Serikali imeshindwa kabisa kusimamia sekta ya usafiri wa pikipiki (bodaboda)!

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,207
Reaction score
13,839
Kama kuna usafiri unaotumiwa na watu wa hali ya kawaida na chini kwa wingi ni pikipiki, tunazoziita bodaboda.

Huduma hii ni rahisi, haraka na unafika uendako kwa kasi sana ukilinganisha na usafiri binafsi au hata mabasi ya Mwendokasi(DART).

Lakini sekta hii haina uratibu wa aina yoyote nchini, si serikali kuu wala serikali za Mita na hata Jeshi letu la Polisi au wasimamizi wa usafiri LART.

Ni aibu kubwa kwamba itabidi mzungu aje atufundishe jinsi ya kudhiti na kuendeleza huu usafiri pendwa kwa wengi.

Chama Tawala kinawatumia bodaboda kama mtaji wa kisiaa, bila kuangalia athari zake kwa usalama wa hao vijana na abiria wao kwa ujumla.

Wahusika wakuu ni kama ifuatavyo:

1. TRA- Wanasajili tu bodaboda na kuzipa namba bila kuweka ukomo.

2. LATRA-Hawajui wafanye nini juu ya bodaboda maana hawajui hata waanzie wapi kuziratibu.

3. Serikali za Mitaa-Halmashauri hazitengi bodaboda zitumike vipi na wapi, wao hata leseni za biashara kwa bodaboda hawakagui.

4. POLISI - Hawa ndio kabisaa wamenyanyua mikono, hwawagusi bodaboda na sasa bodaboda ni kama panya anyechezea sharubu za paka mchana kweupe.
Sheria zipo,
Leseni - zaidi ya 40% ya bodaboda hawana leseni
Helmet - boda boda karibia 90% hakuna
Viatu - ndala ndio vazi kuu
Protective clothing - hakuna
Eye shields - hakuna

Kutokana na makosa hayo yanayotazamwa tu, boda boda wengi kama sio wote, wakifanya ajali, kitu cha kwanza ni kukimbia! Polisi wapo tu!

5. CCM- Sasa watambue kuwa mtaji wa bodaboda kisiasa umekuwa kero kuwa katika jamii. Lazima hatua za kisiasa zitumike kuwadhibiti na kuratibu kistaarabu.

Ajali iliyotokea leo Morogoro Road karibu na Fire, ni uthibitisho wa jinsi serikali kwa ujumla ilivyoshindwa kupanga na kuliweka katika mipango inayoeeweka usafiri huu wa Bodoboda.

USHAURI WANGU
Serikalini kuna ma PhD mengi tu hadi kwa viongozi wetu,ma PhD ya kuombea na kupata kazi, lakini wenye nayo hawajui waanzie wapi kiujumla namna ya kusaidia katika tatizo kama hili la kijamii, kazi na vijana.

Hivyo kwa vile sisi hatuna werevu wa kujtatulia haya matatizo, tutafute mzungu atufikirie nmna ya kuwapanga hawa vijana wa bodaboda na kupunguza vifo na vurugu katika Jamii.

 
Ccm ilishashindwa kuongoza muda mrefu tu.

Sasa hao Bodaboda ndio kafara la Jini Ccm linapotaka kunywa damu, ndio maana wakawajaza ujinga eti ni maafisa usafirishaji.

Godbless Lema alishasema ukweli akazushiwa propaganda, sasa wacha selemara tupige pesa ya majeneza.


 
Kweli nimeamini wabongo wamechoka na maisha mada haiendani na ulichokiandika.
 
Ndugu yangu umeingia Tanzania leo? Ni CCM ndiyo unaipa hiyo challenge? Wana muda? Ni hivi: hakuna kitakachobadilika kama CCM itaendelea kupora madaraka. Uistegemee chochote na zaidi hali itazidi kuwa mbaya. Labda faraja ni kwamba hao wakina bodaboda ni jeshi litakaloitoa CCM kwenye madaraka siku zijazo. Ni lini sijui na nadhani kila mtu hajui.
 
Bodaboda... kazi pekee iliyokua imebaki kwa mtu asiekua na fani, Connection au elimu ila kutokana na ukosefu wa ajira kuna Bodaboda wana master's.
Ni kweli lakini lazima serikali iirasimishe ili iweze kuwa endelevu na vijana wajiajiri kwa misingi inayoeleweka na ustaarabu.
 
Tatizo mtailaumu serikali bure tu kama mtu unajua thamani ya uhai wa maisha yako lazima utafata sheria za barabarani
ipasavyo ikiwemo kuto sababisha ajari kwa wengine wanaokuzunguka uwapo barabarani.


Bodaboda wengi hawana elimu ya darasani ya uendeshaji vyombo vyao na ukiangalia wengi ni vijana matumizi ya vinywaji vikali pia huchangia ajali.


hakuna wa kuthamini maisha yako zaidi yako wewe mwenyewe
 
Serikali ingetimiza wajibu wake ipasavyo, wasio na elimu/ujuzi wa hivyo vyombo hawangekuwa na leseni na na wasingekuwa barabarani. Halikadhalika walevi hawangekuwa barabarani.
 
Kwa serikali na polisi, bodaboda ni mfupa uliomshinda fisi kuutafuna!
 
Wazungu huwa wanawashangaa sana bodaboda wetu jinsi walivyo rafu barabarani
 
Huelewei wajibu wa serikali,
Poor you.
 
Dr Samia ( tunakusamhe kwa sasa),Dr Mwigulu(Fedha) na Prof Kitila Mkumbo(Mipango) , Dr Biteko, mupoo?
Na watetezi Dr Msukuma, Dr Tulia(Spika), hatusikii hoja juu ya hili!
 
Unajua maana ya uongozi? Kwa nini hata nchi zenye ustaarabu mkubwa kunakuwa na sheria za barabarani na polisi wa kusimamia? Kwa nini wasiseme kila mtu athamini maisha yake na waache kujishughulisha kutunga sheria na kufuatilia?
 
Badala ya kuwaambi waratibu Usafiri wa Bodaboda kitu ambacho ni sustainable ni kufanya yafuatayo:-
  • Kuwa na usafiri urafiki na efficient kwa mwananchi (hii itaondoa uhitaji wa watu kutumia hiko chombo kama abiria)
  • Kuhakikisha kuna ajira zenye ujira (hii itaondoa watu kuendelea kubangaiza na kufanya shughuli yoyote hata hatarishi ili mkono uende kinywani...
Tofauti na hapo ni kama una-prune magugu badala ya kuyangoa... AKA Bandaiding a leg which needs amputation....
 
Huwa nashangaa sana serikali imekaa kimya suala hili la boda. Yaani ni kama wana serikali yao na ulimwengu wao. Hawajali sheria hawafuati taa za barabarani yan ni vurugu tupu.

Huwa nawahurumia sana watoto wadogo wa shule, wanafundishwa jinsi ya kuvuka barabara Kwenye zebra au hata kama hakuna zebra wanaelekezwa jinsi ya kuvuka. Boda hawajali lolote kuwa kuna upande taa zimeruhusu watembea kwa miguu kuvuka dah yan shida tu.

Sisemi kuhusu kuchomekea magari ni shida, anakuvhomekea ukimgonga anakuambia kwani hujaniona hapo kavunja taa bumper nk hana leseni hana bima yan shida tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…