Uchaguzi 2020 Sera ya Majimbo ndio mkombozi wa Taifa

Uchaguzi 2020 Sera ya Majimbo ndio mkombozi wa Taifa

Mimi ni muumini wa mabadiliko, Lakini hii sera ya majimbo sikubaliani nayo kwa kweli. Inaweza kuchangia kutugawa kama yanayoanza kujitokeza India ya kuanza mabifu baina ya state hii na hii, India kumeanza tension japo ni ndogo bado baina ya Maharashtra na Bihar tena mpaka kwa wananchi, na pia kudumazisha baadhi ya maeneo ambayo hayana resources nzuri za uzalishaji wa kuleta maendeleo.
Nakubwa kiupande wangu ni ile hali ya kila jimbo kuwa na sheria zake zakiutawala hilo ndio taizo kuu. Unaweza kukuta eneo la huku jimbo Fulani ni uhalifu eneo la huku siuhalifu. hapo nipo penye tatizo Sheria ikiwepo itumike kwa sote.

Ila Pia mikoa imekua ni mingi sana, inahitajika kupunguzwa sana, Nchi imeja ma RC na DC wasiokua nu uweledi wowote.

Ila bado naendelea kuwa na sababu Zaidi ya 100 Kura yangu kumpa Lissu
 
Mimi ni muumini wa mabadiliko, Lakini hii sera ya majimbo sikubaliani nayo kwa kweli. Inaweza kuchangia kutugawa kama yanayoanza kujitokeza India ya kuanza mabifu baina ya state hii na hii, India kumeanza tension japo ni ndogo bado baina ya Maharashtra na Bihar tena mpaka kwa wananchi, na pia kudumazisha baadhi ya maeneo ambayo hayana resources nzuri za uzalishaji wa kuleta maendeleo.
Nakubwa kiupande wangu ni ile hali ya kila jimbo kuwa na sheria zake zakiutawala hilo ndio taizo kuu. Unaweza kukuta eneo la huku jimbo Fulani ni uhalifu eneo la huku siuhalifu. hapo nipo penye tatizo Sheria ikiwepo itumike kwa sote.

Ila Pia mikoa imekua ni mingi sana, inahitajika kupunguzwa sana, Nchi imeja ma RC na DC wasiokua nu uweledi wowote.

Ila bado naendelea kuwa na sababu Zaidi ya 100 Kura yangu kumpa Lissu
Mkuu kupigana kupo tu bila majimbo. Kenya walipasuana kulikua na kaunti?(majimbo) kama tumeweza kuishi miaka yote toka tupate uhuru hatuwezi kupigana tena sababu kwanza tunaingiliana sana kwenye kuoa na makaaz pia
 
Kama sera ya majimbo ingekuwepo toka zamani ungekuta mikoa hii inafanana kimaendeleo au kuzidi mingine
Leo Mtwara isingekuwa chini kama ilivyo leo.
Kila miradi ya maendeleo inapelekwa Dodoma au Dar es Salaam ni lini Mikoa mingine itakuwa na wakaaz wake wafaidiks kiuchumi?
 
Mkuu, hii Sera ni Nzuri Ukiwa katika Jimbo, ama mkoa wenye Resources nyingi na kutoshereza kujiletea maendeleo, swali langu ni kwamba, Kwa kuwa mikoa yenye utajiri wa lasirimali za kutosha huwenda zisifikie hata mikoa 8, hiyo mikoa mingine wataweza kuvumilia umaskini Wao uliopo ktk mikoa Yao ukiwemo mkoa wa Singida anakotokea Raisi wa mitandaoni?

