dubu
JF-Expert Member
- Oct 18, 2011
- 3,502
- 3,483
Salaam Wakuu,
Napenda kujua ni namna gani Serikali imejipanga kuwajumlisha Watoto wa Mtaani kwenye Sensa ya Taifa ili na wao wapate nafasi ya kuhudumiwa kama watu wengine.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepanga kufanya Sensa ya Watu na Makazi ifikapo mwezi Agosti 2022. Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), ipo kwenye maandalizi ya kufanya Sensa hiyo. Sensa ya Watu na Makazi ni zoezi la kitaifa linalofanyika kila baada ya miaka 10 ambapo Sensa ya mwisho kufanyika nchini ni ile ya mwaka 2012. Hivyo Sensa ya mwaka 2022 itakuwa ni sensa ya Sita kufanyika nchini baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964. Sensa nyingine zilifanyika mwaka 1967, 1978, 1988, 2002 na 2012.
Tanzania na Dunia kwa ujumla wake kuna tatizo kubwa la Watoto wa Mitaani na Watoto wasio na Makazi Maalum. Watoto wa mitaani ni watoto ambao wanategemea mitaani kwa ajili ya maisha yao ya kila siku kama kulam kuvaa, kulala, kujitibia, kupata misaada nk.
kuna sababu nyingi za wao kuwa mtaani na kila mtoto ana hadithi yake ya kipekee. Sababu za kuwa mitaani zitatofautiana kutoka na jiji hadi jiji, na kutoka kwa mtu hadi mtu.Sababu kubwa za kuwa Mtaani ni umaskini na kuvunjika kwa familia
vifo vya wazazi, kutelekezwa na wazazi na mambo mengine ya kijamii kama vile unyanyasaji wa watoto nyumbani au ndani ya jamii. Ubaguzi, ukosefu wa haki, ukosefu wa hadhi ya kisheria. Sababu nyingine zinazosababisha kuhamia mtaani ni kama: Unyanyasaji wa kijinsia, kimwili au kihisia, kulazimishwa kufanya uhalifu, kukataliwa na familia zao kwa sababu zinazoitwa "maadili", masuala ya afya ya akili na wengine ulemavu nk.
Watoto wa Mitaani wanadhuriwa kila siku na watu wazima, wakiwemo maafisa wa serikali, polisi, na hata familia zao wenyewe.Watoto wa Mitaani Wanabakwa na kulawitiwa sababu usalama wao ni mdogo. Pia wananyimwa fursa ya kupata elimu na huduma za afya, kitaifa zinaharamisha kuomba au kuzurura, wanaweza kufungwa jela kwa kujaribu tu kuishi. Hawana Mtetezi.
Hivi Karibuni, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dk. Doroth Gwajima, alisema katika kukabiliana na ongezeko la watoto wa mitaani, Serikali imeunda kamati mbalimbali ili kushughulikia watoto hao wasiweze kuongezeka. Akaonya kuwa wazazi waache kuwatumikisha watoto kwa kuwatuma kuomba mitaani.
Pia, alisema katika Mkoa wa Dar es Salaam pekee, Serikali imetambua watoto 5,390 kati yao, wavulana ni 3,452 na wasichana 1,538 ambao tayari wamepewa huduma mbalimbali ikiwemo vifaa vya shule na huduma mbambali za kuimrisha pato la kaya zao. alisema watoto 135 wameunganishwa na familia zao, wasichana walikuwa 43 na wavulana 92.
Kuna tatizo la watoto wanaoshi mitaani hasa katika miji mikubwa kama Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya, Iringa na Dodoma. Hizi Takwimu hapa chini ni kwa Dar Es Salaam tu. Vipi Nchi nzima?
Naiomba Serikali iweke Mkakati na Mkazo Maalum wa kuhakikisha Watoto wa Mtaani Wanatambuliwa na Kusadiwa. Pia wahesabiwe kwenye hii Sensa
Hawa ambao wametambuliwa na hawajasaidiwa wameenda wapi?
