Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 1,096
- 4,948
Kuna jambo nimelifanyia utafiti nimegundua makampuni na mashirika ya umma yanaiba fedha nyingi sana serikalini. Kuna fundi nilimtuma akalipe huduma ya kuunganisha maji. Nakumbuka jumla ya fedha zilizoletwa kama bill kwenda serikalini ilikuwa zaidi ya laki saba na sabini na nane.
Nilimpa moja wa mafundi wangu wakalipie kile kiasi na baadaye nikaletewa karatasi kama uthibitisho wa malipo. Mtu mmoja akaniambia hapo mkuu umepigwa kama laki nne hivi, nikamwambia mbona nimepewa risiti ya malipo? Akaniambia nichukue control number iliyoandikwa kwenye karatasi niingie kwenye mfumo wa malipo ya serikali nione hiyo namba imelipia nini na kiasi gani.
Nilichogundua ni kwamba; ile control numba siyo ya shirika la maji. Imelipia huduma nyingine kabisa, nikafanya ufuatiliaji bila kusema , nilipokwenda kwenye mamlaka husika nikakuta malipo yaliyofanyika ni 254300 tu na control number ya malipo haya siyo ile niliyopewa.
Nilijaribu kufuatilia ila nikagundua wale mabwana wenye ofisi ya maji wanaelewa ule mchezo na ndiyo maana wameweka utaratibu wa watumishi wengi wasio na ajira rasmi ili unapowashtukia wakiambiwa huyo aliyefanya hivyo siyo mwajiriwa wetu ni mtoto mwenye njaa anajitolea. Lakini najiuliza hizi risiti zinazotolewa kinyume cha huduma siyo uhujumu uchumii?
Baada ya kutokea ule mchezo nimekuwa nafanya utafiti kwa huduma nyingi za serikali; napenda kusema kwamba tatizo lipo kwenye malipo ya leseni za udereva, leseni za biashara, kodi mbalimbali, TANESCO kuunganisha umeme, huduma za afya nk
Jambo lililofanywa na viongozi wa utumishi wa umma ili wapate fedha wameondoa ujumbe mfupi wa malipo kwenda kwa mteja. Mifumo hii ya malipo ilikuwa imeunganishwa na namba za simu za mteja na lazima hiyo namba iwe imesajiliwa kwa kitambulisho cha NIDA.
Viongozi na watumishi wameweka huduma nyingi zisizotoa uthibitisho wa malipo wa mteja anayetaka huduma badala yake wameruhusu hata namba za vishoka ziweze kupewa huduma.
Mimi kwa mfano naitwa Shebe Lule Kitwingila na nina namba ya simu iliyosajiliwa kwa jina langu, kwanini mifumo ikubali kuandikwa namba za vishoka kwenye malipo ya awali? Kwanini bili za maji na TANESCO au kodi ya ardhi zinakwenda kwa namba ya mteja ila malipo ya awali bili zitengenezwe kwa namba nyingine?
Juzi kati hapa mlisikia mfanyabiashara aliyekuwa analalamika kwa mkuu wa mkoa; aliomba mifumo iboreshwe lakini sidhani kama watarekebisha kwa sababu wanufaika ni hao hao.
Wizi wa kutumia wrong control number ni mkubwa sana nchini na endapo kila mkuu wa taasisi ataamua kufanya ufuatiliaji watagundua kuna uhalifu mkubwa sana unaendelea.
Mwisho, nitoe wito wa kila mwenye malipo ya serikali au shirika waingie kwenye mfumo wa malipo ya serikali wafanye verification kama malipo yaliyofanywa kwa namba za malipo alizopewa ni sahihi?
Viwanja vingi vya serikali sasa hivi vinauzwa kwa wrong control number na upo uwezekano huko mbeleni tuendako tukaenda ardhi tukakuta fedha zilizopo kwenye risiti siyo zilizopo ardhi.
Watanzania amkeni acheni kuwapa watu wakawafanyie malipo kwenye nyaraka serious kama kununua ardhi, kuunganisha maji, TANESCO, leseni nk.....atakuja Rais mwingine hapa tutaanza kukamatwa kwa uhujumu uchumi....na utakosa haki kwani walipkuhudumia watakuwa wamestaafu.
