Serikali inapokosolewa kwa Constructive Criticism, je, Ifuate Ushauri? Hongera Bunge letu tukufu kufuata ushauri na kutuondolea ubatili huu

Serikali inapokosolewa kwa Constructive Criticism, je, Ifuate Ushauri? Hongera Bunge letu tukufu kufuata ushauri na kutuondolea ubatili huu

Kulikuwa na ulazima wa kuandika majina ya Katibu wa bunge na Katibu mkuu wa CCM kwenye hiyo barua?
Mimi binafsi sioni kwamba kulikuwa na haja ya kuandika majina ya katibu wa chama.

Hapo Wanataka kuendelea kutuhadaa kwa kutuaminisha haya;

1. Kwamba hawakuwa wamekosea toka mwanzo hivyo tuone kuwa hakukuwa na tatizo kubwa kivile,

2. Kwamba bado mihimili yote ikiwemo bunge ionekane haiwezi kuwa na sauti, nguvu au maana kwa wananchi bila uwepo wa ccm.

3. Kwamba bado tupo katika Zama za chama kushika hatamu/dola.
 
No, not necesarily, japo ni kweli JYN hakuwa Spika bora, alikuwa ni bora Spika, japo Dr. Tulia ulikuwa Naibu Spika wa Bora Spika, so she is expected to be another bora Spika, but she has a chance of being Spika Bora.
Hili nimelisema hapa.
Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!.
P
Uandishi wa habari ni kazi kama kazi nyingine zote, waandishi wanaomba kazi na wanaajiriwa na kulipwa mishahara kama wafanyakazi wengine wowote. Waandishi walioajiriwa wanaitwa Press Journalists or media Journalists.

Waandishi ambao hawajaajiriwa wanaitwa Freelance Journalists.
Kwenye kundi la Freelance Journalists, kuna makundi matatu
1. Media Freelance Journalists, ni waandishi wa kujitegemea lakini wanaandikia media fulani as correspondents, hawa wanalipwa na hizo media.
2. Independent media Freelances - hili ni kundi la waandishi wa kujitegemea ambao hawako chini ya chombo chochote cha habari, hawa wanapeleka habari zao chombo chochote cha habari na hicho chombo kinawalipa.
3. Independent Media Freelance Volunteers, hili ni kundi la waandishi wa kujitegemea kwa kujitolea, hawa hawalipwi na media yoyote. Hawa wana shughuli zao nyingine za kuendesha maisha yao, lakini wanafanya uandishi wa habari kwa mapenzi tuu, just for the love of it. Hawalipwi, wanaandika habari bure kwa kujitolea, wanazisambaza bure kwenye media. Mimi ndio niko kwenye kundi hili. Naandika bure, nasambaza habari zangu kwenye
1. Vituo 8 vya TV, Vituo 10 vya Radio, Magazeti 10, na mitandao ya jamii lukuki ikiwemo jf. Nafanya bure, silipwi na media yoyote, ni mapenzi tuu.
P
 
All in all, Ndugai amejiuzulu kwa aibu na fedheha kubwa! Na daima nitamkumbuka kama Kiongozi mwoga, na asiye jiamini.

Kiongozi gani unashindwa kusimamia kile unacho kiamini! Au ndiyo yale yale ya kuongea tu kwa kuropoka, halafu unakuja kujutia kauli yako baadaye?
20220130_142053.jpg
 
Wanabodi,
Hii ni Nipashe ya Leo, 30.01.2022
View attachment 2100761
Kama kawaida yangu, kila nipatapo fursa huteremka na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" leo ni swali na pongezi. "Serikali inapokosolewa kwa constructive criticism, kama ushauri uliotolewa ni ushauri nzuri wenye maslahi kwa taifa, jee serikali ifuate ushauri huo, au iupuuzie kwa kushupaza shingo?. Hongera sana Bunge letu Tukufu kwa kufuata ushauri na kutuondolea ubatili katika Barua ya kujiuzulu Spika JYN!.

Kikawaida ni a being, ila sio human, hivyo serikali haiwezi kukosea jambo lolote, lakini serikali inaendeshwa na watu na inaongozwa na watu, human beings, watu hao wanaoongoza serikali ni binadamu na sio malaika, hivyo wanaweza kukosea, watu hao wanapokosea, inahesabika kuwa ni serikali ndio imekosea, hivyo serikali inapokosea au kwa kukosea yenyewe au kwa kukoseshwa, lazima ikubali kuwajibika kwa makosa hayo. Japo nimesema serikali kama serikali haiwezi kukosea, ila watendaji ndio wanaokosea na kuikosesha serikali.