Sera ya majimbo, ni Nzuri Sana mkiwa na eneo kuuubwa la nchi, nchi yetu ni ndogo na inaweza kulinganishwa na Jimbo moja tu la Taxes Maerekani, maana yake Ni kwamba, Jimbo la Taxes, utajiri ulio katika Baadhi ya maeneo yake, huufunika umaskini wa maeneo mengine yasiyokuwa na utajiri wa rasilimali

Je, hapa, mtaigawaje hii nchi ili kwamba, Kwa mikoa hiyo isiyozidi minane iingizwe kwenye hayo majimbo hata yasiyokuwa na kitu ili sasa kuumeza huo umaskini wa mikoa zaidi ya ishirini+

Hata ukasema uigawe kikanda, Naihofia kanda ya Kati, Kwa kuwa mikoa yake ni myeupe na inakuwaga na njaa sana
Huwa kuna fomula ya kitaifa ya kugawana pesa za serikali kuu isiyolalamikiwa. Majimbo hayaondoi mpango wa kusawazisha maendeleo kitaifa. Hata hivyo hii si maana halisi ya sera ya majimbo ya CHADEMA ya leo. Maana yake ni ugatuzi wa madaraka ili Rais asizipangie wilaya apendavyo, na wakuu wa wilaya, DED, n.k. wapigiwe kura
 
Mkuu, hii Sera ni Nzuri Ukiwa katika Jimbo, ama mkoa wenye Resources nyingi na kutoshereza kujiletea maendeleo, swali langu ni kwamba, Kwa kuwa mikoa yenye utajiri wa lasirimali za kutosha huwenda zisifikie hata mikoa 8, hiyo mikoa mingine wataweza kuvumilia umaskini Wao uliopo ktk mikoa Yao ukiwemo mkoa wa Singida anakotokea Raisi wa mitandaoni?

Sera ya majimbo, ni Nzuri Sana mkiwa na eneo kuuubwa la nchi, nchi yetu ni ndogo na inaweza kulinganishwa na Jimbo moja tu la Taxes Maerekani, maana yake Ni kwamba, Jimbo la Taxes, utajiri ulio katika Baadhi ya maeneo yake, huufunika umaskini wa maeneo mengine yasiyokuwa na utajiri wa rasilimali

Je, hapa, mtaigawaje hii nchi ili kwamba, Kwa mikoa hiyo isiyozidi minane iingizwe kwenye hayo majimbo hata yasiyokuwa na kitu ili sasa kuumeza huo umaskini wa mikoa zaidi ya ishirini+

Hata ukasema uigawe kikanda, Naihofia kanda ya Kati, Kwa kuwa mikoa yake ni myeupe na inakuwaga na njaa sana
hakuna mkoa masikini tanzania hii narudia tena hakuna,hiyo singida unayoisema sio masikini hata kidogo umasikini wa singida unatokana na sera mbovu za nchi yetu,labda nikuulizi tunatumia trilion ngapi kuagiza mafuta ya kula nje ya nchi? Singida dodoma wana wanajiweza kwenye kilimo cha alizeti,karanga,ufuta mahindi vitunguu vya kulisha nchi nzima, leo unasema hawa watu masikini huo ni umasikini wa kufilika na kusababishiwa,tukishakuwa majimbo hutaenda kuzoa tu vitunguu singida kwa bei za bure,utavinunua kwenye masoko rasmi au vitasindikwa na kuongezewa thamani ndio uvipate kwa bei stahiki,kwa ufupi hakuna jimbo masikini Tanzania
 
hakuna mkoa masikini tanzania hii narudia tena hakuna,hiyo singida unayoisema sio masikini hata kidogo umasikini wa singida unatokana na sera mbovu za nchi yetu,labda nikuulizi tunatumia trilion ngapi kuagiza mafuta ya kula nje ya nchi? Singida dodoma wana wanajiweza kwenye kilimo cha alizeti,karanga,ufuta mahindi vitunguu vya kulisha nchi nzima, leo unasema hawa watu masikini huo ni umasikini wa kufilika na kusababishiwa,tukishakuwa majimbo hutaenda kuzoa tu vitunguu singida kwa bei za bure,utavinunua kwenye masoko rasmi au vitasindikwa na kuongezewa thamani ndio uvipate kwa bei stahiki,kwa ufupi hakuna jimbo masikini Tanzania
Mkuu, asante, labda nikuulize, Je hayo mazao Kutokea mikoa hiyo huwa yanakwenda wapi mpaka sasa,

Ndiyo, mikoa hiyo huwa inalima, lakini ni Kwa kiwango gani kilimo cha kutegamea mvua kimewahi kuondoa umaskini?

