Serikali imeona wabunge wamepuyanga bungeni imerudi kukusanya maoni kwa wenye akili timamu

Serikali imeona wabunge wamepuyanga bungeni imerudi kukusanya maoni kwa wenye akili timamu

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Tuliona walichofanya wabunge Dodoma; tumeona wanachofanya wanazuoni kutoka kwenye dini na fani mbalimbali nchini. Wanajadili mule mule alipopita Mzee Mbowe na Lissu, tofauti ni kwamba wanazuoni wanawapiga shule mawaziri wakati wabunge waliwapigia makofi mawaziri bila kuwapa maarifa mapya.

Hiki kinachoendelea ni fedheha kwa bunge na wabunge; kwamba pamoja na kupitisha kumbe wao siyo final bali kazi yao ilikuwa rubber stamp au kukamilisha ratiba.

Goma limekuwa gumu na endapo Mbowe na Safu yao wataingia uwanjani kwenye mikutano ya adhara kwa agenda hii upo uwezekano pakatokea mmomonyoko mkubwa na makundi kuhusu bandari.

Changamoto kubwa ya Watanzania ni wanafiki wazuri; wakiona unataka kusikia habari hoja fulani nao wanakupigia makofi ila moyoni wana ukweli na wewe ukijiongezea unagundua huna watu nyuma yako.

Magufuli alisifika ila waliokuwa wanamsifu angewaruhusi wapige kura ya siri angelalamika kaibiwa kura kwa sababu baada ya kuondoka tu watu walewale waliokuwa mgongoni mwake walijitokeza kumkataa.

Kama walimkataa hadharani akiwa ameondoka je, walimpigia kura sirini? Kwa kuwa alifahamu fika kwamba amewakosea Watanzani aidha akiwa na nia nzuri au mbaya ndipo akaona njia sahihi ni kuchafua uchaguzi.

Kwa mantiki hii, hakuna mwenye uhakika wa nani ambaye anamkubali kiongozi wa CCM sirini. Wote tumebaki kusikia uungwaji mkono wa majukwaani ila unapokuja sirini hakuna mwenye uhakika wa kutoboa. Hii inatokana na ukweli kwamba tumewaweka makovu Watanzania kwa muda mrefu kwa kuwaaminisha tunafanya uwekezaji wenye tija matokeo yake hakuna tija.

Kwa hatua za awali Mhe. Rais ameona walipokosea wasaidizi wake, amejifunza kwa ndani nini jamii inataka, amewasikia viongozi wa kijamii na imani wanasimamia nini, lakini amewasikia wale wasaidizi wake bungeni walichangia nini; obviously amebaini wanaompotosha na kumchonganisha na jamii siyo wapinzani bali wasaidizi wake.

Inatia hasira unapodhani una wataalam wazuri kisha unagundua kazi waliyofanya inapigwa vita na kila msomi; swali la kujiuliza, hao wasomi walioteuliwa kukusaidia wameelimika? Wana exposure au wapo kwa sababu wapo?

Naamini soon Mwanasheria Mkuu wa Serikali na timu yake watapisha ofisi kwa kilichotokea, vinginevyo ikibainika mkataba haukuwa shirikishi, pamoja na kiburi cha kibinadamu bora tuchelewe kufika kuliko tufike tukiwa siyo wamoja.

Padri Kutima ametueleza Somalia na Sudan, mimi nataka niongeze Loliondo na Tarime mgodini, je, tunadhani ni nia zote nzuri ni nia nzuri?
 
Mh.Rais SSH ana mtihani mkubwa sana.....ila atauvuka aaamin aaamin[emoji120]

Maswali fikirishi.

Hivi wazanzibari ni raia wa daraja la pili katika JMT?!!!

Mbona wanaposhika madaraka makubwa huwa wanashambuliwa sana kwa hoja kuwa UWEZO WAO WA KIUONGOZI NI MDOGO...HAWANA MAAMUZI....WANAUZA NCHI....?!!!

Watanzania wasio wabaguzi wawe makini sana na haya mambo.....

#SayNoToRacism
#SayNoToBigotry

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mh.Rais SSH ana mtihani mkubwa sana.....ila atauvuka aaamin aaamin[emoji120]

Maswali fikirishi......

Hivi wazanzibari ni raia wa daraja la pili katika JMT?!!!

Mbona wanaposhika madaraka makubwa huwa wanashambuliwa sana kwa hoja kuwa UWEZO WAO WA KIUONGOZI NI MDOGO...HAWANA MAAMUZI....WANAUZA NCHI....?!!!