Kila serikali inapofanya makosa, sometimes huwa kunatokea watu wenye jicho tunduizi, ambao wanaona makosa hayo na kuikosoa serikali kwa kutumia ukosoaji wa ujengaji (constructive criticism) ambao hufanyika kwa kuonyesha kosa lililofanyika na wakati huo huo kutoa mapendekezo ya jinsi ya kurekebisha makosa na kushauri a way forward kurekebisha makosa yaliyofanyika yasijirudie na maisha yaendelee. Naishauri serikali yetu tukufu, pale inapokosolewa kwa makosa ya wazi, kwanza isikasirike, pili ifuate ushauri na kurekebisha makosa na kujitahidi makosa kama hayo yasijirudie. Kitendo cha serikali kukubali kosa, not expressly but impliedly kwa kurekebisha kosa bila kukiri kosa, kwa kupokea ushauri, sio udhaifu ni uimara, na kuonyesha serikali yetu ni serikali sikivu.

Moja ya makala yangu ya nyuma, nilishauri, viongozi wa kisiasa na wa serikali, wanapofanya makosa ya wazi na kuifanya serikali ionekane imekosea, wanapaswa kwanza kukubali makosa, kuomba msamaha na kuwajibika. Hiki ndicho kilichofanyika kwa Spika aliyejiuzulu, Mhe. Job Ndugai, Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere? kwanza alikubali makosa, kisha akaomba msamaha, japo msamaha wenyewe ulikuwa ni msamaha batili Ndoa halali, ndoa batili na ndoa batilifu. Je, wajua pia kuna msamaha halali wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu? Msamaha ule ni batilifu!
akidhani atasamehewa, na baada ya kuomba msamaha huo batili, sisi waona mbali tukashauri, Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away? na baada ya shinikizo, ndipo JYN akakubali kujiuzulu ila huku nako alikurupuka na kuandika barua batili, hatukukaa kimya, Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away?

Taarifa ya kujiuzulu uspika ya Spika Mhe. Job Ndugai kwa vyombo vya habari, iliyosambazwa na ofisi ya Bunge, ni hii
View attachment 2100870
Taarifa hii ya Ofisi ya Bunge kwa vyombo vya habari, illionyesha Spika Ndugai ameandika barua ya kujiuzulu na kuilekeza kwa Katibu Mkuu wa CCM na nakala ofisi ya Bunge. Msemaji wa Katibu Mkuu wa CCM akakiri kuipokea barua hiyo, na Ofisi ya Bunge ikakiri kupokea nakala ya barua hiyo kutoka CCM.

Taarifa hiyo ya kujiuzulu ilisababisha mjadala mkubwa wa kwanini ipelekwe CCM badala ya ofisi ya Bunge kama katiba inavyoelekeza. Mjadala huo ulihitimishwa na taarifa ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa alichokifanya Spika Ndugai kuandika barua CCM badala ya Bungeni ni sawa tuu. Mimi nami nikaweka ukosoaji wangu ila ukosoaji wangu ulikuwa ni a constructive criticism kwa kukosoa na kushauri kitu sahihi cha kufanyika. Je, wajua haramu isipoharimishwa inageuka halali? Na batili isipobatilishwa inageuka halali. Je, tuhalalishe ubatili huu kwa mhimili wetu wa Bunge?

Mimi nilisema jambo fulani likielekezwa na katiba namna ya kufanyika, hakuna tena mjadala lifanyikeje, ni lazima lifanyike kwa jinsi ile ile katiba ilivyoelekeza, likifanyika kinyume, linakuwa ni batili au batilifu. Hivyo nilionyesha kifungu cha katiba kinachoekeza Spika akijiuzulu barua yake ya kujiuzulu inaandikwa kwa nani.

