Uchaguzi 2020 Sera ya upinzani ingepaswa kuwa moja tu, kuondoa udikteta na kuruhusu Haki na Uhuru

Uchaguzi 2020 Sera ya upinzani ingepaswa kuwa moja tu, kuondoa udikteta na kuruhusu Haki na Uhuru

Naanto Mushi

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2015
Posts
6,236
Reaction score
15,677
Nimefurahishwa sana na sera ya Chadema ya, uhuru, haki, na maendeleo. Ila binafsi ningependa kama ingeweza kusomeka, kuondoa udikteta, kuleta haki, na uhuru. Udikteta, kukosekana kwa haki na uhuru, ndo mambo yaliyokithiri kwenye utawala wa Magufuli kwa miaka mitano iliyopita.

Kwanini uhuru na haki? Kuna siri kubwa na uhusiano kati ya uhuru, haki, na maendeleo, na ndio haswa chimbuko la maendeleo ya nchi za ulaya na America.

Hivyo basi, ukiweza kuwa na uhuru na haki, ni lazima uwe na maendeleo. Mfano kwa sasahivi, kuna malalamiko mengi ya kukosekana haki kwa wafanyabiashara.

Hii imepelekea wengi kukosa uhuru wa kuwekeza na kuzalisha huduma na bidhaa. Unakuwa na uoga, kwamba ukifungua duka la tatu pale, TRA kesho wapo mlangoni kwako, matokeo yake mawazo ya kupanuka kibiashara yanadumaa na hivo hata rate ya maendeleo inakuwa inapungua.

Kukosekana huko kwa haki, uhuru na udikteta wa wazi, umekuwa ni mwiba mkali wa maendeleo ya nchi hii.

Ntazidi kuwasihi CHADEMA waendelee kushikilia na kuhubiri kuleta uhuru, haki na kutokomeza udikteta nyemelezi.

Kwa mahali nchi ilipofika, hivi vitu vyote CCM wanajisifu navyo vitakuwa si kitu kama kutakosekana uhuru, na itakuwa ni ngumu sana nchi kupata maendeleo halisi ambayo yatagusa maisha ya wananchi.
 
Yaan kumbe kuna watu nchi hii hamna shukran yaan rais maguful nchi zote za africa zinamlilia na transparency international tz ni nchi ya 38 kati ya nchi 180 dunian kwa kutumia vzr fedha za umma bado mnaongelea matumizi mabaya
 
Hii awamu imezalisha maskini wengi Sana kwasabb ya kukosekana kwa Uhuru na haki. Na mgombea huyu huyu ndiye aliyesema matajiri wataishi kama mashetani
 
Yaan kumbe kuna watu nchi hii hamna shukran yaan rais maguful nchi zote za africa zinamlilia na transparency international tz ni nchi ya 38 kati ya nchi 180 dunian kwa kutumia vzr fedha za umma bado mnaongelea matumizi mabaya
Sio excuse ya kuminya haki..
 
Hii awamu imezalisha maskini wengi Sana kwasabb ya kukosekana kwa Uhuru na haki. Na mgombea huyu huyu ndiye aliyesema matajiri wataishi kama mashetani
Huu uchaguzi hata upinzani wasipofanya kampeni, mtu anayejielewa anajua mpaka sasa, kura yake ataipeleka wapi
 
Back
Top Bottom