Huyo malaika wenu ameshuka na pesa za kuanzisha stimu za umwagiliaji hayo maeneo ili kumaliza umaskini ktk mikoa hiyo?

Halafu tunaposema mikoa masikini sio kwamba haina Aridhi yenye rutuba ya kilimo, maana yake Hata hiyo mikoa tunayosema inautajiri,inayopia Aridhi nzuri yenye kuzalisha mazao mbalimbali!

Kwa uelewa wako Wanatalaam wanaposema DRC Congo inautajiri wa matirioni katika rasilimali zake, huwa wanamaanisha ni Aridhi yenye rutuba inayoweza kutoa alizeti kama Singida?

Hivi ninyi wasomi wa Tanzania mnajifanya hamnazo siyo? Ndivyo mnavyomshauri huyo mbeligiji wenu kwamba Kwa kigezo cha Aridhi ya Singida kuzalisha alizeti maana yake Ni mkoa tajiri siyo?

Nairudia tena, mpango wa majimbo bila kuzingatia resources za maeneo husika ni kuleta uvunjifu wa Amani kama inavyoendelea Kutokea Naigeria!

Ni upumbavu Kwa nchi ndogo kama hii ambayo inalingana na Jimbo mojawapo la Marekani kuigawa kimajimbo, ni upumbavu kuwa Sera inayoondoa madini ktk umiliki wa majimbo na kuyafanya ndio kiendesheo cha serikali kuu, hii Ndiyo itakayomfanya Mbeligiji wenu asiweze kuiongoza hii nchi,

Hawatakubali wananchi wote wanaotokea maeneo ya madini, labda muwauwe wote haki ya nani ndio muweze kuwanyang'anya madini na kumpatia huyo mtakayempa Bondi

Na Ndiyo Maana kuna nguvu kubwa iliyonyuma ya huyo, kumbe madini yetu mtawapa wao Kwa kigezo cha Sera ya majimbo siyo?
 
Nani kakudanganya kuwa natural resources peke yake ndio zinaweza kuleta maendeleo? SINGIDA ambayo ndio mnaitumia kama kigezo,singida sio masikini hata kidogo kuna kilimo,ingawa kuna viongozi wetu wamekuwa wakitumia zaidi ya trion moja kila mwaka kuagiza mafuta ya kula nje,waimalishe kilimo cha alizeti wakose kidogodogo kinachotokana na waagizaji wa mafuta nje? tuache hilo,SINGIDA kuna maji moto pia upepo wa kutosha kuzalisha umeme mwingi ambao wanaweza kuuza kwenye mkondo wa umeme wa taifa,kuna madini aina 49 kati ya hayo ni dhahabu na madini ya jasi ndio zinachimbwa na kutumika,madini ya jasi yamekuwa yakitumika hovyo bila ya kuwa na tozo yoyote hadi hivi karibuni serikari iliposhituka jasi = gypsum hutumika kwenye utengenezaji wa simenti kwa miaka nenda rudi imechimbwa singida na wajanja wakijitwalia kwa bei wanazota.
Enyi walishwa matango komeni toka leo kusema singida ni masikini
 

Attachments

  • Opera Snapshot_2020-09-23_173033_www.singida.go.tz.png
    Opera Snapshot_2020-09-23_173033_www.singida.go.tz.png
    65.9 KB · Views: 1
Sera hiyo inafaa labda kwa nchi matajiri siyo kwa nchi maskini .na ukiaanzisha watu watagawanyika sana.by the way hata kama Lissu angeshinda hawezi pata wabunge wakutosha wakumwezesha ku Indoce sharia labda awe dictator
 
Tumchague Lissu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
#niyeye #Lissukwanza...
 
Wananchi wawe huru kuamua hatima yao kwenye majimbo yao ikisimamiwa na serekali kuu.

Ukiona mtu anabeza Sera ya majimbo, huyo ni MKOLONI MWEUSI. Maana mfumo huu tulio nao bado unamapungufu mengi sana kama vile ukabila na ukanda . Angalieni kwa sasa viongozi wote wa taasisi za umma ni wakutoka kanda ipi? Sio uchochezi bali ndo ukweli.

