DOKEZO Serikali chukueni hatua za haraka dhidi ya Nabii Dominiki "Kiboko ya Wachawi"

DOKEZO Serikali chukueni hatua za haraka dhidi ya Nabii Dominiki "Kiboko ya Wachawi"

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Si wameona nchi ni ya wajinga toka kichwani hadi mkiani hivyo hiyo ni fursa kwao tusiwalaumu, tuwe wenye akili tunapochagua viongozi
 
Wajing ndio waliwao

Kam havunji sheria kazi iendelee
 
Sina shida na manabii na mitume feki.
Ni kama waganga wengine wa kienyeji na wachawi na matapeli wanaotafuta maisha yao kupitia upumbavu wa wengi.

Soko la wapumbavu ni kubwa tanzania, kiasi kila tapeli anasajili kanisa na kuvuna pesa kwa kutumia jina la bwana!
 
Alafu mkongomani huyu
Hawa wengi matapeli tu
Wanacheza na akili za watu

Mfano leo hii,mm nianze kumshobokea kakob wakati
Wengine tumekuwa na tunamuona kakob anauza cd kko
Leo hii nabii 😄
Ukiishi kwa kuona mengi elimu tosha kabisa huwezi kubabaishwa
Na mtu

Ova

Kabisa ni matapeli sana hao ,ila huyo nabii feki sijui kwanini watu wanashindwa kugundua usanii wake.

Duuh kumbe Katortoise alikuwa anauza CD k/koo 😀 😀 daaa hatari sana.

Kabisa kuishi kwingi kuona mengi ,ndio maana hawa matapeli hawatuiingizi mkenge.
 
Kabisa ni matapeli sana hao ,ila huyo nabii feki sijui kwanini watu wanashindwa kugundua usanii wake.

Duuh kumbe Katortoise alikuwa anauza CD k/koo 😀 😀 daaa hatari sana.

Kabisa kuishi kwingi kuona mengi ,ndio maana hawa matapeli hawatuiingizi mkenge.
Alikuwa anauza mikanda ya miziki
Duka lake kama nakumbuka lioiandikwa jina something galaxy, hawa manabii sijui kwanini serikali inaawachia naona mambo ya kiimani zaidi labda

Ova
 
Ila twendeni mbele hii nchi tuna tatizo sehemu kwani huko alipo hakun mtendaji wa mtaa au mkuu wa wilaya mban ni jambo dogo tu tena mtu mwenyewe si mtanzania ..

Kwanini tunamwacha anarubuni watu wetu.
 
Lengo la huh Uzi ni nini..!?

Ni Nabii kutumia Matangazo unayoyaita Fake Radioni ama..!?

Ni kitendo cha Kuwalipisha kiwango kikubwa cha pesa watu wanaoenda kuonana nae face to face...!?

Ama malalamiko yako yanamaanisha kwamba Ni Nabii Taperi asiye na ukweli wowote.....!?

Binafsi sikubaliani na namna yeye anavyowalipisha Watu pesa ili kumuona, Angetumia Ubunifu kama wa Mwamposa, pale anapowataka watu kuchangia kusambaza Injili, kwa sababu kuna gharama kubwa kurusha Matangazo iwe TV ama Radio...!

Aisifuye Mvua imemnyea, yakikukuta wewe mwenyewe utajua Manabii wote wanapatikana wapi.....!

Kile watu wasichojua Kuna mstari mdogo sana kati ya Nabii na Mganga wa Kienyeji, Mganga wa Kienyeji mpiga Ramli akiamua kuokoka akitaka kumtumikia Mungu, anakua Nabii straight, utofauti ni kwamba akiwa Mganga alikua anafanya kazi kwa Usaidizi wa Mizimu na Majini, na sasa ni Nabii anafanya kazi kwa usaidizi wa Roho Mtakatifu.

Kuna Matatizo ya Watu yanawahitaji Manabii moja kwa moja, kumsaidia mtu atoke shimoni then uanze kumfundisha kuomba, kufunga n.k....!

