Serikali ina mpango gani na mbuyu ulioanguka kata ya Kimanga?

Serikali ina mpango gani na mbuyu ulioanguka kata ya Kimanga?

Torch

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2013
Posts
1,200
Reaction score
1,121
Wanabodi kwa hapa Tabata Kimanga njia ya kwenda machimbo ukitokea Chang'ombe, kituo cha Mbuyuni


Mbuyu ulioanguka hapa una siku nne. Serikali ipo wapi? Njia mbadala ni ipi?

Hiyo ni njia yetu ya kila siku
 
BaraBara imefungwA Tufanyaje raia!?
 
Wanabodi kwa hapa Tabata Kimanga njia ya kwenda machimbo ukitokea Chang'ombe, kituo cha Mbuyuni


Mbuyu ulioanguka hapa una siku nne. Serikali ipo wapi? Njia mbadala ni ipi?

Hiyo ni njia yetu ya kila siku
Ngoja kwanza tumuite David Livingstone atueleze nani alimuonesha njia ya kwenda Ujiji kutoka Bagamoyo.
 
Ukiona hivyo hakuna mtu mwenye wadhifa au connection na mwenye wadhifa anaishi maeneo hayo. Nchi hii wanufaika wakubwa ni wale walio juu ama wanaojuana na walio juu.

Kungekuwa kuna mchepuko tu wa Katibu wa wizara unaishi huko sasa hivi mngeshasahau hata kama kulikuwa na mti umeanguka.

Kama ni kadhia sana huo mti jikusanyeni wananchi wenyewe mtafute suluhisho, mkitegemea serikali mtasubiri sana.
 
Bureaucracy inatutesa sana nchi hii
Nakumbuka nikiwa mdogo, palikuwa na siku ya maendeleo Mara moja kwa wiki. Yaani siku Hiyo watu wanaenda kumfanya kazi ya usafi au kusogeza tofari za shule/zahanati, kuzibua mitaro n.k Asiye na muda anaweka pesa inayotosha kumlipa kibarua afanye kazi badala yake.
Leo tunasubiri mwenyekiti amwambie mtendaji, mtendaji aombe excavator ya halmashauri kupitia kwa technician wa Wilaya, technician amwambie DED.....
 
Nakumbuka nikiwa mdogo, palikuwa na siku ya maendeleo Mara moja kwa wiki. Yaani siku Hiyo watu wanaenda kumfanya kazi ya usafi au kusogeza tofari za shule/zahanati, kuzibua mitaro n.k Asiye na muda anaweka pesa inayotosha kumlipa kibarua afanye kazi badala yake.
Leo tunasubiri mwenyekiti amwambie mtendaji, mtendaji aombe excavator ya halmashauri kupitia kwa technician wa Wilaya, technician amwambie DED.....
Siasa zimeharibu mengi sana
 
Wanabodi kwa hapa Tabata Kimanga njia ya kwenda machimbo ukitokea Chang'ombe, kituo cha Mbuyuni


Mbuyu ulioanguka hapa una siku nne. Serikali ipo wapi? Njia mbadala ni ipi?

Hiyo ni njia yetu ya kila siku
Nchi hii undezi mwingi mjumbe, mwenyekiti mtaa, diwani hawawajibiki kwa yeyote na hawana kiranja, wananchi nao hawajui nguvu na mamlaka yap, Wqchungaji na mashekh hawajumuiki kuhamasisha na hawana wigo wa kufanya hivo.
 
Wanabodi kwa hapa Tabata Kimanga njia ya kwenda machimbo ukitokea Chang'ombe, kituo cha Mbuyuni


Mbuyu ulioanguka hapa una siku nne. Serikali ipo wapi? Njia mbadala ni ipi?

Hiyo ni njia yetu ya kila siku
Watu wa Dar mnashida sehemu, mnapenda sana kuendekeza umwinyi na ubwanyenye mbuyu kuanguka hamuwezi ata kuorganise kama wana jamii na kusaidiana kuuondoa adi serikali ije, huu upumbavu utaisha lini kila kitu kutegemea serikali, itafikia hatua mtaita serikali ije iwasaidie kuwachakata wake zenu.
 
Ukiona hivyo hakuna mtu mwenye wadhifa au connection na mwenye wadhifa anaishi maeneo hayo. Nchi hii wanufaika wakubwa ni wale walio juu ama wanaojuana na walio juu.

Kungekuwa kuna mchepuko tu wa Katibu wa wizara unaishi huko sasa hivi mngeshasahau hata kama kulikuwa na mti umeanguka.

Kama ni kadhia sana huo mti jikusanyeni wananchi wenyewe mtafute suluhisho, mkitegemea serikali mtasubiri sana.
Uvuteni mje muutupe apa Mandela road
 
Kila kitu ni serikali, hamjui mkijikusanya, mkaita watu wenye chainsaw, mkajichanga, huo mti inakuwa vipande vya kuwashia Moto???
Serikali ni sisi wenyewe, ndiyo maana hata raisi tunamlipa sisi wenyewe kwa nguvu zetu!
Tuchangamke muda mwingine, unasubiria TANROADS, TARURA sijui TEMESA, haya
 
Kila kitu ni serikali, hamjui mkijikusanya, mkaita watu wenye chainsaw, mkajichanga, huo mti inakuwa vipande vya kuwashia Moto???
Serikali ni sisi wenyewe, ndiyo maana hata raisi tunamlipa sisi wenyewe kwa nguvu zetu!
Tuchangamke muda mwingine, unasubiria TANROADS, TARURA sijui TEMESA, haya
Serikali ndio yenye wajibu wa kuhakikisha barabara ni salama na zinapitika.
 
Wewe ushaambiwa mti wenyewe "MBUYU "
hapo kuna wazee wamekaa.
Sio kila mti mnaweza kuukata kata tu.
Waje serikali wanaosema hawarogeki kuutoa.kama haujitaki nenda kaukate kate
Kila kitu ni serikali, hamjui mkijikusanya, mkaita watu wenye chainsaw, mkajichanga, huo mti inakuwa vipande vya kuwashia Moto???
Serikali ni sisi wenyewe, ndiyo maana hata raisi tunamlipa sisi wenyewe kwa nguvu zetu!
Tuchangamke muda mwingine, unasubiria TANROADS, TARURA sijui TEMESA, haya
 
Back
Top Bottom