Serikali haileti vichwa vya Treni unavyovifikiria wewe

Serikali haileti vichwa vya Treni unavyovifikiria wewe

Monica Mgeni

Member
Joined
Oct 7, 2021
Posts
82
Reaction score
134
TUTAPOTEZA TUKISUBIRI VICHWA VIPYA VYA TRENI 2023.

Tarehe 04/07/2022 Ikulu Jijini Dar Es Salaam wakati wa Hafla ya Utiaji Saini Mkataba wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) sehemu ya Tabora hadi Isaka, Km 165 njia Kuu na Km 35 njia za kupishana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alieleza nia ya Serikali yake ya kuimarisha Usafiri wa Reli Nchini.

Moja ya kauli iliyotolewa na Mhe. Rais ni kwamba Serikali itanunua Vichwa vya Treni vilivyotumika lakini vikiwa katika hali nzuri ili vianze kutumika wakati tunasubiri Vichwa vipya vilivyoagizwa na Serikali ambavyo vinatarajiwa kuwasili Nchini mwaka 2023.

Ifahamike kuwa, Vichwa vya Treni vya awali vinavyotarajiwa kununuliwa na Serikali vitahifadhiwa na kutumika kama mbadala (Backup) pindi Vichwa vipya vitakapopata hitilafu. Suala hili litasaidia kuendelea kutolewa kwa Huduma za Usafirishaji kama kawaida.

Pili, Gharama za ununuzi wa Vichwa vipya vya Treni ya Mwendokasi ni sawa na kununua Mashangingi 10 mapya na gharama zake zinakadiriwa kufikia Tshs. Bilioni 4 kwa kichwa kimoja.

Tatu, Kihistoria kutokana na gharama kubwa ya ununuzi wa vipuri vipya vya Treni, Tanzania haijawahi kununua Vichwa vipya wala Injini mpya ya Treni tangu enzi za Mkoloni. Ambapo mwaka 1990 Shirika ya Reli ilinunua Injini (Used) namba 826 kutoka Sweden.

Uchumi wa Mataifa yanayoendelea umekuwa kikwazo kwa Nchi zetu kufanya manunuzi ya Vichwa vyote vipya kama ilivyofanyika kwa jirani zetu wa Kenya.

Vilevile, Uamuzi huu wa Serikali wa kuanza kutumia Treni iliyotumika yenye hali nzuri ni mzuri kutokana na ushindani wa Kibiashara uliopo katika Nchi za Afrika Mashariki ambapo kusubiri Treni Mpya ni kupoteza mapato katika kipindi ambacho reli tayari imekamilika kwa ajili ya matumizi.

Tumuunge mkono Rais wetu mwenye maono chanya ya kuinua Uchumi wa Taifa letu

Katuni VIWANGO.jpg
 
Bl 4 mbona kwa serikali ni ndogo sana.
Tozo tu ndani ya quater 1 zinaweza fika billion 5O ila tunaambiwa serikali inawaza kununua vichwa vipya vya treni kweli?

Ndege moja ilikuwa billion karibia 3OO na zilinunuliwa 1O ina maana bei ya ndege moja tu tungeweza pata vichwa vya kutosha tu tena vikiwa vipya maana sidhani kama kichwa cha treni mpya kinazidi billion 5O!

Haya mambo ya milolongo ndio yanasababishaga wizi wa hela na michongo ndio maana yule bwana alikuwa anakwapua cash analipa mkawa mnamuona mjinga. Tanzania ina watumishi wapumbavu sana.
 
huu ujumbe naomba umfikie Bimkubwa ni hivi SGR haina maana bila kukamilika Nyerere Dam sasa mbona hazungumzii yote kwa pamoja? Kuna nini hakisemi kuhusu Nyerere Dam wapenda maendeleo tuungane tumsumbue Bimkubwa hadi atupiganie na hilo pia maana ameonesha uwezo mkubwa na ushawishi kupewa mikopo kwa wazungu na wachina.

Ila kwa dhati kabisa napenda kumpongeza Mama Samia kwa kukomaa na SGR project ukweli itatulipa sana na tutaipiku Kenya kiuchumi. Kenya waliiba mno pesa za SGR reli yao ikaishia njiani Naivasha na haileti faida iliyotarajiwa na wanadaiwa matrilioni!
 
Kwa muktadha huu ni kwamba hata ndege za ATCL zilizonunuliwa ni used?
Mwendazake huwezi mlinganisha na Rais yoyote bongo kile kichwa watu wengi hawakukielewa!! Ndege mpya tu alinunua kwa pesa ya ndani ambayo sasa ina matumizi mengine kama sensa, safari za nje kufungua nchi na pesa zingine zinawekwa personal accounts!!!

kupanga ni kuchagua!!
 