Ibara hii ya 149 1 (c) ya Katiba imeelekeza Spika akijiuzulu, ataandika barua kuliarifu Bunge. Kitu kikiishwa elekezwa na katiba namna ya kufanyika, kikifanyika kwa namna nyingine yoyote kinyume cha katiba, kitu hicho ni batili. Kujiuzulu halali ni kuandika barua kwa mamlaka yako ya uteuzi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Spika kwa vyombo, imearifu ameandika barua ya kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa CCM na copy kwa Katibu wa Bunge. Katiba imeelekeza barua ya kujiuzulu Spika, itatumwa kwa Bunge. Kitendo cha Spika kuandika barua na kuituma kwa CCM kabla ya Bungeni, kumeifanya Barua ya Spika kuwa Batilifu, Bila huo ubatilifu kuondolewa, then barua hiyo imekuwa ni barua barua batili!. Katibu Mkuu wa CCM ametoa taarifa ya kupokea barua ya kujiuzulu Spika na tayari ameliarifu Bunge kuhusu kujiuzulu huko, na Bunge limeipokea taarifa hiyo b
atilifu hivyo hivyo ubatili wake na kuikubali. Huu ni ubatili!. Kama Bunge ndio mhimili wa kutunga sheria, Bunge lisipofuata katiba kwa kuukubali ubatili, nani atafuata katiba?.

Haki ya CCM Kupokea barua ya kujiuzulu, ni kama Mhe Spika JYN angejiuzulu uanachama wa CCM, hivyo kupoteza ubunge wake na uspika, ndipo CCM ingeliarifu Bunge.

Jee tuliruhusu Bunge letu tukufu kukumbatia ubatili katika madogo, jee ubatili huu ukihamia katika makubwa, nani atakuwa na jeuri ya kulihoji Bunge?
Hivyo nilitoa ushauri ufuatao
  1. Japo Spika Mhe. JYN tayari ameisha jiuzulu uspika, kujiuzulu huko, japo ni kujiuzulu batilifu, kufuatia taarifa kupelekwa mahali kusikohusika, lakini kujiuzulu ni kujiuzulu tuu, yaani Spika Ndugai ameishajiuzulu, lakini kwa kuheshimu katiba, lazima ubatili katika barua yake ya kujiuzulu uondolewe kwa kuandikwa barua rasmi kwa mujibu wa katiba.
  2. Kwa vile tayari CCM imeisha kiri kuipokea barua ile batilifu, Bunge nalo limekiri kuipokea barua kutoka CCM, marekebisho ya kuondoa ubatili huu, yafanyike kimya kimya. Spika mstaafu aelekezwe kuandika barua nyingi na Bunge lipokee kimya kimya barua mpya ya kujiuzulu kwa Spika iliyoandikwa kwa mujibu wa katiba, for filing kisha Bunge ndio litoe copy kwa CCM.
Kufuatia ubatili huu, Kiongozi wa NCCR Mageuzi, James Mbatia, amefungua shauri Mahakama Kuu kuupinga ubatili huu, serikali ikaleta mahakamani barua rasmi ya Spika Ngugai kujiuzulu Uspika, ambayo imeonyesha Spika Ndugai, amejiuzulu kwa mujibu wa katiba, ni hii
View attachment 2100876
Barua hii ni utekelezaji wa ule ushauri wangu wa iandikwe barua nyingine kimya kimya na kuireplece ile barua batili. Barua yenyewe rasmi sasa ndio hii, na ndiyo iliyopelekea shauri la Mbatia kutupwa!. Japo ile taarifa ya kujiuzulu batili imeoishaondolewa kwenye website ya Bunge, lakini taarifa za CCM kuipokea barua batili ile ziliishatolewa na Bunge kuipokea barua batili ile ziliisha tolewa, ila ukienda kwenye files, hukuti tena barua batili, sasa utakutana na barua halali.

Natoa wito wa dhati kwa Serikali yangu, kukosea makosa madogo madogo is not a sin, to err is a human nature, kunapotokea makosa madogo madogo kama haya, na serikali kukosolewa, ni vitu vido tuu vya kurekebisha makosa na maisha yakaendelea. Serikali yetu ingekuwa inakubali makosa na kufuata ushauri, hii sintofahamu yote hadi kufikishana mahakamani, tusingefika huku kote. Hili jambo lilikuwa ni jambo dogo tuu, baada ya Bunge kutoa taarifa ya kujiuzulu kwa Spika Ndugai ikionyesha ameandika barua CCM, badala ya Ofisi ya Bunge, Bunge lingetoa taarifa ya pili kuonyeshea kulifanyika kosa dogo kwa barua kuelekezwa CCM, badla ya Ofisi ya Bungena kuonyesha kuwa Barua imeandikwa kwa Katibu wa Bunge na copy ndio kupalekwa CCM.

