Salaam!
Naomba kutoa hoja hii kuhusu barabara tajwa! Ina changamoto kubwa sana ya msongamano wa magari makubwa na madogo. Na hii inatokana na ufinyu wa barabara kutokana na mahitaji ya sasa. Tunaiomba serikali iangalie uwezekano wa kuikamilisha barabara hii kwa njia nne kuanzia ilipoishia eneo la Tengeru hadi njia panda ya Himo.
Lengo pia la hoja hii ni kutokana pia na umuhimu wa barabara barabara hii ktk sekta ya utalii ambayo inaiingizia serikali mapato mengi sana. Watalii wengi wanaotumia barabara hii kutoka uwanja wa ndege wa Kilimanjaro kwenda kupanda mlima K'njaro au kwenda mbuga za wanyama zilizopo ukanda wa kaskazini. Wanalalamikia wingi wa vibao vya speed limit (50kph) vilivyojaa njia nzima,ambavyo kiuhalisia vimewekwa kudhibiti mwendo kutokana na barabara hii kuwa jinsi ilivyo kwasasa kwa kuongezeka kwa makazi ya watu pembezoni mwa barabara.
Hali ambayo ingeweza kudhibitika kwa kuweka hizo njia 4 Kisha kuweka uzio katikati na kuijenga madaraja juu kwa ajili ya wavuka kwa miguu na kuruhusu magari kupita angalau kwa 80 kph speed. Hali ambayo itaokoa muda mwingi wa safari unaopotea kwa watumiaji wa barabara hii. Tuige kwa jirani zetu Kenya mfano wa barabara ya Thika super highway Kuna hadi 110kph na barabara imepita kwenye eneo la makazi ya watu. Tunatambua serikali Ina uwezo wa kutekeleza jambo hili kutokana na umuhimu wake.
Jambo lingine ni wingi wa traffic police na speed torch za kuvizia kwenye barabara hii. Jambo ambalo ninaamini ni kutokana na jinsi barabara hii kuwa jinsi ilivyo. Hivyo kulazimu kudhibiti mwendo wa magari Ili kupunguza ajali. Ila kama miundombinu hii ikiwekwa sawa kwa njia 4 na kuijenga madaraja ya juu, na vibao vya onyo kuzuiwa waenda kwa miguu kuhakikisha wanavuka kupitia madaraja yatakayojengwa kwa juu, hizo speed za 59 kph hazitakuwa na haja ya kuwepo.
Angalau serikali kupitia Tanroads waonyeshe weledi wao sasa kukabiliana na changamoto hizi zinazo dhibitika. Wageni wa nchi za nje wakipita na kuona hali hizi wanatucheka na kutudharau sana. Tunasafiri nao mara nyingi tunawasikia wakizungumza. Serikali amkeni tuijenge nchi yetu. Naomba kuwasilisha kwa wahusika waliopo humu wafikishe kwa viongozi wakuu.
Naomba kutoa hoja hii kuhusu barabara tajwa! Ina changamoto kubwa sana ya msongamano wa magari makubwa na madogo. Na hii inatokana na ufinyu wa barabara kutokana na mahitaji ya sasa. Tunaiomba serikali iangalie uwezekano wa kuikamilisha barabara hii kwa njia nne kuanzia ilipoishia eneo la Tengeru hadi njia panda ya Himo.
Lengo pia la hoja hii ni kutokana pia na umuhimu wa barabara barabara hii ktk sekta ya utalii ambayo inaiingizia serikali mapato mengi sana. Watalii wengi wanaotumia barabara hii kutoka uwanja wa ndege wa Kilimanjaro kwenda kupanda mlima K'njaro au kwenda mbuga za wanyama zilizopo ukanda wa kaskazini. Wanalalamikia wingi wa vibao vya speed limit (50kph) vilivyojaa njia nzima,ambavyo kiuhalisia vimewekwa kudhibiti mwendo kutokana na barabara hii kuwa jinsi ilivyo kwasasa kwa kuongezeka kwa makazi ya watu pembezoni mwa barabara.
Hali ambayo ingeweza kudhibitika kwa kuweka hizo njia 4 Kisha kuweka uzio katikati na kuijenga madaraja juu kwa ajili ya wavuka kwa miguu na kuruhusu magari kupita angalau kwa 80 kph speed. Hali ambayo itaokoa muda mwingi wa safari unaopotea kwa watumiaji wa barabara hii. Tuige kwa jirani zetu Kenya mfano wa barabara ya Thika super highway Kuna hadi 110kph na barabara imepita kwenye eneo la makazi ya watu. Tunatambua serikali Ina uwezo wa kutekeleza jambo hili kutokana na umuhimu wake.
Jambo lingine ni wingi wa traffic police na speed torch za kuvizia kwenye barabara hii. Jambo ambalo ninaamini ni kutokana na jinsi barabara hii kuwa jinsi ilivyo. Hivyo kulazimu kudhibiti mwendo wa magari Ili kupunguza ajali. Ila kama miundombinu hii ikiwekwa sawa kwa njia 4 na kuijenga madaraja ya juu, na vibao vya onyo kuzuiwa waenda kwa miguu kuhakikisha wanavuka kupitia madaraja yatakayojengwa kwa juu, hizo speed za 59 kph hazitakuwa na haja ya kuwepo.
Angalau serikali kupitia Tanroads waonyeshe weledi wao sasa kukabiliana na changamoto hizi zinazo dhibitika. Wageni wa nchi za nje wakipita na kuona hali hizi wanatucheka na kutudharau sana. Tunasafiri nao mara nyingi tunawasikia wakizungumza. Serikali amkeni tuijenge nchi yetu. Naomba kuwasilisha kwa wahusika waliopo humu wafikishe kwa viongozi wakuu.