Cha ajabu sheria ya manunuzi ya vitu vipya ingekuwa inabana manunuzi ya sekta binafsi, sheria hiyo ingeshikiliwa, na ingetokea uende kinyume ungekutana na adhabu kali
 
Mwendazake huwezi mlinganisha na Rais yoyote bongo kile kichwa watu wengi hawakukielewa!! Ndege mpya tu alinunua kwa pesa ya ndani ambayo sasa ina matumizi mengine kama sensa, safari za nje kufungua nchi na pesa zingine zinawekwa personal accounts!!!

kupanga ni kuchagua!!

Nyie akili ndogo ndio aliwaaminisha ni fedha za ndani, ukweli ni kuwa alichukua fedha za mifuko ya jamii kibabe bila kufuata sheria, na nyingine alikopa. Matokeo yake kaliiacha taifa na deni kubwa kupita maelezo.
 
Nyie akili ndogo ndio aliwaaminisha ni fedha za ndani, ukweli ni kuwa alichukua fedha za mifuko ya jamii kibabe bila kufuata sheria, na nyingine alikopa. Matokeo yake kaliiacha taifa na deni kubwa kupita maelezo.
mkuu simama hapo hapo, haya vaa kitanzi!! tayari? ngoja nirudishe akili ifanane na yako maana ulinipa pepa ukagundua nina akili kidogo ila Wizara ya elimu ilinipangia Special school A level kwa vibanda nilivyotandaza.

Just one question natumia mawazo yako tu yangu hapa situmii, je mifuko ya jamii ni pesa za ndani Tanzania au za Kenya? je wajua mchezo uliokuwepo NSSF kukopesha wadau wananunua ardhi laki na kuwauzia tena NSSF kwa milioni mia eti wajenge magorofa ya makazi, pesa haina kazi ile!! hata Mama Samia inabidi aichukue anunue vichwa na mabehewa mapya ya SGR manake Fao la Kujitoa lilifutwa pesa imerundikana tu kule kwenye mifuko ya jamii! Aachane na mikangafu na ngarangara huwa zinakula sana pesa za maintenance!!

mkuu Tindo leo tuna jambo letu na Injinia Hersi Jangwani ukikosa jutia kuzaliwa Danganyika Republic
 
mkuu simama hapo hapo, haya vaa kitanzi!! tayari? ngoja nirudishe akili ifanane na yako maana ulinipa pepa ukagundua nina akili kidogo ila Wizara ya elimu ilinipangia Special school A level kwa vibanda nilivyotandaza.

Just one question natumia mawazo yako tu yangu hapa situmii, je mifuko ya jamii ni pesa za ndani au za Kenya? je wajua mchezo uliokuwepo NSSF kukopesha wadau wananunua ardhi laki na kuwauzia tena NSSF kwa milioni mia eti wajenge magorofa ya makazi, pesa haina kazi ile!! hata Mama Samia inabidi aichukue anunue vichwa na mabehewa mapya ya SGR manake Fao la Kujitoa lilifutwa pesa imerundikana tu kule kwenye mifuko ya jamii! Aachane na mikangafu na ngarangara huwa zinakula sana pesa za maintenance!!

mkuu Tindo leo tuna jambo letu na Injinia Hersi Jangwani ukikosa jutia kuzaliwa Danganyika Republic

Zingatia neno kuchukua pesa za watu kibabe bila kufuata sheria kwenye post yangu.
 
TUTAPOTEZA TUKISUBIRI VICHWA VIPYA VYA TRENI 2023.

Tarehe 04/07/2022 Ikulu Jijini Dar Es Salaam wakati wa Hafla ya Utiaji Saini Mkataba wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) sehemu ya Tabora hadi Isaka, Km 165 njia Kuu na Km 35 njia za kupishana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alieleza nia ya Serikali yake ya kuimarisha Usafiri wa Reli Nchini.

Moja ya kauli iliyotolewa na Mhe. Rais ni kwamba Serikali itanunua Vichwa vya Treni vilivyotumika lakini vikiwa katika hali nzuri ili vianze kutumika wakati tunasubiri Vichwa vipya vilivyoagizwa na Serikali ambavyo vinatarajiwa kuwasili Nchini mwaka 2023.

Ifahamike kuwa, Vichwa vya Treni vya awali vinavyotarajiwa kununuliwa na Serikali vitahifadhiwa na kutumika kama mbadala (Backup) pindi Vichwa vipya vitakapopata hitilafu. Suala hili litasaidia kuendelea kutolewa kwa Huduma za Usafirishaji kama kawaida.