Unapokosoa kwa kuandika na kushauri, kitu cha kufanyika, halafu ukaona ushauri wako umefuatwa kama ulivyo, na makosa yamerekebishwa kama ulivyoshauri, huna budi kuandika tena na kutoa pongezi kwa serikali yetu kuwa ni serikali sikivu na kuuondoa ubatili ule, hivyo hapa nalipongeza Bunge letu Tukufu kwa kuondoa ubatili wa Barua ya Kujiuzulu kwa Spika Ndugai sasa imefuata katiba. Hongera sana kwa hili.

Sasa kumebakia ubatili mmoja tuu wa Naibu Spika, ajiuzulu kwanza nafasi ya unaibu Spika kabla ya kugombea Uspika na akiisha jiuzulu uNaibu Spika, ndipo angombee Uspika.

Nawatakia Jumapili Njema.
Wasalaam

Paskali
Barua mpya mbona haijasema kama inafuta barua ya awali?

Maana ndio utaratibu
 
Kiti kilicho wazi ni cha Spika, Naibu Spika yupo ni Dr. Tulia Akson.
Katiba imeelekeza baadhi ya viongozi hawaruhusiwi kugombea uspika, miongoni mwao ni Naibu Spika. Hivyo kabla hajagombea uspika, inampasa kujiuzulu kwanza unaibu Spika ndipo agombee uspika.
P
Hii nchi Nani analiharibu kwa kukubali uvunjifu wa katiba na taribu waziwazi hivi?
Ni wakati gani Wana habari mnatakiwa kuwabarisha jamii kuhusiana na uvunjifu wa katiba kama ilivyo Sasa?
Kuna watu wapo kwenye sekta muhimu na nyeti sana lakini hawajitambui tu, mojawapo ya hao watu ni waandisi wa habari...hapa Tanzania ni mabogus ziro kabisa.
Wanastahili kuuliwa na kilufutwa kabisa, jinga kwelikweli.
 
Barua mpya mbona haijasema kama inafuta barua ya awali?

Maana ndio utaratibu
Ushauri wangu ni kwa vile the original letter was never on public, hivyo nikashauri marekebisho yafanywe kimya kimya, kwa kunyofoa na kupachika kimya kimya, hivyo hata ile taarifa kwa media iliyosema barua imepelekwa CCM, imeisha nyofolewa kimya kimya from Bunge Website.
Mambo ni kimya kimya.
P
 
Ni wakati gani Wana habari mnatakiwa kuwabarisha jamii kuhusiana na uvunjifu wa katiba kama ilivyo Sasa?
Kuna watu wapo kwenye sekta muhimu na nyeti sana lakini hawajitambui tu, mojawapo ya hao watu ni waandisi wa habari...hapa Tanzania ni mabogus ziro kabisa.
Wanastahili kuuliwa na kilufutwa kabisa, jinga kwelikweli.
Duh yaani unatuombea kifo!.
Huku ni kutupigia ramli chonganishi!.
P
 
Ushauri wangu ni kwa vile the original letter was never on public, hivyo nikashauri marekebisho yafanywe kimya kimya, kwa kunyofoa na kupachika kimya kimya, hivyo hata ile taarifa kwa media iliyosema barua imepelekwa CCM, imeisha nyofolewa kimya kimya from Bunge Website.
Mambo ni kimya kimya.
P
Hakuna bunge hapo hilo ni genge la wahuni tupu
 
Ibara hii ya 149 1 (c) ya Katiba imeelekeza Spika akijiuzulu, ataandika barua kuliarifu Bunge. Kitu kikiishwa elekezwa na katiba namna ya kufanyika, kikifanyika kwa namna nyingine yoyote kinyume cha katiba, kitu hicho ni batili. Kujiuzulu halali ni kuandika barua kwa mamlaka yako ya uteuzi.
Kwa bahati mzuri, huwa nasoma katiba mara kwa mara! Na hapa wala sina sababu ya kufungua katiba kukuambia HAKUNA PAHALA POPOTE KWENYE IBARA YA 149 (1) (C) ILIPOTAJA HABARI ZA BARUA!

Swahili version imetaja TAARIFA, na newest version ambayo ipo kwa lugha ya mabeberu imesema NOTICE of Resignation!! So, utakuwa sahihi endapo BARUA = TAARIFA=NOTICE!

