Serikali Awamu ya Tano yasaini Mkataba wa kusambaza maji Kutoka ziwa Victoria Kuelekea Majimbo ya Musoma, Bunda na Butiama Wenye Thamani ya Bil 70

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Serikali Ya Awamu ya 5 inayoongozwa na Mzalendo Nambari 1 nchini Dkt John Pombe Magufuli Imeamua kutimiza ahadi yake kwa kishindo Mkoani Mara

Imegharamia mradi mkubwa wa Thamani ya Tsh Bilioni 70 utakaosambaza Maji Kutoka Ziwa Victoria kuelekea Majimbo ya Musoma Vijii, Butiama na Bunda

Hongereni kwa kuchagua Wabunge wa CCM
Hongereni kwa kuchagua Madiwani wa CCM
Hongereni Sana kwa Kumchagua Mheshimiwa Magufuli


 
Elezea wahusika wa mkataba,

Elezea huo mkataba utakuwa ni wa kipindi gani,

Elezea fedha za huo mradi kama zimetolewa na serikali au wahisani kutoka nje,

Elezea hatua ambayo huo mradi umefikia: Kama umeshaanza au bado wanajiandaa kuanza,

Ukishaandika haya mambo ya msingi ndiyo uanze kuimba hizo ngonjera zako za CCM na Daktari John Pombe Magufuli.
 
Hongera nyingi kwa Serikali kwa Mradi mkubwa, kikubwa Vijiji bomba linakopita wapatiwe Maji ili kuepuka hujuma za miundombinu.
 
Hii ni taarifa mbaya sana kwa wazee wa kuzungusha mikono. Watamani kujichimbia sasa matatizo ya wananchi yakiisha kwa kipindi cha miaka mitano inayoanza. MWAKA 2025 sijui watakuja na ngonjera zipi. Hakika 2025 itakuwa yakijani tuu.

Hakuta kuwa na hayo magunzi yaliyokimbia nje ya nchi yakiahidi yamekwenda kujipanga kwa ajili ya kuja kuchua nchi. Labda nchi ya kusadikika
 
Muda utasema ?? Vipi wale waarabu walioombwa na Magu fool kuja kuchimba visima mashuleni , hawatokuja tena ??


 
Ni jambo zuri kitu kilichonishangaza kampuni iloyoshinda Tenda ya mradi inaitwa Unik kutoka Lessotho?wasi wasi ni hii kampuni hakuna mkono wa wizi,chawah kusikia kuwa Lesotho wanauzoefu wowote na miradi hii ya Maji.
 
Mchanganuo wote huo unataka ufanyiwe BURE?
 
Miaka 50 bado mnahangaika na maji wilayani [emoji23][emoji23][emoji23]. Huku mjini tu mvua dakika 5 barabara zinafungwa.
Akili za CCM bana
Akili za BAVICHA bana! Miaka yote mnahangaika kuichungulia Sisiemu weeeeee, mpaka mnashtuka hiyooo 2025 hata hamjui nani ni nani humo mwenu sakosini. Enewei, tuna mpango wa kukata jina fulani, mtaenda na huyo. Halafu maandamano leo ni mtaa gani hivi???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…