Serikali imuondoe Paul Makonda haraka kabla mambo hayajaharibika. Tamko lijalo linaweza kuathiri nchi pakubwa

Serikali imuondoe Paul Makonda haraka kabla mambo hayajaharibika. Tamko lijalo linaweza kuathiri nchi pakubwa

Wanaoshabikia upuuzi huo, wapuuzi pia sawa na mwanamke anayesimama kwa mashoga zake kumsema mumewe kwamba anakojoa kitandani bila kujua ni aibu yake mwenyewe. Na madhara ya kuachwa atayapata wewe.
 
Mi sioni kwanini aondolewe...hata wakitususa tuna utajiri wa kutosha ndiyo maana wao wanajipendekeza kwetu hata kama tuna madeni kibao hatujalipa bado wanatukopesha...Mwache Makonda afaidi zama zake hizi mpaka mwisho
 
Tatizo ni pale unapouliza Magufuli anakwama wapi kwa huyu Makonda, wakati Magufuli hajawahi kuwa na consistent and coherent agenda popote.

Hapa atakwambia anapiga vita rushwa, kule kauza nyumba za serikali nje ya utaratibu mpaka kwa hawara zake. Pia anasema trafiki kupewa rushwa ni "hela ya kupiga viatu brashi tu".

Hapa atakwambia yeye ni rais wa wanyonge, na maendeleo hayana vyama, pale atakwambia atapiga wapinzani mpaka shangazi zao.

Hapa atamfukuza kazi Kangi Lugola kwa kupiga dili ambalo halijapitia bungeni, kule atanunua ndege bila idhini ya bunge, tender ya wazi wala kuruhusu ukaguzi wa CAG ATCL.

Hapa atasema anawakilisha maslahi ya wakulima wanyonge, halafu hapo hapo ataingilia manunuzi ya korosho na kuharibu soko kwa namna ambayo inaangusha mapato ya mazao ya kilimo kwa asilimia 55 katika mwaka mmoja tu unaoishia Agosti 2019, kwa mujibu wa ripoti ya Bank of Tanzania ya Oktoba 2019.

Sasa mtu kama huyu utategemea vipi ajielewe zaidi ya wholesale politics?

Na watu waliokuwa sane serikalini waliotaka kummdhibiti Makonda na kufanya "damage control" kama kina Dr. Mahiga ndiyo wanaondokewa kwenye prominence. Go figure.

Wizara ya Mambo ya Nje sasa hivi tungehitaji sana watu wenye busara na uzoefu wa kimataifa. Lakini wameondolewa, wamewekwa die hard ideologues waimba sifa. Clear mesage kwamba hatutaki watu wa busara, tunataka watu wa kujikomba kwa mkuu.

For all I know yeye Magufuli na Makonda hawajapishana sana katika kufikiri, na sasa wanaandaa vita dhidi ya "mabeberu".

Sent using Jamii Forums mobile app

Akili ya huyu mzee ilianza kunichosha alipoanza kusema kuna watu wameficha pesa ndani ndo maana mzunguko amna mara naingia kwenye madaraka sukali 5000 sasa hivi 2500 mtu wa namna hiyo unaweza kumwelewaje mara matajiri wataishi kama mashetani mara nataka nitengeneze mabilione


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali yetu inaogopa kuabika wazungu sio mazeruzeru jamaa wanatujua kuliko tunavyojijua sisi.
Sikitiko langu kubwa ni tuhuma aliooredheshewa ya kudhulumu uhai wa watu kadhaa (kukatisha uhai wa watu kabla ya wakati wao). Hili ni jambo ambalo serikali inapaswa ilitolee maelezo ni kwa namna gani vyombo vya usalama vya nje vifahamu pasipo na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kufahamu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Marekani imesema: Makonda ni mkandamizaji wa haki za kibinaadamu ikiwemo haki ya kuishi (kwa tafsiri isiyo rasmi ni kuwa anahusika na mauaji ya raia); haki ya kidemokrasia na nyinginezo. Anapaswa kuwekwa kando haraka!

Marekani imetega mtego usio na magego. Mtego mkali. Mtego wao unaanzia kwenye swali la kiudadisi: Makonda amefikiaje kukandamiza haki za kibinaadamu hadi kupigwa marufuku ya kuingia Marekani akiwa amezungukwa na wakuu wake(ukiwemo Mwenyekiti wangu) waliopaswa kumdhibiti?

