Serikali ina mpango gani na mbuyu ulioanguka kata ya Kimanga?

Serikali ina mpango gani na mbuyu ulioanguka kata ya Kimanga?

Wanabodi kwa hapa Tabata Kimanga njia ya kwenda machimbo ukitokea Chang'ombe, kituo cha Mbuyuni


Mbuyu ulioanguka hapa una siku nne. Serikali ipo wapi? Njia mbadala ni ipi?

Hiyo ni njia yetu ya kila siku
Picha ingewafanya waje haraka kuutoa
 
hamjui mkijikusanya, mkaita watu wenye chainsaw, mkajichanga, huo mti inakuwa vipande vya kuwashia Moto???
Mibuyu ina mengi yaliyofichika, hato hao serikali huenda waliko bado wanatupiana mpira nani aende ...usishangae kuna mtu amepangiwa hiyo kazi ila hayuko tayari kuwa chambo
 
Nakumbuka nikiwa mdogo, palikuwa na siku ya maendeleo Mara moja kwa wiki. Yaani siku Hiyo watu wanaenda kumfanya kazi ya usafi au kusogeza tofari za shule/zahanati, kuzibua mitaro n.k Asiye na muda anaweka pesa inayotosha kumlipa kibarua afanye kazi badala yake.
Leo tunasubiri mwenyekiti amwambie mtendaji, mtendaji aombe excavator ya halmashauri kupitia kwa technician wa Wilaya, technician amwambie DED.....
Zama zinabadilika mkuu kwa hali hii ya maisha ya sasa unaweza kuilinganisha na zama ambazo ulikua mdogo mkuu?fikiri kwa kina
 
Back
Top Bottom