Mtu ana matatizo lukuki, ni Mgonjwa, hatembei, Macho hayaoni kwa sababu ya Husda za Wanadamu,hafu unamwambia asome Biblia, afunge, akemee, anaanzia wapi.... Unahitaji Nabii atayekwambia tatizo lako na kutatua then akufundishe kumtegemea Mungu.
 
Itaje kabisa na radio station yenyewe una ficha Nini si passion FM au ipi nyingine Tanzania wajinga ni wengi mnoo ndugu ndio maana CCM pamoja na urojo wote huu inaendelea kutawala tunayo safali ndefu sana
 
Maisha mqgumu, watu tunatafuta namna ya ku survive, vibinti vimeamua kuwa vidangsji vinatoa matangszo jinsi ya kutongozana na kupigana miti! Vishetani vidogo,

Vijana wa kiume, ama machawa, madalali chawa, ma, mc, wengine ma pastor, kila motivational speaker sasa hv ni pastor ana kanisa!
 
Huyu Jamaa tushawasanua sana watu humu kwamba jamaa ni Tapeli ,yaani anafufua wafu ,yaani ukipiga simu hata uwe na ugonjwa gani utapona tu ,cha kushangaza hiyo namba muda wote ipo busy tu ,kwa kifupi anafanya usanii ,na tatizo letu sisi waTZ hatushirikishi ubongo easy sana kudanganywa.
Hizo simu unazosikia ni feki. Ni watu wake amewapanga. Hata Arusha kuna redio nimeishitukia kuna mganga ana kipindi basi watu wanapiga simu kumshukuru kwamba walienda kwake matatizo yao yakatatuliwa. Ukichunguza utaona sauti ni zilezile kila siku! Nashindwa kuelewe kilicho nyuma ya hivi vituo vya redio.
 
Mbona hata wanaotapeliwa mitaani au mitandaoni wanatoa pesa kwa hiari yao wenyewe lakini utapeli wa mtandaoni unahesabika ni kosa na ukikamatwa utafikishwa mahakamani. Iweje hawa wanaoibia watu mchana kweupe kwa jina la dini wasiwe na hatia?
Usihusishe serikali na vitu vya kipumbavu kila mtu amepewa akili hapo inategemea unaitumiaje akili uliyopewa,wanaoenda huko wameenda kwa ridhaa zao wenyewe wacha tu wapigwe
 
Sure ,watu sijui wanadanganyika vipi na usanii wanaoufanya ,Tapeli Dominic anachofanya anaingia studio anarecord mazungumzo ya kisanii ya mpiga simu then wanyarusha Furaha Redio,Efm au Times FM.

Kuna siku kuna dada alimpigia simu kwamba hajui amepewa mimba na nani hivyo akampigia Kiboko ya wachawi amtajie ,then Nabii akamtajia kwamba ni Fundi Ujenzi ndiyo aliyempa ujazito kati ya wanaue wake sita.

Mimi huwa namsikiliza kama ze comedy huwa nafurahi sana anavyoigiza.
Hivi vituo vya redio siku hizi basi tu.......
Sidhani kama kama RTD ya enzi zetu ingeweza kurusha upuuzi kama huu. Siku hizi wanajali pesa tu. Hakuna content za maana ni porojo na kuchezesha kamari tu
 
Babu wa loliondo alianza hivyo hivyo, watu wakaacha dose na kufa. Huyo ni tapeli, anatumia nguvu za giza, asijiite nabii ila ni "mganga mashuhuri " anapiga ramli chonganishi.
 
Kwahiyo unataka kusema wachina hawana akili? Uchina hata kukusanyika ukafanya maubili utawekwa ndani, unaambiwa nenda nyumbani kwako ukaombe unavyotaka na sio kukusanya watu.
Wana akili walendio maana wameendelea maana wanajua maendeleo yanapatikana kwa kufanya kazi siyo uwakusanye watu uwauzie maneno matupu na mafuta ya upako.
 
Back
Top Bottom