Marekani imeamua kukusaidia kujitenga na Makonda. Marekani imekutega Rais na Mwenyekiti wangu Dr. John Pombe Magufuli. Imekusaidia na kukupa nafasi adhimu. Jitenge na Makonda kabla ya mambo mrama kwenda!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Kuna mtu anaandaliwa taiming mda mwalimu mzuri


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akili ya huyu mzee ilianza kunichosha alipoanza kusema kuna watu wameficha pesa ndani ndo maana mzunguko amna mara naingia kwenye madaraka sukali 5000 sasa hivi 2500 mtu wa namna hiyo unaweza kumwelewaje mara matajiri wataishi kama mashetani mara nataka nitengeneze mabilione


Sent using Jamii Forums mobile app
Yeye mwenyewe hajui anaenda au anarudi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sikitiko langu kubwa ni tuhuma aliooredheshewa ya kudhulumu uhai wa watu kadhaa (kukatisha uhai wa watu kabla ya wakati wao). Hili ni jambo ambalo serikali inapaswa ilitolee maelezo ni kwa namna gani vyombo vya usalama vya nje vifahamu pasipo na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kufahamu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata vya hapo vinafahamu lakini vinamuogopa sana Daud Bashite visingeweza kusema ukweli
 
Sidhani kama utakuwa uamuzi wa busara kwa mwenyekiti kujitenga na Makonda kwa sasa,Kujitenga na Makonda ni kukubaliana na mawazo ya wamarekani, Kuna vitu lazima ujifunze kuviangalia kwa macho ya tatu, Mwalimu wangu wa Physics alikuwa anasema jaribu kuwa nje ya mada na uwe mwangaliaji kwa mbali ndio utaona uhalisia,

Nakukumbusha,

Mwana Mfalme wa Saud alipoamua kwa makusudi na maslahi yake na kwa uwazi kabisa kumuua Mwandishi wa Habari aliyekuwa anaandikia CNN Jamal Khashogi, Turkey alikuwa kiranja kuionyesha US Kuwa Mwanamfalme ni mkosaji, na ushaidi upo, lakini US Iliziba masikio,umeshajiuliza kwanini?

Maslahi, Trump alimtetea mwanamfalme waziwazi, na pia Pompeo alitumwa Turkey na baadaye SAUDIA Kuhakikisha kwamba mambo yanakaa sawa, hatimaye ERDOGAN alisalimu amri! Unajua sababu?

Nini nafasi ya maslahi ya US na magharibi katika serikali ya awamu ya 5. Toka Rais ameapishwa hajakanyaga US wala EU na kwingineko, Je maslahi ya US na washirika wake yaliyoimarishwa awamu ya 4 yanarindwaje? Ikiwa Kiongozi aliyeko madarakani hana muda nao!!!

Je nani ni wamiliki wa makampuni ya ACACIA na BARICK? Nini hatima ya maslahi ya Mataifa ya nje?
Embu jiulize unamfungia mtu ambaye hana umuhimu wa kuja nchini kwako si ujinga huo.

Suala la Makonda halihitaji Muhemuko, wala Siasa za Kipumbavu, Sababu zilizoongelewa ni za Kishabiki zaidi.

Vipi kuhusu mauaji wanayomtuhumu nayo je vipi kuhusu kuna watu kenya wamezuiliwa kwenda nao USA [emoji631] je na hao wakenya wamegusa maslai ya USA [emoji631]


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ubaya zaidi wanasema wana ushahidi. Hawa wamarekani huu uchunguzi walioufanya lini? Inawezekana CIA ina operate Bongo kimya kimya, inakusanya data na kuzirusha kwao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Platforms zote zao kwa nn? Wasijue satellites zao, simu zao, Android, window, Symbian, iPhone, IOS, ATM card, Facebook Google, Instagram, YouTube, Wikipedia, Twitter
Kwa nn wasijue

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sio kuomuondoa tu, aseme mwenyewe mahala alipoficha mwili wa Ben Saanane na wa Azory ili familia zao ziwazike kwa utaratibu unaofaa.
Hivi inawezekana!!!!! Hivi ni kweli???? Napata shida hivi uenda kuna jambo anajua!!!! Msitunge mambo mkampa mwezenu matatizo.
 
Hawana haja ya kuja huku. Hiyo kazi wanampa dogo wa fildi anachokonoa kwenye kilaptop chake ndani ya dakika 3 taarifa zote wanazo.
Unaweza kuta wanazo picha za satellite na video za satellite za matukio yote yasiyoeleweka. Mpaka coordinates zao ili wakitaka wanaweza kufanya alichofanyiwa jenerali wa iran.


Mawazo:Serikali ikitaka isifatiliwe kwa njia ya sattelite. Wahakikishe wanaezeka barabara zote Tanzania kwa mabati manene kwa juu ili magari yapite chini ya paa la mabati.
Satellites za USA na Galileo za ulaya zinaona kilometers 3 kwenda china ya aridhi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu wana JF, kila mmoja amesoma tamko la hasira la Marekani juu ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ndugu Paul Makonda.

Chonde Chonde washauri wa Rais Magufuli, tunawapenda sana na tunaipenda serikali yetu, Makonda Mmoja asiingize nchi kwenye mgogoro wa Kidiplomasia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hutupangiwi na mabeberu!.
P
 
Back
Top Bottom