Watanzania wasio wabaguzi wawe makini sana na haya mambo.....

#SayNoToRacism
#SayNoToBigotry

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

..daraja la pili ni sisi Watanganyika ambao tumenyimwa kuwa na serikali yetu.

..pia tumenyimwa kuwa na vitambulisho vya Tanganyika, lakini Zanzibar wana vitambulisho vyao.

..Mtanganyika hata uwe msomi kiasi gani huwezi kuajiriwa au kuteuliwa ktk serikali ya Zanzibar, ingawa tunaambiwa ni nchi moja.
 
..daraja la pili ni sisi Watanganyika ambao tumenyimwa kuwa na serikali yetu.

..pia tumenyimwa kuwa na vitambulisho vya Tanganyika, lakini Zanzibar wana vitambulisho vyao.

..Mtanganyika hata uwe msomi kiasi gani huwezi kuajiriwa au kuteuliwa ktk serikali ya Zanzibar, ingawa tunaambiwa ni nchi moja.
Kwani NIDA ni ya Zanzibar??
 
Swala la bandari utadhani DP world ilisaini na vipofu..

Ni wazi mtu mwenye akili timamu hawezi saini mkataba wa kijinga kama huu..

Kuna kila dalili za upendeleo either kwa rushwa au kwa sababu tuu wana dini zinazo fanana
 
..daraja la pili ni sisi Watanganyika ambao tumenyimwa kuwa na serikali yetu.

..pia tumenyimwa kuwa na vitambulisho vya Tanganyika, lakini Zanzibar wana vitambulisho vyao.

..Mtanganyika hata uwe msomi kiasi gani huwezi kuajiriwa au kuteuliwa ktk serikali ya Zanzibar, ingawa tunaambiwa ni nchi moja.
Huyu anaweza kuwa Rais wa mwisho kutoka zanzibar kutawala Tanganyika
 
Mh.Rais SSH ana mtihani mkubwa sana.....ila atauvuka aaamin aaamin[emoji120]

Maswali fikirishi......

Hivi wazanzibari ni raia wa daraja la pili katika JMT?!!!

Mbona wanaposhika madaraka makubwa huwa wanashambuliwa sana kwa hoja kuwa UWEZO WAO WA KIUONGOZI NI MDOGO...HAWANA MAAMUZI....WANAUZA NCHI....?!!!

Watanzania wasio wabaguzi wawe makini sana na haya mambo.....

#SayNoToRacism
#SayNoToBigotry

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Hili liko wazi wanauwezo mdogo sana wa kiakili,we huoni tofauti yake na jpm,kwanza hata shule zao ndio zinaongoza kwa wanafunzi wanaofeli tz nzima.
 
Tuliona walichofanya wabunge Dodoma; tumeona wanachofanya wanazuoni kutoka kwenye dini na fani mbalimbali nchini. Wanajadili mule mule alipopita Mzee Mbowe na Lissu, tofauti ni kwamba wanazuoni wanawapiga shule mawaziri wakati wabunge waliwapigia makofi mawaziri bila kuwapa maarifa mapya.

Hiki kinachoendelea ni fedheha kwa bunge na wabunge; kwamba pamoja na kupitisha kumbe wao siyo final bali kazi yao ilikuwa rubber stamp au kukamilisha ratiba.

Goma limekuwa gumu na endapo Mbowe na Safu yao wataingia uwanjani kwenye mikutano ya adhara kwa agenda hii upo uwezekano pakatokea mmomonyoko mkubwa na makundi kuhusu bandari.

Changamoto kubwa ya Watanzania ni wanafiki wazuri; wakiona unataka kusikia habari hoja fulani nao wanakupigia makofi ila moyoni wana ukweli na wewe ukijiongezea unagundua huna watu nyuma yako.

Magufuli alisifika ila waliokuwa wanamsifu angewaruhusi wapige kura ya siri angelalamika kaibiwa kura kwa sababu baada ya kuondoka tu watu walewale waliokuwa mgongoni mwake walijitokeza kumkataa.

Kama walimkataa hadharani akiwa ameondoka je, walimpigia kura sirini? Kwa kuwa alifahamu fika kwamba amewakosea Watanzani aidha akiwa na nia nzuri au mbaya ndipo akaona njia sahihi ni kuchafua uchaguzi.

Kwa mantiki hii, hakuna mwenye uhakika wa nani ambaye anamkubali kiongozi wa CCM sirini. Wote tumebaki kusikia uungwaji mkono wa majukwaani ila unapokuja sirini hakuna mwenye uhakika wa kutoboa. Hii inatokana na ukweli kwamba tumewaweka makovu Watanzania kwa muda mrefu kwa kuwaaminisha tunafanya uwekezaji wenye tija matokeo yake hakuna tija.

