KERO Serikali angalieni namna ya kutatua kero hii ya N-Card Kivukoni Ferry. Si vema kutumia kadi ya mtu kuvuka

KERO Serikali angalieni namna ya kutatua kero hii ya N-Card Kivukoni Ferry. Si vema kutumia kadi ya mtu kuvuka

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Serikali ya Tanzania haijawahi kuwa serious na kazi zake hata siku moja nimeshangaa sasa utaratibu uliopo hapa Kivukoni Ferry (Dar es Salaam) ukitaka kwenda kupanda Panton kuvuka kwenda Kigamboni.

Kwanza nikiri kuwa utaratibu uliowekwa kutumia kadi (N - Cards) ni hatua nzuri sana lakini hatua hii bila ufanisi hakuna la maana lolote, utaratibu kwa kadi hizi umewekwa kwa ajabu sana.

Mimi sio mvukaji wa mara kwa mara kwenda Kigamboni ile leo nimekuja kuvuka hapa na kukutana na hali ya ajabu, kwanza unatakiwa lazima uwe na kadi ndio uweze kuvuka vizuizi vya kuingia kusubiri Kivuko, ni hatua nzuri sana na ipo njema na napongeza.

Shida inakuja pale ambapo huna kadi na si mvukaji wa mara kwa mara utaratibu uliowekwa ni mbovu.

Kwanza upatikanaji wa kadi hizi ni shida ni majira ya Saa 10 jioni na tayari kadi zimeisha na Wahudumu wanakuambia hapo huwezi kupata tena hadi kesho. Swali nawauliza sasa navukaje?

Jibu lao ni la ajabu sana, wanakuambia mwombe mtu utumie kadi yake kisha umpatie TZS 200/-. Nawauliza kama nisipopata huyo wa kunisaidia hiyo kadi nafanyaje? Jibu lao ni jepesi sana wewe omba watakubali tu.

Wakati huo huo pembeni kuna mtu anauza kadi, mtu huyu ni nani? Ametoa wapi kadi hizi hadi na yeye anauza? Ni masuala ya kushangaza.

Serikali tukiamua kufanya jambo lenye tija basi tulifanye kweli sio kujaribu na kisha kutafuta mianya ya ubabaishaji.

Wezesheni watumishi wenu kuwa na kadi za kutosha na pia tafuteni utaratibu mzuri kwa watu ambao wao si wavukaji wa kila siku, wengine hutumia Panton mara moja kwa mwaka.
 
Nimesoma maelezo yako vizuri kitu cha kwanza tuwacho ni tabia ya kulaumu serikali kwa kila jambo. Vivuko vyote nchini vinajulikana viko chini ya wizard gani hao ndio watu wa kulaumu kama wahusika na sio serikali. Viongozi na wizara zao wanapewa kazi za kufanya na hawafanyi vizuri lawama zinaenda kwa serikari ni makosa. Wizara husika inafaa kubeba msalaba wake na kutatua shida zake kama wameshindwa waseme watu wengine wapate nafasi ya kufanya hiyo kazi ambae wataweza kufanya kwa umakini.
Usiongelee kivukotu Train station kuna mapungufu mengi na ukiuliza maswali hakuna majibu ya kurizisha. Shida ipo kwa wizard na mawaziri washughulikie kazi zao muwache kutupia lawama serikali kila wakati. Asante.
 
Nimesoma maelezo yako vizuri kitu cha kwanza tuwacho ni tabia ya kulaumu serikali kwa kila jambo. Vivuko vyote nchini vinajulikana viko chini ya wizard gani hao ndio watu wa kulaumu kama wahusika na sio serikali. Viongozi na wizara zao wanapewa kazi za kufanya na hawafanyi vizuri lawama zinaenda kwa serikari ni makosa. Wizara husika inafaa kubeba msalaba wake na kutatua shida zake kama wameshindwa waseme watu wengine wapate nafasi ya kufanya hiyo kazi ambae wataweza kufanya kwa umakini.
Usiongelee kivukotu Train station kuna mapungufu mengi na ukiuliza maswali hakuna majibu ya kurizisha. Shida ipo kwa wizard na mawaziri washughulikie kazi zao muwache kutupia lawama serikali kila wakati. Asante.
Leo ndio nimeelewa kwamba WIZARA sio sehemu ya SERIKALI.

Lakini nina kiu ya kujua Serikali ni nini na wizara ni nini.
 
Serikali ni watu na taasisi ndani ya jamii hasa dola vyenye mamlaka ya kutawala na kufanya maazimio kwa wote katika eneo fulani.
Serikali inatunza na kutekeleza sheria, kanuni na miongozo na kuendesha shughuli muhimu za umma.
Shabaha kuu ya serikali ni kutunza amani na usalama wa raia katika jamii.

Kuna serikali za ngazi mbalimbali kwa mfano kwenye taifa, jimbo, mji na kijiji. Taratibu hutofautiana kati ya nchi na nchi. Katika mfumo wa shirikisho mamlaka ya serikali hugawiwa kwa kusudi kwenye ngazi mbalimbali hasa za taifa na jimbo.

Kinyume chake ni itikadi ya serikali kuu inayoweka mamlaka yote katika ngazi ya serikali kuu inayoweza kuamua kukabidhi sehemu ya madaraka yake kwa maeneo na vitengo vya kiutawala.
 
Back
Top Bottom