MgungaMiba
JF-Expert Member
- Aug 28, 2011
- 999
- 816
Kwahiyo tukiambiwa tushike ukuta itakuwaje?Kwa sasa tumeshachemsha, hivyo tutalazimika kukubali hata mashariti ambayo pengine tungeweza kuyakataa as long as miradi hii ilikuwa bado haijaanza kutekelezwa.
Uhuru wa nchi utakua na hali gani kama chombo kizito mfano wa jeshi la polisi kuendesha na wageni!japo sijaona polisi wa kihindi au kiarabu tanzania lakini nauliza je mchina hawezi kuwa raia wa zambia na akapatiwa fursa yoyote ile?
Sasa mtu anapita karibu na Ziwa, anasema mimi nafikiri tujenge daraja hapa ziwani anaagiza palepale mchakato uanze na pes zitengwe bila kuangalia kwanza pririty ni nini.
Shilingi bilion 700 za ujenzi wa daraja la Busisi zingeingia kwenye barabara au hata Stieglers zingefanya kitu kikubwa zaidi.
Kule Busisi wananchi walikuwa wanahitaji vivuko vizuri tu kwa sasa kwanza
Hii inatokana na Viongozi wetu mafisadi kununuliwaWachina si wabaya wakati wanatuhumiwa na Internal Labour Organisation ILO kwa kukiuka sheria za kazi na haki za binadamu katika makampuni yao ya Afrika karibu yote.
KWANI IGP WAO ALIKUWA MCHINA AU ASKARI WA KAWAIDA TU NDIYE ALIKUWA MCHINA BADO TUNAMIFUMO AMBAYA KWA DUNIA YA SASA HAINA FAIDA YOYOTE UKINIAMBIA KUAJIRI MCHINA TPDF WAWE WANAJESHI HAPO NITAKATAAUhuru wa nchi utakua na hali gani kama chombo kizito mfano wa jeshi la polisi kuendesha na wageni!
China mfungwa ni kama mtumwa, na biashara ya viungo vya binadamu imeshamiri sana. Wazungu wananunua sana maini ya binadamu kutoka China baada ya unywaji wa pombe uliopitiliza kuharibi maini yao. Waarabu ni figo kutokana na kisukari na magonjwa ya moyo ya muda mrefu. China inatuhumiwa kuuza viungo vya wafugwa kwa wateja kutoka nje. Hili pia limesababishwa na rushwa ya viongozi wetu wa Africa!Hii inatokana na Viongozi wetu mafisadi kununuliwa
Ni kweli. Zambia ni mfano, kuna taarifa kule wamejimilikisha ardhi kufidia madeni.Teyari Wachina wameshaanza kuzengezengea ukiona ndege aina ya tai akizunguka angani sehemu fulani ujue chini kuna mnyama anakaribia kuwa mzoga.
Wanaendesha na shirika la umeme linaitwa ZescoNi kweli. Zambia ni mfano, kuna taarifa kule wamejimilikisha ardhi kufidia madeni.
Sri lanka wamechukua Bandari kufidia deni.Wanaendesha na shirika la umeme linaitwa Zesco
CCM wanaamini kuwa huyu mkoloni ni ndugu yao wa damu!Sri lanka wamechukua Bandari kufidia deni.
Huyu mkoloni mpya toka kwa kina hio!! Haa!! Atatuacha uchi afrika.
Hawa wavimba macho wakikuita rafiki!! Jua ulichonacho ndio rafiki.China Tanzania friendship jina zuri Sana Hawa ni rafiki wa kwel wa raslimali zetu,CCM wanaamini kuwa huyu mkoloni ni ndugu yao wa damu!
Mawazo haya mazuri yapite wapi katika nchi ya mihemuko ya siasa za kipumbavu, pole yetuShida kuu ya tza tumekosa uongozi bora vyote tunavyo. Tumekosa uongozi wenye weledi wa kutumia raslimali zetu kwa kuchochea uzalishaji wa ndani iwe ndo tegemeo na sio misaada ndo iwe tegemeo.
Tungewekeza kwenye kilimo tuilishe dunia tungepata pesa nyingi Sana.
V8 moja isiyo na tija kwa taifa ni sawa na trekta 6 brand new na vifaa vyake zingetumika kufukua ardhi zingezalisha ajira tele na kuleta pesa tele za kigeni Wala tusingehitaji mikopo
Sahihi ni Yale ya kuwashughulikia wapinzani au jinsi ya kuuwa upinzani.Mawazo haya mazuri yapite wapi katika nchi ya mihemuko ya siasa za kipumbavu, pole yetu
1. Je SGR si ilikuwa ikijengwa na Waturuki? Tumevunja mkataba?Binafsi naona serikali hii mpaka sasa imeshajiweka katika mazingira magumu yatayopelekea kukubali mashariti magumu kutoka kwa mtu yoyote (wakiwemo wachina) anaetaka kuwekaza fedha zake katika kukamilisha miradi mikubwa ya awamu ya tano kama ule wa Bwawa la Umeme wa mto Rufiji na ule wa ujenzi wa reli ya kisiasa (SGR).
Hatuna jeuri mbele ya mabeberu. Cha muhimu ni Jiwe kutambua falsafa ya JK "ukitaka kula vya watu kubali kuliwa".Binafsi naona serikali hii mpaka sasa imeshajiweka katika mazingira magumu yatayopelekea kukubali mashariti magumu kutoka kwa mtu yoyote (wakiwemo wachina) anaetaka kuwekaza fedha zake katika kukamilisha miradi mikubwa ya awamu ya tano kama ule wa Bwawa la Umeme wa mto Rufiji na ule wa ujenzi wa reli ya kisiasa (SGR).
Kwa mtazamo wangu, sababu ni hizi:
1. Miradi hii imeshaanza kutekelezwa, hivyo ni lazima tupambane iishe vinginevyo itakuwa ni aibu na pigo kisiasa.
2. Tumeshatangaza kwa umma na dunia kuwa miradi hii ni lazima ikamilike na ahadi hii kwa watanzania teyari ni deni la kisiasa na pia ikifeli ni kete kwa wapinzani.
3. Tumeshaingia mikataba na wakandarasi na sijui kama mikataba tulioingia inatambua kusitishwa kwa mradi wakati wowote ule na kwasababu yoyote ile bila kuwa na gharama ya kusitisha mradi husika.
4. Kitaalamu sijui kama inawezekana/ inashauriwa kusitisha miradi ya aina hii pale inapokuwa tayari imeshaanza kutekelezwa.
5. Kusimamisha miradi hii kwa muda sidhani kama ndio itakuwa ni kusimamisha gharama za mradi kwa asilimia 100 ili hali mitambo na vitu vingine tayari viko site na kazi ya ujenzi tayari ilishaanza.
Hivyo basi, kwa kuzingatia sababu hizo hapo juu na nyingine ambazo inawezekana sijazitaja, sioni kama tutaingia kwenye meza ya mazungumzo tukiwa na jeuri ya kukataa mashariti magumu iwapo yatatolewa na Wachina au mtu mwingine yeyote atakaekuwa tayari kuokoa jahazi kwa kuwekaza fedha zake katika hii miradi.
Vile vile sidhani kama mchina au mtu mwingine yeyote ataacha ku-take advantage ya hali hii kutunyonya tofauti na ku-negotiate wakati mradi/miradi bado haijaanza kutekelezwa.
Tusubiri.