Napenda kujua ni namna gani Serikali imejipanga kuwajumlisha Watoto wa Mtaani kwenye Sensa ya Taifa ili na wao wapate nafasi ya kuhudumiwa kama watu wengine.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepanga kufanya Sensa ya Watu na Makazi ifikapo mwezi Agosti 2022. Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), ipo kwenye maandalizi ya kufanya Sensa hiyo. Sensa ya Watu na Makazi ni zoezi la kitaifa linalofanyika kila baada ya miaka 10 ambapo Sensa ya mwisho kufanyika nchini ni ile ya mwaka 2012. Hivyo Sensa ya mwaka 2022 itakuwa ni sensa ya Sita kufanyika nchini baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964. Sensa nyingine zilifanyika mwaka 1967, 1978, 1988, 2002 na 2012.
Tanzania na Dunia kwa ujumla wake kuna tatizo kubwa la Watoto wa Mitaani na Watoto wasio na Makazi Maalum. Watoto wa mitaani ni watoto ambao wanategemea mitaani kwa ajili ya maisha yao ya kila siku kama kulam kuvaa, kulala, kujitibia, kupata misaada nk.
kuna sababu nyingi za wao kuwa mtaani na kila mtoto ana hadithi yake ya kipekee. Sababu za kuwa mitaani zitatofautiana kutoka na jiji hadi jiji, na kutoka kwa mtu hadi mtu.Sababu kubwa za kuwa Mtaani ni umaskini na kuvunjika kwa familia
vifo vya wazazi, kutelekezwa na wazazi na mambo mengine ya kijamii kama vile unyanyasaji wa watoto nyumbani au ndani ya jamii. Ubaguzi, ukosefu wa haki, ukosefu wa hadhi ya kisheria. Sababu nyingine zinazosababisha kuhamia mtaani ni kama: Unyanyasaji wa kijinsia, kimwili au kihisia, kulazimishwa kufanya uhalifu, kukataliwa na familia zao kwa sababu zinazoitwa "maadili", masuala ya afya ya akili na wengine ulemavu nk.
Watoto wa Mitaani wanadhuriwa kila siku na watu wazima, wakiwemo maafisa wa serikali, polisi, na hata familia zao wenyewe.Watoto wa Mitaani Wanabakwa na kulawitiwa sababu usalama wao ni mdogo. Pia wananyimwa fursa ya kupata elimu na huduma za afya, kitaifa zinaharamisha kuomba au kuzurura, wanaweza kufungwa jela kwa kujaribu tu kuishi. Hawana Mtetezi.
Hivi Karibuni, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dk. Doroth Gwajima, alisema katika kukabiliana na ongezeko la watoto wa mitaani, Serikali imeunda kamati mbalimbali ili kushughulikia watoto hao wasiweze kuongezeka. Akaonya kuwa wazazi waache kuwatumikisha watoto kwa kuwatuma kuomba mitaani.
Pia, alisema katika Mkoa wa Dar es Salaam pekee, Serikali imetambua watoto 5,390 kati yao, wavulana ni 3,452 na wasichana 1,538 ambao tayari wamepewa huduma mbalimbali ikiwemo vifaa vya shule na huduma mbambali za kuimrisha pato la kaya zao. alisema watoto 135 wameunganishwa na familia zao, wasichana walikuwa 43 na wavulana 92.
Kuna tatizo la watoto wanaoshi mitaani hasa katika miji mikubwa kama Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya, Iringa na Dodoma. Hizi Takwimu hapa chini ni kwa Dar Es Salaam tu. Vipi Nchi nzima?
Naiomba Serikali iweke Mkakati na Mkazo Maalum wa kuhakikisha Watoto wa Mtaani Wanatambuliwa na Kusadiwa. Pia wahesabiwe kwenye hii Sensa
Hawa ambao wametambuliwa na hawajasaidiwa wameenda wapi?