Mpaka tunaambiwa musiponichagulia mmbuge wa ccm siwaletei maji, nakwamba kila jimbo alipo mpinzani maendeleo ananyimwa kwa maksudi kisa ni waupinzani. Mfumo wa Majimbo hautakua na huo upuuzi na upendeleo wakijinga kama tunavoona sasa.

Majimbo yataleta ushindani wa maendeleo kwa kasi kubwa kuliko sasa. Angaliene maeneo ambayo yanapendelewa kimaendeleo kwa sasa ni Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Arusha. Kwani Mbeya na miji mingine hawahitaji flyover, hawahitaji taa za barabarani? Yote haya yanashindika kwa sababu ya mfumo tulio nao. Nchi hii ni kubwa mno, majimbo yataleta urahisi wakiutawala.

Eti majimbo yataleta utawala wawazungu. Hoja yakipuuzi na kitoto kweli hii. Mbona hata sasa tunakimbiza ma bakuli kwa wazungu? Inamaana hawaoni hilo? Mbona ccm walisha tuuza kitambo kwa wazungu.
CCM ndo waliingia vimkataba vyaajabu vya madini, tuseme vya raslimali yetu yote. Wao ndo wametufikisha hapa. Leo magufuli anatekeleza kwa kiasi kilio cha wapinzani, wanajiona analeta ukombozi. Kiukweli ni kwamba kwavile sio jadi ya ccm kuleta maendeleo, ndo maana wanashindwa kupanga vipaumbele vya maendeleo, vizuri wanaishia kuumiza wanchi.

CCM inajua kua wamechelewesha maendeleo wenyewe, ndo maana utaona mtu anashangaa na kupiga makelele na ka flyover ka Mfugale na Ubungo interchange. Vitu vidogo vingefanyika miaka mingi ilio pita.
Hela ccm na serekali YAKE walikua nazo, ila wizi na kujilimbizia mali viongozi. Leo wanatuamisha ni malaika! Lol!

Majimbo yatafuta umwinyi wakujimilikisha nchi unao fanywa na Rais. Rais ndo kila kitu na ndo anakugawia hela na ndo anaamua kipi kifanyike na wapi? Ndo maana yeye anamua tuu kujenga uwanja wa ndege kwao, wakati watumishi nyongeza hamna, akakurupuka kununua ndege, akakurupuka kujenga Reli na Bwawa la Nyerere wakati wananchi wanaumia bila kuwashilikisha.

Majimbo yataleta fikra chanya na kufutilia mbali ule upuuzi wa NDIYOOOOO! BUNGENI unaofanywa na ccm, ule ukiritimba wa wabunge kuunga mkono kila jambo na kupitisha kila Matumizi, sheria, kanuni kwa Nia ovu pasipokujua kwamba watawala wa leo ni wapinzani wakesho, the same sheria zitakuja kuwaumiza hata wao wakiwa wapinzani.

Majimbo, yatakuja kuleta ufanisi zaidi kwa kila nyanja na anae ogopa mfumo wakiutawala wa majimbo, kama nilivyosema, ni mkoloni mweusi na Mnufaika mkubwa wa utawala wa ccm.
Tuwe wakweli, anaye tetea ccm muangalie kwa umakini wadhifa wake ndani ya serekali na chama. Utagundua ni mnufaika mkubwa wa ccm na uogozi wake.

Hata Kamuzu Banda wa Malawi, Moi wa Kenya, Mobuto wa Zaire, Bokasa wa Afika ya Kati, Peter Botha wa Afrika ya Kusini, Adolf Hitler wa Ujerumani, walikua na wapambe, hata Benito Mussolini wa Italy alikua na wapambe, hata Joseph Stalin wa USSR Siku hizi Russia alikua na wapambe. Kwahio watu waina hiyo hawakosekani, wote wanakua wanufaika wakubwa wa chama tawala.
Wote twajua utawala wa miaka 5 wa Magufuli umekua kandamizi kweli kweli. Lakini wengine hapa jamvini wanaongea na kutoa mada utafikiri alikua anaishi Nje ya nchi hajui kilichokua kina fanyika.