Kutokana na hilo, mwanzoni kabisa wakati Ndugai anajiuzulu nilisema wazi sioni kama Ndugai amekosea. haidhuru hata kama majority walisema kujiuzulu kwako hakukufuata katib!!

Na nilisema wazi kwamba mchakato wa kumpata Spika kwa mtu ambae ni mbunge unaanzia kwenye chama! Na chama kikishapitisha jina, anayewasilisha jina kwa Katibu wa Bunge ni chama chake na sio Mgombea Mteule kama isemavyo Kanuni #7(3) ya Bunge kwamba:-
Inapofika wakati wa Uchaguzi wa Spika, Chama chochote cha Siasa chenye kusudio la kushiriki kwenye uchaguzi huo kitawasilisha kwa Katibu wa Bunge jina moja tu ama la Mbunge wa Chama hicho au la mtu mwingine yeyote wa Chama hicho aliye na sifa za kuwa Ubunge kuwa mgombea wake.
Na ndo maana nikasema, kwa mchakato kama huo, Uspika wa mtu upo mikononi mwa chama zaidi kuliko kwa Katibu wa Bunge! Chama kikimfukuza uanachama, Uspika unafia hapo hapo hata kama Katibu wa Bunge ni mjomba wako!

Ni kutokana na hilo ndo maana hata anapolazimika kujiuzulu, mwenye haki ya kupata BARUA ni Chama kwa sababu ndicho kilimtuma akagombee na sio Katibu wa Bunge!! Kama ataandika na nakala kwa Katibu wa Bunge, well and good, Ibara ya 149(1)(c) INAMLAZIMISHA kutoa TAARIFA (na sio barua) kwenye bunge!!

Lakini kwavile suala la Spika lina public interest, ndipo kupitia barua ya kujiuzulu, Chama kitautaarifu umma kwa kutoa TAARIFA kwamba XYZ amejiuzulu! Na Katibu wa Bunge nae kwavile atakuwa amearifiwa kuhusu kujiuzulu kwa Spika, awe alipewa nakala ya barua au taarifa, nae atakachofanya ni kutoa TAARIFA kwa umma kwamba XYZ amejiuzulu Uspika!!

Unaanzaje kwa mfano, kuanza kupeleka barua kwa Katibu wa Bunge, and assume Katibu wa Bunge anakubali kujiuzulu kwako wakati aliyekutuma ukagombee Uspika ni chama?!
 
Waheshimiwa wepi?.
Mimi ni mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, naandika just for the love of it, naandika bure kwa kujitolea bure bila kulipwa na yeyote.
P
Unaishauri serilaki kupita uchochoro na unafurahi kuwa ni sikivu haya mkuu we ni mwanahabari ngulin
 
Kwa hiyo Bunge/Serikali kwa kushirikiana na Ndugai waneandika barua juzi na kurudisha tarehe nyuma ionekane iliandikwa Jan 6? Je, hili si kosa kisheria? Mbatia afungue kesi nyingine.
Barua ya marekebisho bila Shaka iliandikwa baada ya wiki 2 kupita, lakini tarehe ikawa hiyo hiyo 6 January! Kwa maana hiyo, hiyo ni barua ya kughushi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Wanabodi,
Hii ni Nipashe ya Leo, 30.01.2022
View attachment 2100761
Kama kawaida yangu, kila nipatapo fursa huteremka na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" leo ni swali na pongezi. "Serikali inapokosolewa kwa constructive criticism, kama ushauri uliotolewa ni ushauri nzuri wenye maslahi kwa taifa, jee serikali ifuate ushauri huo, au iupuuzie kwa kushupaza shingo?. Hongera sana Bunge letu Tukufu kwa kufuata ushauri na kutuondolea ubatili katika Barua ya kujiuzulu Spika JYN!.

Kikawaida ni a being, ila sio human, hivyo serikali haiwezi kukosea jambo lolote, lakini serikali inaendeshwa na watu na inaongozwa na watu, human beings, watu hao wanaoongoza serikali ni binadamu na sio malaika, hivyo wanaweza kukosea, watu hao wanapokosea, inahesabika kuwa ni serikali ndio imekosea, hivyo serikali inapokosea au kwa kukosea yenyewe au kwa kukoseshwa, lazima ikubali kuwajibika kwa makosa hayo. Japo nimesema serikali kama serikali haiwezi kukosea, ila watendaji ndio wanaokosea na kuikosesha serikali.