Mwisho, taasisi zote ambazo wanatoa huduma ya malipo na hakuna feedback kwamba umelipia huduma ni wezi
Nilimpa moja wa mafundi wangu wakalipie kile kiasi na baadaye nikaletewa karatasi kama uthibitisho wa malipo. Mtu mmoja akaniambia hapo mkuu umepigwa kama laki nne hivi, nikamwambia mbona nimepewa risiti ya malipo? Akaniambia nichukue control number iliyoandikwa kwenye karatasi niingie kwenye mfumo wa malipo ya serikali nione hiyo namba imelipia nini na kiasi gani.
Nilichogundua ni kwamba; ile control numba siyo ya shirika la maji. Imelipia huduma nyingine kabisa, nikafanya ufuatiliaji bila kusema , nilipokwenda kwenye mamlaka husika nikakuta malipo yaliyofanyika ni 254300 tu na control number ya malipo haya siyo ile niliyopewa.
Nilijaribu kufuatilia ila nikagundua wale mabwana wenye ofisi ya maji wanaelewa ule mchezo na ndiyo maana wameweka utaratibu wa watumishi wengi wasio na ajira rasmi ili unapowashtukia wakiambiwa huyo aliyefanya hivyo siyo mwajiriwa wetu ni mtoto mwenye njaa anajitolea. Lakini najiuliza hizi risiti zinazotolewa kinyume cha huduma siyo uhujumu uchumii?
Baada ya kutokea ule mchezo nimekuwa nafanya utafiti kwa huduma nyingi za serikali; napenda kusema kwamba tatizo lipo kwenye malipo ya leseni za udereva, leseni za biashara, kodi mbalimbali, TANESCO kuunganisha umeme, huduma za afya nk
Jambo lililofanywa na viongozi wa utumishi wa umma ili wapate fedha wameondoa ujumbe mfupi wa malipo kwenda kwa mteja. Mifumo hii ya malipo ilikuwa imeunganishwa na namba za simu za mteja na lazima hiyo namba iwe imesajiliwa kwa kitambulisho cha NIDA.
Viongozi na watumishi wameweka huduma nyingi zisizotoa uthibitisho wa malipo wa mteja anayetaka huduma badala yake wameruhusu hata namba za vishoka ziweze kupewa huduma.
Mimi kwa mfano naitwa Shebe Lule Kitwingila na nina namba ya simu iliyosajiliwa kwa jina langu, kwanini mifumo ikubali kuandikwa namba za vishoka kwenye malipo ya awali? Kwanini bili za maji na TANESCO au kodi ya ardhi zinakwenda kwa namba ya mteja ila malipo ya awali bili zitengenezwe kwa namba nyingine?
Juzi kati hapa mlisikia mfanyabiashara aliyekuwa analalamika kwa mkuu wa mkoa; aliomba mifumo iboreshwe lakini sidhani kama watarekebisha kwa sababu wanufaika ni hao hao.
Wizi wa kutumia wrong control number ni mkubwa sana nchini na endapo kila mkuu wa taasisi ataamua kufanya ufuatiliaji watagundua kuna uhalifu mkubwa sana unaendelea.
Mwisho, nitoe wito wa kila mwenye malipo ya serikali au shirika waingie kwenye mfumo wa malipo ya serikali wafanye verification kama malipo yaliyofanywa kwa namba za malipo alizopewa ni sahihi?
Viwanja vingi vya serikali sasa hivi vinauzwa kwa wrong control number na upo uwezekano huko mbeleni tuendako tukaenda ardhi tukakuta fedha zilizopo kwenye risiti siyo zilizopo ardhi.
Watanzania amkeni acheni kuwapa watu wakawafanyie malipo kwenye nyaraka serious kama kununua ardhi, kuunganisha maji, TANESCO, leseni nk.....atakuja Rais mwingine hapa tutaanza kukamatwa kwa uhujumu uchumi....na utakosa haki kwani walipkuhudumia watakuwa wamestaafu.
Mwisho, taasisi zote ambazo wanatoa huduma ya malipo na hakuna feedback kwamba umelipia huduma ni wezi