Serikali imetangaza kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa uko palepale licha ya malalamiko mengi kutaka usifanyike

Serikali imetangaza kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa uko palepale licha ya malalamiko mengi kutaka usifanyike

Doctor Mama Amon

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2018
Posts
2,089
Reaction score
2,725
Waziri Mkuu akoleza uchaguzi serikali za mitaa
Mwananchi, Ijumaa, November 15 2019, Dodoma.
1573898812621.png

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Majaliwa Kassim Majaliwa

Hakuna kulala uchaguzi wa serikali za mitaa uko palepape. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya kauli ya Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa kuliambia Bunge leo Ijumaa Novemba 15, 2019 kuwa Watanzania wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi huo utakaofanyika Novemba 24, 2019.

Akitoa hotuba ya kuahirisha mkutano wa 17 wa Bunge, Majaliwa amesisitiza Watanzania kujitokeza na kuwachagua viongozi wanaowapenda kwa ajili ua kuwatumikia.

Baadhi ya vyama vya siasa na wanaharakati wamekuwa wakilalamikia dosari kadhaa katika uchaguzi wakiomba usitishwe ili vyama vijadiliane.

Vyama vingine vimetangaza kujitoa katika uchaguzi huo na kuomba majina na nembo za wagombea wao visitumike kwenye uchaguzi huo.

Katika maeneo mengi, chama tawala cha CCM kimepita bila kupigwa katika vitongoji, mitaa na vijiji kutokana na sababu mbalimbali.

Vyama vilivyokwisha kutangaza kususia uchaguzi huo ni; Chadema, CUF, ACT- Wazalendo, NCCR-Mageuzi, NLD, UPDP na Chaumma.

Chanzo: Mwananchi
 
Ni uchaguzi au kutangaza waliochaguliwa na tume ya uchaguzi
 
Je, ni sahihi kwa Taifa kuingia gharama za uchaguzi katika maeneo ambako asilimia 99.9 ni wagombea wa CCM pekee?

Narejea takwimu rasmi za serikali zilizotolewa na Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Jaffo. Alise kuwa CCM walisimika wagombea kwa 74%, CHADEMA wakasimika wagombea kwa 19%, CUF wakasimika 4%, ACT wakasimika 1.5%, NCCR wakasimika 0.4%, na vyama vingine (NLD, CCK, UPDP, SAU CHAUMA na TLP) wakasimika 0.1%. Tayari HADEMA , CUF, ACT , NCCR, NLD na UPDP wamejitoa kwenye uchaguzi. Kwa hiyo, kwa mujibu wa takwimu hizi, sehemu ya nchi itakayoshuhudia uchaguzi wenye mchuano kati ya CCM na vyama baki haiwezi kuzidi 0.1%.

Katika mazingira haya, Watanzania wamegawanyika katika kambi mbili. Kambi ya Kina Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania, wanasema kampeni za uchaguzi uendelee katika maeneo yote. Kambi ya pili ni wale wanaosema hapana. Nani yuko sahihi?
 
Waendelee kususa sisi tuendelee na uchaguzi

Ngoma droo

State agent
 
Back
Top Bottom