Mwalimu wa tuisheni
JF-Expert Member
- Oct 19, 2019
- 6,602
- 10,801
Wenzake wakienda huko ndo sehemu ya kutokea kurudi na medali na kupanda vyeo yeye anaenda kujivunja, shenzi kabisa 🚮🚮He's the one.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wenzake wakienda huko ndo sehemu ya kutokea kurudi na medali na kupanda vyeo yeye anaenda kujivunja, shenzi kabisa 🚮🚮He's the one.
Alphonce Simbu hana mazoezi ya kutosha, hana mafunzo mazuri na pia hana maandalizi ya kutosha kushindana na vijana wadogo."Leo nimegundua kuwa kumbe Mazoezi niliyoyafanya hayakuwa sahihi Kwangu na nilipofika Kilomita ya 30; kuelekea ya 35 sikuona haja ya Kuendelea hadi Kilomita 42 tulizokuwa tunakimbia, hivyo naomba Radhi na asitafutwe Mchawi nitajitahidi katika Mashindano yajayo" amesema Mwanariadha aliyejivunja ( aliyeyakimbia ) Mashindano ya Kimataifa ya Riadha duniani Alphonse Felix Simbu.
Chanzo: Spoti Leo ya Radio One Usiku huu Saa 1 na Nusu hadi Saa 2 Kamili.
Kwanini GENTAMYCINE nimesema akamatwe na ahojiwe?
Kwanza kitendo cha kukata Tamaa na kuachia Njiani ( tena akienda pembeni kabisa Kujificha ) ni Kutudhalilisha Watanzania.
Pili Kauli yake kuwa amegundua hakufanya Mazoezi sahihi yanakinzana na Kauli yake aliyoitoa Juzi na Jana kuwa amejiandaa Kikamilifu na atatuletea Medali Watanzania matokeo anaenda kutuletea Medali ya Kuyatoroka Mashindano na kwenda Kujificha Porini kwa muda.
Tatu Binafsi kwa ninavyowajua Viongozi wa Michezo mbalimbali nchini Tanzania walivyo Wajanja na Matapeli ( Panjuani na Samjo ) huenda huyu Mwanariadha Alphonse Felix Simbu amepewa chake ( Pesa ) kisha akaambiwa ajichomeshe ( ajifelishe ) kwa Makusudi ili asiwe Kikwazo kwa Wanariadha wengi Wakubwa waliokuwa Wakimhofia kutokana na Uimara wake.
Msichokijua
Wanariadha wote walioshiriki Mashindano haya huko Jijini Budapest nchini Hungary walipewa Ratiba yote ya Mashindano kuanzia Eneo mpaka Umbali na huyu Mwanariadha aliomba Msaada kutoka Serikalini ili kuweka Kambi na Kujiandaa Kikamilifu huko huko Ulaya ambapo alipewa na hata Yeye Mwenyewe kushukuru ila Leo kwa Makusudi, Uhuni na Usanii anayaachia Mashindano katikati tena kwa Kutoroka na Kuzamia ( Kuingia ) Porini ( Msituni )
Na alivyo Mpuuzi ( asivyo na Akili ) ameshindwa hata Kudanganya kuwa alishikwa na Tumbo la Kuhara au Haja Kubwa ( Kuukweka ) kwa ghafla kutokana na Kufakamia hovyo Mivyakula ya Wazungu muda mchache kabla ya kuanza Mashindano Yeye kaona atudanganye kuwa hakuwa na Mazoezi ya Kutosha.
Asitufanye Watanzania Wote Fools.
Acha kupotosha wewe. Simbu awaze MacDonalds wakati hizo 5 star hotels ni sehemu ya maisha yake kwa sasa? Kuhusu umri ondoa shaka. Simbu ni miongoni mwa wanariadha au wanamichezo wachache sana kutoka Afrika wenye passport zenye umri wao halisi. Bado Simbu ana miaka mingi tu ya kukimbia Marathon kwa ubora wa hali ya juu. Hao kina Selassie na Kipchoge chukua miaka yao jumlisha 7 ndo utapata umri halisi.Alphonce Simbu hana mazoezi ya kutosha, hana mafunzo mazuri na pia hana maandalizi ya kutosha kushindana na vijana wadogo.