Pili, Gharama za ununuzi wa Vichwa vipya vya Treni ya Mwendokasi ni sawa na kununua Mashangingi 10 mapya na gharama zake zinakadiriwa kufikia Tshs. Bilioni 4 kwa kichwa kimoja.

Tatu, Kihistoria kutokana na gharama kubwa ya ununuzi wa vipuri vipya vya Treni, Tanzania haijawahi kununua Vichwa vipya wala Injini mpya ya Treni tangu enzi za Mkoloni. Ambapo mwaka 1990 Shirika ya Reli ilinunua Injini (Used) namba 826 kutoka Sweden.

Uchumi wa Mataifa yanayoendelea umekuwa kikwazo kwa Nchi zetu kufanya manunuzi ya Vichwa vyote vipya kama ilivyofanyika kwa jirani zetu wa Kenya.

Vilevile, Uamuzi huu wa Serikali wa kuanza kutumia Treni iliyotumika yenye hali nzuri ni mzuri kutokana na ushindani wa Kibiashara uliopo katika Nchi za Afrika Mashariki ambapo kusubiri Treni Mpya ni kupoteza mapato katika kipindi ambacho reli tayari imekamilika kwa ajili ya matumizi.

Tumuunge mkono Rais wetu mwenye maono chanya ya kuinua Uchumi wa Taifa letu

Mkuu watu wengi wanafikili wataleta bullet train hawajui kwamba bullet train in very expensive, kama ujenzi wake tu wa reli yake ya bullet train inachukua zaidi ya billion 39 Tsh kwa 1km , train yake ni shilingi ngapi,
 
TUTAPOTEZA TUKISUBIRI VICHWA VIPYA VYA TRENI 2023.

Tarehe 04/07/2022 Ikulu Jijini Dar Es Salaam wakati wa Hafla ya Utiaji Saini Mkataba wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) sehemu ya Tabora hadi Isaka, Km 165 njia Kuu na Km 35 njia za kupishana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alieleza nia ya Serikali yake ya kuimarisha Usafiri wa Reli Nchini.

Moja ya kauli iliyotolewa na Mhe. Rais ni kwamba Serikali itanunua Vichwa vya Treni vilivyotumika lakini vikiwa katika hali nzuri ili vianze kutumika wakati tunasubiri Vichwa vipya vilivyoagizwa na Serikali ambavyo vinatarajiwa kuwasili Nchini mwaka 2023.

Ifahamike kuwa, Vichwa vya Treni vya awali vinavyotarajiwa kununuliwa na Serikali vitahifadhiwa na kutumika kama mbadala (Backup) pindi Vichwa vipya vitakapopata hitilafu. Suala hili litasaidia kuendelea kutolewa kwa Huduma za Usafirishaji kama kawaida.

Pili, Gharama za ununuzi wa Vichwa vipya vya Treni ya Mwendokasi ni sawa na kununua Mashangingi 10 mapya na gharama zake zinakadiriwa kufikia Tshs. Bilioni 4 kwa kichwa kimoja.

Tatu, Kihistoria kutokana na gharama kubwa ya ununuzi wa vipuri vipya vya Treni, Tanzania haijawahi kununua Vichwa vipya wala Injini mpya ya Treni tangu enzi za Mkoloni. Ambapo mwaka 1990 Shirika ya Reli ilinunua Injini (Used) namba 826 kutoka Sweden.

Uchumi wa Mataifa yanayoendelea umekuwa kikwazo kwa Nchi zetu kufanya manunuzi ya Vichwa vyote vipya kama ilivyofanyika kwa jirani zetu wa Kenya.

Vilevile, Uamuzi huu wa Serikali wa kuanza kutumia Treni iliyotumika yenye hali nzuri ni mzuri kutokana na ushindani wa Kibiashara uliopo katika Nchi za Afrika Mashariki ambapo kusubiri Treni Mpya ni kupoteza mapato katika kipindi ambacho reli tayari imekamilika kwa ajili ya matumizi.

Tumuunge mkono Rais wetu mwenye maono chanya ya kuinua Uchumi wa Taifa letu

Kwahiyo ndio yake yale, unaagiza vichwa too late, kwanini usiahize mapema ili reli ikiwa tayari na vichwa vianze kutumika?

Ndio yale yale, bwawa la Nyerere halijaanza kujazwa maji, kwahiyo tukikamilisha ujenzi, badala ya kufua umeme itabidi tusubiri mwaka mmoja ndio bwawa lijae
 
Back
Top Bottom