Serikali iangalie namna ya kuwapa Askari elimu ya ushauri nasaha kuhusu VVU

Serikali iangalie namna ya kuwapa Askari elimu ya ushauri nasaha kuhusu VVU

Kwitogelo

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2023
Posts
310
Reaction score
442
Kuna huu utaratibu wa baadhi ya watu hasa askari wengi wanaochukua wanawake ambao siyo wapenzi wala wake zao na kwenda nao kujipima VVU kwa kutumia hivi vipimo vya rapid tests kabla ya kukutana nao kimwili lakini kitu kibaya zaidi hawa askari hawana elimu ya namna ya kuongea na mtu endapo atakutwa na maambukizi kitu kinachopelekea watu hao kushikwa na presha za ghafra na pengine kupoteza na maisha kabisa kutokana na kwamba hawa waathirika wanakuwa wanakosa ushauri wa kisaikolojia(psychological counselling).

Serikali iangalie namna ya kuwapatia hawa askari elimu ya namna ya kuongea na mtu atakaekutwa na VVU mara baada ya kujipima wenyewe kwasababu hakuna namna yoyote ile kwamba watu wasipimane au watumie mipira wakati vipimo vipo.
 
Sasa hapa huwa wanajipima Kama Askari au wao binafsi?
Kwnini usiseme serikali kwa raia wote? Ila ni serilaki kwa Askari?
Unaishi kambini au mpakani?.
Mkuu huu in utafiti nimeufanya;

Watu ambao siyo askari wengi huwa hawana hayo mambo ya kupimana na wengi hutumia mipira.

Nimeongelea hawa askari kwasababu wengi wanachukua wanawake wa huku uraiani na ndyo wanaopenda kutumia hizi rapid tests.

Kwasababu hawa askari wanaweza kupewa elimu hii kwa muda mfupi kwasababu wanakuwa kwenye groups na ndyo wanaotumia hizi tests ndyo maana uzi wangu umelenga huko.
 
Back
Top Bottom