Kingine ni kwamba hana ari, nguvu na pia hana kasi ya kukimbia na wakati wenzie wakikimbia kwa kuhifandhi pumzi yeye awaza zile MC-Donalds alizoficha chumbani kwake hotelini.
Na si kukimbiza upepo bali ni kukimbia kwa kupanga muda (timing), mbinu na maarifa
Hivyo , kwa umri wake leo wa miaka 31 ni bora Tanzania itafute vijana wapya chipukizi wa kukimbia mbio ndefu.
Ni Haile GebrSellasie pekee ndie alieweza kukimbia mbio za marathon hadi akiwa na umri wa miaka 42 alipostaafu akiwa na umri wa miaka 42.
Tulikuwa na akina mzee Juma Ikangaa walikimbia uzuri tu kwa nidhamu.
Na alifunja rekodi yake mwenyewe ya marathon mwaka 2008 mjini Berlin ambayo bado hadi leo haijavunjwa na mwanariadha yoyote.
Hilo la McDonalds nimetumia tu kusisitizia "disappointment" yangu baada ya Simbu kuitia aibu nchi yetu huko Budapest.Acha kupotosha wewe. Simbu awaze MacDonalds wakati hizo 5 star hotels ni sehemu ya maisha yake kwa sasa? Kuhusu umri ondoa shaka. Simbu ni miongoni mwa wanariadha au wanamichezo wachache sana kutoka Afrika wenye passport zenye umri wao halisi. Bado Simbu ana miaka mingi tu ya kukimbia Marathon kwa ubora wa hali ya juu. Hao kina Selassie na Kipchoge chukua miaka yao jumlisha 7 ndo utapata umri halisi.
Pia elewa Marathon ni mbio kwa ajili ya wazoefu na wakongwe wanaokaribia kustaafu. Vijana chipukizi wanaishia 10k. Kabla ya kuingia kwenye marathon kina Filbert Bayi, Kipchoge, Gebre, Kenenisa na wakali wengine walikichafua sana kwenye 5000m na 10000m.
Wewe ndo unaleta siasa kwenye mambo usiyoyajua. Mimi nimekulia kwenye familia ya riadha kwahiyo nimeandika ninayoyajua kiundani bila kuhadithiwa wala kuona kwenye TV kama wewe. Unaposema Tanzania kwenye michezo ni 0 nakuona ni mtu usiyejua lolote kwenye michezo. Mwezi wa 4 mwanariadha Geay alikuwa wa pili kwenye Boston Marathon nayo ilikuwa 0? Kumbuka kwenye Boston Marathon bingwa wa dunia Kipchoge alikuwa wa 6. Siku nyingine bisha ukiwa na facts sio hizo hisia zako.Hilo la McDonalds nimetumia tu kusisitizia "disappointment" yangu baada ya Simbu kuitia aibu nchi yetu huko Budapest.
Usilete siasa na urongo.
Wanamichezo wa Afrika ni wachache sana wenye umri wao halisi, hizi detalis umezipatia wapi, na kutoka katika takwimu zipi? Hizi ndo sifa zenu kuongea siasa kwenye kila jambo hata yale mambo serious..
Tanzania kwenye michezo ni 0 hamna kitu miaka nenda rudi.
Pia acha urongo hawa wenzetu wengine si kama sisi kudanganya na kutafuta njia za mkato wao hujiandaa khasa na huwa na personal trainer na vifaa vya kisasa.
Wataka kusema Sellasie ambae sasa ana miaka 50 ujumlishe na 7 awe 57?
Kipchoge nae wasema ana 38 (umri wake halisi) ujumlishe na 7 kwahiyo sasa hivi ni 45?