Kwa hatua za awali Mhe. Rais ameona walipokosea wasaidizi wake, amejifunza kwa ndani nini jamii inataka, amewasikia viongozi wa kijamii na imani wanasimamia nini, lakini amewasikia wale wasaidizi wake bungeni walichangia nini; obviously amebaini wanaompotosha na kumchonganisha na jamii siyo wapinzani bali wasaidizi wake.

Inatia hasira unapodhani una wataalam wazuri kisha unagundua kazi waliyofanya inapigwa vita na kila msomi; swali la kujiuliza, hao wasomi walioteuliwa kukusaidia wameelimika? Wana exposure au wapo kwa sababu wapo?

Naamini soon Mwanasheria Mkuu wa Serikali na timu yake watapisha ofisi kwa kilichotokea, vinginevyo ikibainika mkataba haukuwa shirikishi, pamoja na kiburi cha kibinadamu bora tuchelewe kufika kuliko tufike tukiwa siyo wamoja.

Padri Kutima ametueleza Somalia na Sudan, mimi nataka niongeze Loliondo na Tarime mgodini, je, tunadhani ni nia zote nzuri ni nia nzuri?
Ahsante sana kwa hoja zako nzuri, kinachoenda kufanyika ni ubabaishaji tu, na ndio maana hawataki kujibu maswali ya msingi badala yake wanakazania tu tuwe na imani na wawekezaji na inavyoonekana mwekezaji ndiye kaandaa mkataba na wanaogopa kuondoa baadhi ya vipengele ili mwekezaji asije akakasilika.Jamani, tumesema chakula ni kibovu, kina wadudu lkn unajibiwa chakula kitakuwa kinaletwa kwa wakati na kila mtu atapata sahani nzima, je hilo ndilo jibu la swali/,dukuduku letu?
 
Hili liko wazi wanauwezo mdogo sana wa kiakili,we huoni tofauti yake na jpm,kwanza hata shule zao ndio zinaongoza kwa wanafunzi wanaofeli tz nzima.
Chuki huuviza moyo wako mwenyewe....uzuri hatujakuja duniani kupendwa na binadamu wote....

Kwa akili yako kubwa kabisa karne hii ya 21 unaamini kabisa kuwa kuna nchi raia wake wana " low IQ"

#MamAnaupigaMwingi[emoji7]

#Siwezi Kuizuia Chuki iwakayo Moyoni Mwako Dhidi Ya Ndugu Zetu Wa Zanzibar

#SiempreJMT[emoji120]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mh.Rais SSH ana mtihani mkubwa sana.....ila atauvuka aaamin aaamin[emoji120]

Maswali fikirishi......

Hivi wazanzibari ni raia wa daraja la pili katika JMT?!!!

Mbona wanaposhika madaraka makubwa huwa wanashambuliwa sana kwa hoja kuwa UWEZO WAO WA KIUONGOZI NI MDOGO...HAWANA MAAMUZI....WANAUZA NCHI....?!!!

Watanzania wasio wabaguzi wawe makini sana na haya mambo.....

#SayNoToRacism
#SayNoToBigotry

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Soo wazanzibari tu, watu wa pwani wote hawana uwezo wa uongozi. Matokeo ya utawala wa waarabu kwa watu wa pwani ni mkubwa sana.

Waarabu waliharibu uwezo wa watu wa pwani, ndio maana wengi hawajioni kama waafrika, wanajiona kama waarabu tu. Nenda Zanzibar kila mtu anafikiri kwao ni Oman.

Tumekua na mwinyi, mikataba yote ya hovyo hovyo, kuuza nchi na mambo yasiyo na maana yalianzia kwake, tukaja kikwete, nchi ilijaa rushwa, ufisadi wa kutisha, mikataba isiyo na kichwa wala miguu, wizi wa wazi wazi, magenge ya wezi wa mali za umma yalishamiri, kama Samia mwendo ni ule ule, kuuza nchi kwa waarabu, mikataba ya ajabu ajabu hapo ana miaka 2 tu, akifikisha 10 hii nchi itakuwepo kweli?

Watu wanaofikiri kwao ni oman wanakujaje kufanya maamuzi makubw ahivyo kuhusu mustakabali wa nchi yetu sisi ambao kwetu ni hapa hapa, hatuna pa kwenda.
 
Back
Top Bottom