DOKEZO Serikali, elezeni ukweli kuwa watoto chini ya miaka 5 wanalipia huduma, kama sivyo kituo cha afya Kimara wawajibishwe kwa kutoza pesa na huduma mbovu

DOKEZO Serikali, elezeni ukweli kuwa watoto chini ya miaka 5 wanalipia huduma, kama sivyo kituo cha afya Kimara wawajibishwe kwa kutoza pesa na huduma mbovu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mambo ya siasa yananihusu na naifatilia, kuhusu kuhoji hicho ulichosema nadhani tukutane kwenye hoja husika inayohusika na saa hiyo na si hapa panapojadiliwa kuhusu wajibu wa Serikali kutekeleza sera zake
Usione kuwa nimekupa challenge kwa sababu hoja yako haina maana.

Nimetaka tu ku-rise awareness ya jinsi kila mwananchi anavyotakiwa kuwa makini na kushiriki kwenye siasa za nchi. Tatizo lako limekuwepo kila siku na kila sehemu ya nchi, labda tu ulikuwa hujakutana nalo.

Ukweli ni kuwa siyo muda wa kuihoji serikali sasa, bali ni muda wa kufanya madadiliko. CCM haiwezi kubadilika tena hata ukihoji namna gani.

Tusipokubali hii fact basi tuendelee kuishi maisha ya kulalamika kila uchao.
 
Hakuna cha mtoto Wala mzee huduma za afya ni malipo hata mtoto akiwa na siku Moja.Ndiyo azabu ya kuminya demokrasia
 
Kipindi cha Magu,
Ummi alionekana kuwa msimamizi mzuri wa sera ya afya.
Ila sasa kusema ukweli wizara imemshinda. Sio kwenye matibabu tuu, hata NHIF nayo imemshinda.
Haiingii akini watoto chini ya miaka 18 wakate bima kwa mkusanyiko.
Je kama mtoto hayuko shule hastahili kuwa na bima? Kuna vitu vingine havihitaji elimu kutoa maamuzi. Ummi kachoka.
 
Leo nilifika kituo cha afya Kimara baada ya ndugu yangu kuniita nikalipie gharama ili mtoto wake apatiwe matibabu baada ya kuanguka na kuumia mguu.

Picha linaanza kuingia kwa daktari, mama wa mtoto anaeleza mwanaye kaumia baada ya kuaguka wakati anacheza, dk bila hata kumgusa wala kumwangalia mtoto akatoa jibu, NENDA KAMCHUE NA UMPE NA DAWA YA MAUMIVU!

Mama wa mtoto akamwambia dk nishampa dawa ya maumivu na kumchua ila hakuna matokeo mazuri, dk akasisitiza aende, ikabidi mama wa mtoto alazimishe kuomba dk aandike akapigwe X-ray, cha ajabu dk. anakubali ila anamuuliza mama wa mtoto unataka apigwe picha wapi, mama akamwambia mkague ili uone ni eneo gani hasa maana alipoumia mguu ulivimba na hataki kuguswa, dk akarudia tena we sema apigwe wapi mama wa mtoto ikabidi ajibu apigwe picha mguu mzima.

Daktari akaandika kwenda kwenye picha(X-ray), kufika huko mama wa mtoto akiwa na kadi ya kliniki akijua huduma ni bure, anaambiwa anatakiwa kulipia 15000 kwa ajili ya kupata huduma hiyo na hakuwa na hela hapo maana Serikali kutwa inaimba huduma ya matibabu chini ya miaka 5 ni bure, huku wananchi wanatozwa pesa.

Nikaenda nikapewa namba nikalipia japo mwanzo hawakutaka nilipie kwa namba ya malipo walitaka niwape pesa taslimu nikakataa, ili kuonesha ni malipo halali ya serikali hivyo sina shaka kuwa serikali inawadanganya wananchi kuwa huduma za matibabu chini ya miaka 5 ni bure na huku wanalipa na hii ni risiti halali ya malipo.


Baada kupiga picha kurudisha majibu kwa Dk, akasema kavujika mguu kwenye paja, na apewe 50000 ili mtoto afungwe PoP, nikasema hiyo hela ni ya nini? akajibu ni ya kununua vifaa na gharama ya kufungia, nikasema nipewe namba ya malipo nilipe, dk akakunja sura mara mbili zaidi maana tangu mwanzo alishaonesha chuki.

Dk akasema hapa hakuna vifaa ni vya kununua na gharama yake ni 32,000 nikamwambia niandikie nikanunue mwenyewe, akaandika huku anasema kwa hiyo umeamua kwenda kununua mwenyewe sawa kanunue.

Nikafika duka la dawa nikapata vifaa kwa gharama ya 11500, nikapata hisia huenda alikuwa kashapiga hesabu zake juu ya hela ya kunuua vifaa ndio maana sura ilibadilika na kuuliza kama nimeamua kwenda kununua mwenyewe.

Niliporudi kwa Dk. akasema nikalipie gharama ya huduma ya kufunga, nikaenda mapokezi kulipia nao vilevile wakataka niwape pesa taslimu nikagoma ndipo wakanipa namba ya kulipia nikalipa sh, 20,000.