Kila serikali inapofanya makosa, sometimes huwa kunatokea watu wenye jicho tunduizi, ambao wanaona makosa hayo na kuikosoa serikali kwa kutumia ukosoaji wa ujengaji (constructive criticism) ambao hufanyika kwa kuonyesha kosa lililofanyika na wakati huo huo kutoa mapendekezo ya jinsi ya kurekebisha makosa na kushauri a way forward kurekebisha makosa yaliyofanyika yasijirudie na maisha yaendelee. Naishauri serikali yetu tukufu, pale inapokosolewa kwa makosa ya wazi, kwanza isikasirike, pili ifuate ushauri na kurekebisha makosa na kujitahidi makosa kama hayo yasijirudie. Kitendo cha serikali kukubali kosa, not expressly but impliedly kwa kurekebisha kosa bila kukiri kosa, kwa kupokea ushauri, sio udhaifu ni uimara, na kuonyesha serikali yetu ni serikali sikivu.

Moja ya makala yangu ya nyuma, nilishauri, viongozi wa kisiasa na wa serikali, wanapofanya makosa ya wazi na kuifanya serikali ionekane imekosea, wanapaswa kwanza kukubali makosa, kuomba msamaha na kuwajibika. Hiki ndicho kilichofanyika kwa Spika aliyejiuzulu, Mhe. Job Ndugai, Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere? kwanza alikubali makosa, kisha akaomba msamaha, japo msamaha wenyewe ulikuwa ni msamaha batili Ndoa halali, ndoa batili na ndoa batilifu. Je, wajua pia kuna msamaha halali wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu? Msamaha ule ni batilifu!
akidhani atasamehewa, na baada ya kuomba msamaha huo batili, sisi waona mbali tukashauri, Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away? na baada ya shinikizo, ndipo JYN akakubali kujiuzulu ila huku nako alikurupuka na kuandika barua batili, hatukukaa kimya, Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away?

Taarifa ya kujiuzulu uspika ya Spika Mhe. Job Ndugai kwa vyombo vya habari, iliyosambazwa na ofisi ya Bunge, ni hii
View attachment 2100870
Taarifa hii ya Ofisi ya Bunge kwa vyombo vya habari, illionyesha Spika Ndugai ameandika barua ya kujiuzulu na kuilekeza kwa Katibu Mkuu wa CCM na nakala ofisi ya Bunge. Msemaji wa Katibu Mkuu wa CCM akakiri kuipokea barua hiyo, na Ofisi ya Bunge ikakiri kupokea nakala ya barua hiyo kutoka CCM.

Taarifa hiyo ya kujiuzulu ilisababisha mjadala mkubwa wa kwanini ipelekwe CCM badala ya ofisi ya Bunge kama katiba inavyoelekeza. Mjadala huo ulihitimishwa na taarifa ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa alichokifanya Spika Ndugai kuandika barua CCM badala ya Bungeni ni sawa tuu. Mimi nami nikaweka ukosoaji wangu ila ukosoaji wangu ulikuwa ni a constructive criticism kwa kukosoa na kushauri kitu sahihi cha kufanyika. Je, wajua haramu isipoharimishwa inageuka halali? Na batili isipobatilishwa inageuka halali. Je, tuhalalishe ubatili huu kwa mhimili wetu wa Bunge?

Mimi nilisema jambo fulani likielekezwa na katiba namna ya kufanyika, hakuna tena mjadala lifanyikeje, ni lazima lifanyike kwa jinsi ile ile katiba ilivyoelekeza, likifanyika kinyume, linakuwa ni batili au batilifu. Hivyo nilionyesha kifungu cha katiba kinachoekeza Spika akijiuzulu barua yake ya kujiuzulu inaandikwa kwa nani.

Ibara hii ya 149 1 (c) ya Katiba imeelekeza Spika akijiuzulu, ataandika barua kuliarifu Bunge. Kitu kikiishwa elekezwa na katiba namna ya kufanyika, kikifanyika kwa namna nyingine yoyote kinyume cha katiba, kitu hicho ni batili. Kujiuzulu halali ni kuandika barua kwa mamlaka yako ya uteuzi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Spika kwa vyombo, imearifu ameandika barua ya kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa CCM na copy kwa Katibu wa Bunge. Katiba imeelekeza barua ya kujiuzulu Spika, itatumwa kwa Bunge. Kitendo cha Spika kuandika barua na kuituma kwa CCM kabla ya Bungeni, kumeifanya Barua ya Spika kuwa Batilifu, Bila huo ubatilifu kuondolewa, then barua hiyo imekuwa ni barua barua batili!. Katibu Mkuu wa CCM ametoa taarifa ya kupokea barua ya kujiuzulu Spika na tayari ameliarifu Bunge kuhusu kujiuzulu huko, na Bunge limeipokea taarifa hiyo b
atilifu hivyo hivyo ubatili wake na kuikubali. Huu ni ubatili!. Kama Bunge ndio mhimili wa kutunga sheria, Bunge lisipofuata katiba kwa kuukubali ubatili, nani atafuata katiba?.