Hitimisho, mfumo wakiutawala wa majimbo ndo suluhu kuu na chachu ya ushindani wa maendeleo ndani ya nchi. Tusidanganyane huu mfumo wa sasa umefeli. Tulianza na mfumo wa ujamaa kwa miaka 25 ukafeli 1984, tukaanza mfumo wa sasa 1985 chini ya Mwinyi. Imepita miaka 35, umefika wakati tujaribu mfumo mwingine ili tuone tutapigaje hatua ya maendeleo haraka zaidi. Let us be dynamic!
Kama watu hatuwezi kuwa na mfumo usiokua na tija kiutawala tukaukumbatia daima. Ndiyo, wanao nufaika nao kama ilivokua kwa ujamaa, watakua wagumu kuuacha na kukumbatia mfumo mpya wa majimbo.

Mfumo wa majimbo ni mzuri sana na unawapa wananchi mamlaka yakuongoza na kuamua maendeleo ya jimbo lao na huleta wivu wa maendeleo kwa hali ya juu.
Tumeona kila mmoja kua mtumwa wakutaka kuja na kuishi Dar es Salaam na sasa Dodoma. Tunahitaji miji mingi na ustawi wa taifa kimaendeleo. Na mpinga Sera ya Majimbo halitakii meema taifa letu na ni mtu anaye jali tumbo lake tuu.

KILA MFUMO WAKIUTAWALA UNA FAIDA NA CHANGAMOTO ZAKE. ILA KWASASA MFUMO WA SASA WAKIUTAWALA UNAONEKANA KUA NA CHANGAMOTO ZAIDI KULIKO FAIDA TUKILINGANISHA NA UTAWALA WA MFUMO WA MAJIMBO.
 
Wananchi wawe HURU kuamua hatima yao kwenye majimbo yao ikisimamiwa na serekali kuu.

Ukiona mtu anabeza Sera ya majimbo, huyo ni MKOLONI MWEUSI. Maana mfumo huu tulio nao bado unamapungufu mengi sana kama vile ukabila na ukanda . Angalieni kwa sasa viongozi wote wa taasisi za umma ni wakutoka kanda ipi? Sio uchochezi bali ndo ukweli.

Mpaka tunaambiwa musiponichagulia mmbuge wa ccm siwaletei maji, nakwamba kila jimbo alipo mpinzani maendeleo ananyimwa kwa maksudi kisa ni waupinzani. Mfumo wa Majimbo hautakua na huo upuuzi na upendeleo wakijinga kama tunavoona sasa.

Majimbo yataleta ushindani wa maendeleo kwa kasi kubwa kuliko sasa. Angaliene maeneo ambayo yanapendelewa kimaendeleo kwa sasa ni Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Arusha. Kwani Mbeya na miji mingine hawahitaji flyover, hawahitaji taa za barabarani? Yote haya yanashindika kwa sababu ya mfumo tulio nao. Nchi hii ni kubwa mno, majimbo yataleta urahisi wakiutawala.

Eti majimbo yataleta utawala wawazungu. Hoja yakipuuzi na kitoto kweli hii. Mbona hata sasa tunakimbiza ma bakuli kwa wazungu? Inamaana hawaoni hilo? Mbona ccm walisha tuuza kitambo kwa wazungu.
CCM ndo waliingia vimkataba vyaajabu vya madini, tuseme vya raslimali yetu yote. Wao ndo wametufikisha hapa. Leo magufuli anatekeleza kwa kiasi kilio cha wapinzani, wanajiona analeta ukombozi. Kiukweli ni kwamba kwavile sio jadi ya ccm kuleta maendeleo, ndo maana wanashindwa kupanga vipaumbele vya maendeleo, vizuri wanaishia kuumiza wanchi.

CCM inajua kua wamechelewesha maendeleo wenyewe, ndo maana utaona mtu anashangaa na kupiga makelele na ka flyover ka Mfugale na Ubungo interchange. Vitu vidogo vingefanyika miaka mingi ilio pita.
Hela ccm na serekali YAKE walikua nazo, ila wizi na kujilimbizia mali viongozi. Leo wanatuamisha ni malaika! Lol!