Je, Serikali kwa nini mnadanganya matibu bure kwa watoto chini ya miaka 5? Kama si kweli hamdanganyi ni kwa nini kituo cha Kimara watoze pesa ambazo zinakuja Serikalini?

Wafatilieni watoa huduma wa Kimara, wana lugha mbaya na wanatoa huduma mbovu, na hawako makini kabisa maana wakati nipo pale kuna mama mmoja alikuwa karudia kupiga picha mara ya pili baada ya mwanzo kupigwa uti wa mgongo na wakati yeye anasumbuliwa na kichwa!

Pia wanataka walipwe pesa wao na si kwenye mfumo wa malipo.
Dunia ya leo bado kuna mafala wanaamini kuwa wewe zaa kama sungura, halafu wanafikiri kuna wajinga huko duniani watalipa kodi kukutunzia wanao!
 
Tanzania inabidi tuwe na mentality ya kujitegemea. Hizi akili tegemezi za kijamaa zinaturudisha nyuma. Yaani mtoto wangu nimzae mwenyewe, niililie serikali kuhusu shule na matibabu. Kesho utaanza kusema Mwigulu Mchemba anapeleka watoto shule nzuri. Wasiojiweza ndio waisubiri serikali.

Leo nilifika kituo cha afya Kimara baada ya ndugu yangu kuniita nikalipie gharama ili mtoto wake apatiwe matibabu baada ya kuanguka na kuumia mguu.

Picha linaanza kuingia kwa daktari, mama wa mtoto anaeleza mwanaye kaumia baada ya kuaguka wakati anacheza, dk bila hata kumgusa wala kumwangalia mtoto akatoa jibu, NENDA KAMCHUE NA UMPE NA DAWA YA MAUMIVU!

Mama wa mtoto akamwambia dk nishampa dawa ya maumivu na kumchua ila hakuna matokeo mazuri, dk akasisitiza aende, ikabidi mama wa mtoto alazimishe kuomba dk aandike akapigwe X-ray, cha ajabu dk. anakubali ila anamuuliza mama wa mtoto unataka apigwe picha wapi, mama akamwambia mkague ili uone ni eneo gani hasa maana alipoumia mguu ulivimba na hataki kuguswa, dk akarudia tena we sema apigwe wapi mama wa mtoto ikabidi ajibu apigwe picha mguu mzima.

Daktari akaandika kwenda kwenye picha(X-ray), kufika huko mama wa mtoto akiwa na kadi ya kliniki akijua huduma ni bure, anaambiwa anatakiwa kulipia 15000 kwa ajili ya kupata huduma hiyo na hakuwa na hela hapo maana Serikali kutwa inaimba huduma ya matibabu chini ya miaka 5 ni bure, huku wananchi wanatozwa pesa.

Nikaenda nikapewa namba nikalipia japo mwanzo hawakutaka nilipie kwa namba ya malipo walitaka niwape pesa taslimu nikakataa, ili kuonesha ni malipo halali ya serikali hivyo sina shaka kuwa serikali inawadanganya wananchi kuwa huduma za matibabu chini ya miaka 5 ni bure na huku wanalipa na hii ni risiti halali ya malipo.


Baada kupiga picha kurudisha majibu kwa Dk, akasema kavujika mguu kwenye paja, na apewe 50000 ili mtoto afungwe PoP, nikasema hiyo hela ni ya nini? akajibu ni ya kununua vifaa na gharama ya kufungia, nikasema nipewe namba ya malipo nilipe, dk akakunja sura mara mbili zaidi maana tangu mwanzo alishaonesha chuki.

Dk akasema hapa hakuna vifaa ni vya kununua na gharama yake ni 32,000 nikamwambia niandikie nikanunue mwenyewe, akaandika huku anasema kwa hiyo umeamua kwenda kununua mwenyewe sawa kanunue.

Nikafika duka la dawa nikapata vifaa kwa gharama ya 11500, nikapata hisia huenda alikuwa kashapiga hesabu zake juu ya hela ya kunuua vifaa ndio maana sura ilibadilika na kuuliza kama nimeamua kwenda kununua mwenyewe.

Niliporudi kwa Dk. akasema nikalipie gharama ya huduma ya kufunga, nikaenda mapokezi kulipia nao vilevile wakataka niwape pesa taslimu nikagoma ndipo wakanipa namba ya kulipia nikalipa sh, 20,000.

Je, Serikali kwa nini mnadanganya matibu bure kwa watoto chini ya miaka 5? Kama si kweli hamdanganyi ni kwa nini kituo cha Kimara watoze pesa ambazo zinakuja Serikalini?

Wafatilieni watoa huduma wa Kimara, wana lugha mbaya na wanatoa huduma mbovu, na hawako makini kabisa maana wakati nipo pale kuna mama mmoja alikuwa karudia kupiga picha mara ya pili baada ya mwanzo kupigwa uti wa mgongo na wakati yeye anasumbuliwa na kichwa!

Pia wanataka walipwe pesa wao na si kwenye mfumo wa malipo.
 
Usizae na kuacha jukumu lako kama mzazi,
Jukumu lako ni kuhakikisha anatibiwa na sio kusubiria serikali
 
Back
Top Bottom