Mkuu umemaliza Kila kitu, asipoelewa hatoelewa tena mpaka anakufaMkuu Genta kwenye riadha kuna ishu ya hali ya hewa na mwili kukataa. Akisema alazimishe madhara yanaweza kuwa makubwa na huenda hata kupoteza maisha. Mwaka 2004 mke wa mwanariadha mkubwa wa Ethiopia ndugu Kenenisa Bekele alifariki mida ya asubuhi baada ya kufanya mazoezi ya kukimbia umbali mrefu akifuata pace ya Kenenisa. Hata Kenenisa mwenyewe alishawahi kuishia njiani kwenye mashindano ya mbio za nyika zilizofanyikia Mombasa Kenya. Ikumbukwe Kenenisa kabla ya mbio za Mombasa alikuwa mshindi wa mbio za nyika kwa miaka mitano mfululizo. Usain Bolt nae alishawahi kufanya kama Simbu.
Pia kwa mwanariadha mkubwa kama Simbu bora alivyofanya kwasababu haiwezi haribu sana hadhi yake kwenye ulimwengu wa marathon kama angekuja na muda mbaya huku akiwa nafasi za nje ya top ten. Ingemshushia thamani na kujikuta anakosa madili mengi. Wanariadha wa hadhi ya Simbu huwa wanakuwa na mikataba minono na makampuni kama Nike, Adidas, Puma, Hublot, Seiko na mengine mengi yanayojihusisha na michezo.
Na kama wewe popoma ulikuwa hujui ni kuwa huyo dogo kaanzia mbali sana harakati zake. Tangu 2006 alijiunga na shule ya michezo na kujaribu sana kupenya ila ikachukua miaka mingi kufanikiwa kupenya na kuwa Staa mkubwa duniani. Binafsi nilishashuhudia mtu fulani akimwambia dogo kuwa hana kipaji cha riadha kwa hiyo bora apambane na shule tu. Simbu darasani pia alikuwa njema.
Ninashauri serikali ikukamate wewe popoma na kukuweka ndani kwa masaa 48.
Kumbe Bekele umo huku JF?Mkuu umemaliza Kila kitu, asipoelewa hatoelewa tena mpaka anakufa
Hahah!!Kumbe Bekele umo huku JF?
bondia yupi, yule dogo anayepaka poda na kufuga nywele?nakumbuka tuhuma kama hizi zikienda kwa bondia kutoka tanga bw mwakinyo,lakini baada ya makelele kuwa mengi ilibidi kijana apasuke kwa codes,kwamba “sitakula sifa mimi😂😂”.
nilimuelewa sana.
watu wanakuja na kibunda mezani unafikiria carrier yako na hatima yake kisha familia yako,unaamua kujilipa pension haraka.
Hata mimi ni shabiki lialia wa Bekele. Kwenye cross country alivuruga mno. Kipchoge sijawahi kumkubali.Hahah!!
Nilikuwa napenda battle ya Kipchoge na Bekele kwenye field and track
Kushiriki hayo mashindano unatakiwa ushiriki mashindano yanayotambulika na shirikisho la riadha duniani na kufikia viwango vyao. Hapa Tanzania mashindano yanayotambulika ni Kili Marathon. Hizi marathon zingine kama ile ya Tulia Marathon ni kama kufanya tu mazoezi na kujipatia chochote kitu ila kwenye CV haiongezi kitu kwasababu hayatambuliki kimataifa. Muhimu ni kuhakikisha wanamichezo wengi wanashiriki mashindano mengi yanayotambulika na shirikisho.Juz nimeona had mchezo wa kurusha TUFE na mkuki Tanzania hakuna mwakilishi?
Kipchoge lakini ni mwamba mwingine kwenye marathonHata mimi ni shabiki lialia wa Bekele. Kwenye cross country alivuruga mno. Kipchoge sijawahi kumkubali.
Ni kweli ndugu ila bahati mbaya sina mzuka naye kabisa. Kiukweli katika wanariadha wa Kenya nilikuwa namkubali Paul Tergat tu.Kipchoge lakini ni mwamba mwingine kwenye marathon
Kwanini MzeeNi kweli ndugu ila bahati mbaya sina mzuka naye kabisa. Kiukweli katika wanariadha wa Kenya nilikuwa namkubali Paul Tergat tu.