Serikali inafanya makosa kutomfunga jela Zitto Kabwe kwa makosa ya uchochezi anayofanya. Afungwe kwa mujibu wa sheria ili iwe fundisho

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Mtu anapotosha umma kuwa zaidi ya wananchi mia moja wameuwawa na jeshi la polisi. Ushahidi upo wazi na anatiwa hatiani alafu sababu ni mwanasiasa anapewa adhabu ya Conditional discharge. Huu ni upendeleo.

Anatamka hadharani kuwa mkuu wa nchi aliyefariki alituma watu wachome nyumba yake.Na anakiri waliochoma wamemuomba radhi, kwa nini asiwapeleke polisi? Maana kuchoma moto nyumba ni jinai na haina mwisho .

Anachafua hadharani kuwa taasisi ya rais inatumia maofisa wa serikali kufanya uharifu alafu anaachwa tu. Kwa nini amchafuae kiongozi aliyetangulia mbele za haki? Alafu anaangaliwa tu?
 
Pitia orodha ya watu ambao Zitto anadai wamepotezwa.

 
Bora umesema asee, mtu mzima unaamka kabla hata ya kunywa chai unaanza kumsema mwanaume ZZK . Chuki, wivu, husda na dhiki ndio vinawasumbua watu wa namna hii.
 
Mtu anapotosha umma kuwa zaidi ya wananchi mia moja wameuwawa na jeshi la polisi. Ushahidi upo wazi na anatiwa hatiani alafu sababu ni mwanasiasa anapewa adhabu ya Conditional discharge. Huu ni upendeleo...
Anaachwa kwasababu; "ni bora nusu shari kuliko shari kamili".
 
Mtu anapotosha umma kuwa zaidi ya wananchi mia moja wameuwawa na jeshi la polisi. Ushahidi upo wazi na anatiwa hatiani alafu sababu ni mwanasiasa anapewa adhabu ya Conditional discharge...
Kiongozi aliyetangulia yaani Magufuli, hachafuliwi kwa kuwa alikwishachafuka kabla.

Yanayoongelewa kuhusu yeye na Zitto Kabwe ni kama kusoma ukurasa mmoja wa kitabu, lakini bado kuna page 500 za uozo na maovu ya DIKTETA huyo.

Kadri unavyoandika nyuzi nyingi za kumtetea Magufuli wewe Nyankurungu2020 ndiyo unavyoonyesha USUKULE wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…