Haki ya CCM Kupokea barua ya kujiuzulu, ni kama Mhe Spika JYN angejiuzulu uanachama wa CCM, hivyo kupoteza ubunge wake na uspika, ndipo CCM ingeliarifu Bunge.

Jee tuliruhusu Bunge letu tukufu kukumbatia ubatili katika madogo, jee ubatili huu ukihamia katika makubwa, nani atakuwa na jeuri ya kulihoji Bunge?
Hivyo nilitoa ushauri ufuatao
  1. Japo Spika Mhe. JYN tayari ameisha jiuzulu uspika, kujiuzulu huko, japo ni kujiuzulu batilifu, kufuatia taarifa kupelekwa mahali kusikohusika, lakini kujiuzulu ni kujiuzulu tuu, yaani Spika Ndugai ameishajiuzulu, lakini kwa kuheshimu katiba, lazima ubatili katika barua yake ya kujiuzulu uondolewe kwa kuandikwa barua rasmi kwa mujibu wa katiba.
  2. Kwa vile tayari CCM imeisha kiri kuipokea barua ile batilifu, Bunge nalo limekiri kuipokea barua kutoka CCM, marekebisho ya kuondoa ubatili huu, yafanyike kimya kimya. Spika mstaafu aelekezwe kuandika barua nyingi na Bunge lipokee kimya kimya barua mpya ya kujiuzulu kwa Spika iliyoandikwa kwa mujibu wa katiba, for filing kisha Bunge ndio litoe copy kwa CCM.
Kufuatia ubatili huu, Kiongozi wa NCCR Mageuzi, James Mbatia, amefungua shauri Mahakama Kuu kuupinga ubatili huu, serikali ikaleta mahakamani barua rasmi ya Spika Ngugai kujiuzulu Uspika, ambayo imeonyesha Spika Ndugai, amejiuzulu kwa mujibu wa katiba, ni hii
View attachment 2100876
Barua hii ni utekelezaji wa ule ushauri wangu wa iandikwe barua nyingine kimya kimya na kuireplece ile barua batili. Barua yenyewe rasmi sasa ndio hii, na ndiyo iliyopelekea shauri la Mbatia kutupwa!. Japo ile taarifa ya kujiuzulu batili imeoishaondolewa kwenye website ya Bunge, lakini taarifa za CCM kuipokea barua batili ile ziliishatolewa na Bunge kuipokea barua batili ile ziliisha tolewa, ila ukienda kwenye files, hukuti tena barua batili, sasa utakutana na barua halali.

Natoa wito wa dhati kwa Serikali yangu, kukosea makosa madogo madogo is not a sin, to err is a human nature, kunapotokea makosa madogo madogo kama haya, na serikali kukosolewa, ni vitu vido tuu vya kurekebisha makosa na maisha yakaendelea. Serikali yetu ingekuwa inakubali makosa na kufuata ushauri, hii sintofahamu yote hadi kufikishana mahakamani, tusingefika huku kote. Hili jambo lilikuwa ni jambo dogo tuu, baada ya Bunge kutoa taarifa ya kujiuzulu kwa Spika Ndugai ikionyesha ameandika barua CCM, badala ya Ofisi ya Bunge, Bunge lingetoa taarifa ya pili kuonyeshea kulifanyika kosa dogo kwa barua kuelekezwa CCM, badla ya Ofisi ya Bungena kuonyesha kuwa Barua imeandikwa kwa Katibu wa Bunge na copy ndio kupalekwa CCM.

