchumi wamesoma sana kuliko hao waswahili wasiofanikiwa?haiwezekani hata kidogo.
Fundi, je ni mara ngapi hao wenzetu waliofanikiwa wamekwenda kwenye hivyo vituo vya watoto yatima na ku-adopt walau mmoja?madona si katoka zake marekani akaja ku-adopt mnyasa na bado mkamshutumu baba wa mtoto?
Suala la kuchangia harusi, misiba, kitchen party, vipaimara n.k vinafanywa na kila mtu awe anazo au hana.Sasa kama mtu anaoa au anaolewa wanajamii wenzake wakaamua wamsaidie angalau friji ili apate maji ya kunywa ya baridi wewe unaona nongwa?Tunapozungumzia uwezeshwaji lazima tuangalie ukweli wa mambo tusiishie kutoa mifano ambayo inaendelea kutufunika macho, tusijikite katika nadharia wakati hali halisi inaonyesha watanzania wengi ni maskini wa kutupwa.
Je unaweza kujua ni wakulima wangapi wameweza kukopesheka kutoka katika taasisi zetu za kifedha?je ni watu gani wanaoendelea kuhangaika na kilimo cha jembe la mkono huku wakitegemea kudra za mwenyezi Mungu alete mvua
ndipo wapate angalau mavuno ya kuwakidhi kwa kipindi kifupi?ni akina nani wanaofaidika na mikopo kutoka taasisi za fedha kama sio hao hao waliofanikiwa?je huoni kuwa kuna umuhimu wa kuwawezesha hawa wakulima wasiokopesheka ili wajinasue kutoka lindi la umaskini?Ulishawahi kuwaona hao wenzetu wako barabarani wanaombaomba?Juzi juzi hapa katibu tawala wa mkoa wa Dodoma aligoma kuwapokea ombaomba waliokuwa wamerudishwa dodoma toka dar es salaam, huoni kuwa watu kama wale wanahitaji kusaidiwa?na hukuona kuwa wote walikuwa mipingo kama anavyosema sikonge?
Swali la mwisho kwenu mnaopinga wazawa kuwezeshwa, je mmefanya nini kuwasaidia au kuwawezesha hao wenzenu wasiokuwa na uhakika wa mlo hata mmoja?au kwakuwa mmefanikiwa mnataka muendelee kuwa peke yenu ili muendelee kusujudiwa?
[/FONT]
Fundi mbona unaikimbia hoja?wewe si uliuliza kama tumewahi kusaidia watoto yatima walau hata kwa ku-adopt mmoja?Nikakujibu kuwa hako kaugonjwa ka kutowathamini tunako wote, nikakuambia alikwenda madona malawi aka-adopt mtoto mkaishia kumbeza baba yake david banda.
Nikawaomba nyie mnaotulaumu mtwambie mmeisaidiaje jamii, sasa unaposema kuwa kwa kuwa sikujui kwahiyo ukiniambia haitasaidia kitu unakosea sana.Kwa sababu tangu nijiunge hapa JF simjui mtu yeyote na tumekuwa tukijadiliana mambo mengi hapa ilihali hatujuani.Kwahiyo fundi huo utetezi wako hauna mashiko, suala sio mimi kusaidiwa kitu bali hata kama mimi sitakuami(kitu ambacho sio sahihi) inawezekana kuna mtu hapa JF anakufahamu atathibitisha kwamba kweli hayo mambo umeyafanya kweli, na isitoshe sina sababu ya kutokukuamini au kukuamini kwa kuwa hapa tunajaribu kuelezea miatazamo yetu ambayo mara nyingi hutofautiana ingawa mwisho wa siku tutamaliza pamoja kwa kukubaliana au kutokubaliana na maisha yataendelea kama kawa.Kama kweli umewahi kuwasaidia wabongo wenzako sio mbaya ukitushirikisha pengine itasaidia sisi tusiokubaliana na mtazamo wako kubadili misimamo yetu na kuungana na wewe, lengo letu liwe ni kuwasaidia watanzania wote ili wafaidike na nchi yao bila kumuathiri mwingine.Ni hayo tu fundi.