Majimbo yatafuta umwinyi wakujimilikisha nchi unao fanywa na Rais. Rais ndo kila kitu na ndo anakugawia hela na ndo anaamua kipi kifanyike na wapi? Ndo maana yeye anamua tuu kujenga uwanja wa ndege kwao, wakati watumishi nyongeza hamna, akakurupuka kununua ndege, akakurupuka kujenga Reli na Bwawa la Nyerere wakati wananchi wanaumia bila kuwashilikisha.

Majimbo yataleta fikra chanya na kufutilia mbali ule upuuzi wa NDIYOOOOO! BUNGENI unaofanywa na ccm, ule ukiritimba wa wabunge kuunga mkono kila jambo na kupitisha kila Matumizi, sheria, kanuni kwa Nia ovu pasipokujua kwamba watawala wa leo ni wapinzani wakesho, the same sheria zitakuja kuwaumiza hata wao wakiwa wapinzani.

Majimbo, yatakuja kuleta ufanisi zaidi kwa kila nyanja na anae ogopa mfumo wakiutawala wa majimbo, kama nilivyosema, ni mkoloni mweusi na Mnufaika mkubwa wa utawala wa ccm.
Tuwe wakweli, anaye tetea ccm muangalie kwa umakini wadhifa wake ndani ya serekali na chama. Utagundua ni mnufaika mkubwa wa ccm na uogozi wake.

Hata Kamuzu Banda wa Malawi, Moi wa Kenya, Mobuto wa Zaire, Bokasa wa Afika ya Kati, Peter Botha wa Afrika ya Kusini, Adolf Hitler wa Ujerumani, walikua na wapambe, hata Benito Mussolini wa Italy alikua na wapambe, hata Joseph Stalin wa USSR Siku hizi Russia alikua na wapambe. Kwahio watu waina hiyo hawakosekani, wote wanakua wanufaika wakubwa wa chama tawala.
Wote twajua utawala wa miaka 5 wa Magufuli umekua kandamizi kweli kweli. Lakini wengine hapa jamvini wanaongea na kutoa mada utafikiri alikua anaishi Nje ya nchi hajui kilichokua kina fanyika.

Hitimisho, mfumo wakiutawala wa majimbo ndo suluhu kuu na chachu ya ushindani wa maendeleo ndani ya nchi. Tusidanganyane huu mfumo wa sasa umefeli. Tulianza na mfumo wa ujamaa kwa miaka 25 ukafeli 1984, tukaanza mfumo wa sasa 1985 chini ya Mwinyi. Imepita miaka 35, umefika wakati tujaribu mfumo mwingine ili tuone tutapigaje hatua ya maendeleo haraka zaidi. Let us be dynamic!
Kama watu hatuwezi kuwa na mfumo usiokua na tija kiutawala tukaukumbatia daima. Ndiyo, wanao nufaika nao kama ilivokua kwa ujamaa, watakua wagumu kuuacha na kukumbatia mfumo mpya wa majimbo.

Mfumo wa majimbo ni mzuri sana na unawapa wananchi mamlaka yakuongoza na kuamua maendeleo ya jimbo lao na huleta wivu wa maendeleo kwa hali ya juu.
Tumeona kila mmoja kua mtumwa wakutaka kuja na kuishi Dar es Salaam na sasa Dodoma. Tunahitaji miji mingi na ustawi wa taifa kimaendeleo. Na mpinga Sera ya Majimbo halitakii meema taifa letu na ni mtu anaye jali tumbo lake tuu.

KILA MFUMO WAKIUTAWALA UNA FAIDA NA CHANGAMOTO ZAKE. ILA KWASASA MFUMO WA SASA WAKIUTAWALA UNAONEKANA KUA NA CHANGAMOTO ZAIDI KULIKO FAIDA TUKILINGANISHA NA UTAWALA WA MFUMO WA MAJIMBO.
 
Hii ni moja kati ya sera bora kabisa kutoka upinzani hasa chadema. Nchi zinazoendeshwa kwa mfumo huu zina mafanikio makubwa....
 
Back
Top Bottom