Unapokosoa kwa kuandika na kushauri, kitu cha kufanyika, halafu ukaona ushauri wako umefuatwa kama ulivyo, na makosa yamerekebishwa kama ulivyoshauri, huna budi kuandika tena na kutoa pongezi kwa serikali yetu kuwa ni serikali sikivu na kuuondoa ubatili ule, hivyo hapa nalipongeza Bunge letu Tukufu kwa kuondoa ubatili wa Barua ya Kujiuzulu kwa Spika Ndugai sasa imefuata katiba. Hongera sana kwa hili.

Sasa kumebakia ubatili mmoja tuu wa Naibu Spika, ajiuzulu kwanza nafasi ya unaibu Spika kabla ya kugombea Uspika na akiisha jiuzulu uNaibu Spika, ndipo angombee Uspika.

Nawatakia Jumapili Njema.
Wasalaam

Paskali
Kwa ni sawa serikali kusema uongo mahakamani? Huoni kuwa ni hatari nchi kuongozwa na viongozi wanaokosa uadilifu kiasi cha "kutengeneza" barua ya uongo na kuipeleka mahakamani?
 
Kwa bahati mzuri, huwa nasoma katiba mara kwa mara! Na hapa wala sina sababu ya kufungua katiba kukuambia HAKUNA PAHALA POPOTE KWENYE IBARA YA 149 (1) (C) ILIPOTAJA HABARI ZA BARUA!

Swahili version imetaja TAARIFA, na newest version ambayo ipo kwa lugha ya mabeberu imesema NOTICE of Resignation!! So, utakuwa sahihi endapo BARUA = TAARIFA=NOTICE!

Kutokana na hilo, mwanzoni kabisa wakati Ndugai anajiuzulu nilisema wazi sioni kama Ndugai amekosea. haidhuru hata kama majority walisema kujiuzulu kwako hakukufuata katib!!.
Mkuu Chige, kwanza asante sana kwa mchango wako huu elimishi, maana ni kupitia michango kama hii, hutoa fursa ya kuelimisha wengine walio wengi wasiojua, kama jinsi wewe na hata Mwanasheria Mkuu wa serikali, asivyojua!. Lugha ya Kiswahili, ina upungufu mkubwa wa vocabulary, hivyo kunapotokea utata wa neno lolote la katiba ya Kiswahili, tafsiri rasmi huchukuliwa kwenye katiba ya Kiingereza. Hivyo neno "taarifa" kwenye katiba ya Kiswahili, sio taarifa yoyote, maana kutoa taarifa hata kwa mdomo tuu, ni taarifa, neno "taarifa" tafsiri ya taarifa kutoka katiba ya Kiingereza ni "notice", hivyo notice has to be in black and white!, yaani lazima iwe ni kwa maandishi!. Hiyo taarifa ya maandishi, ndio barua ya kujizulu, hivyo kusoma kwako koote katiba, hujaona neno barua, ila umeona taarifa, hivyo darasa la kwanza kwako na wengine wa type yako, taarifa ndio barua!.
Na nilisema wazi kwamba mchakato wa kumpata Spika kwa mtu ambae ni mbunge unaanzia kwenye chama! Na chama kikishapitisha jina, anayewasilisha jina kwa Katibu wa Bunge ni chama chake na sio Mgombea Mteule kama isemavyo Kanuni #7(3) ya Bunge kwamba:-

Na ndo maana nikasema, kwa mchakato kama huo, Uspika wa mtu upo mikononi mwa chama zaidi kuliko kwa Katibu wa Bunge! Chama kikimfukuza uanachama, Uspika unafia hapo hapo hata kama Katibu wa Bunge ni mjomba wako!
Hapa unazungumzia vitu viwili tofauti, hapa unazungumzia mchakato wa kumpata Spika, ndio unaoanzia kwenye chama, jukumu la chama cha siasa ni kututeulia tuu mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa, jukumu la chama cha siasa, linaishia kwenye mapendekezo tuu ya mgombea. Kwenye ubunge, udiwani na urais, jukumu hilo linaishia anapopeleka majina ya wagombea wale NEC, NEC ikiisha fanya uteuzi wa wagombea wa udiwani, ubunge na urais, sasa wanakuwa ni wagombea rasmi wa uchaguzi wa umma, kwa udhamini tuu wa chama fulani, lakini wanachaguliwa na umma, na wakiisha chaguliwa wanakuwa ni madiwani, wabunge na rais wa umma, na sio madiwani, wabunge na rais wa CCM, hawakuchaguliwa na CCM, wamechaguliwa na umma wa Watanzania, hawawajibiki kwa CCM, wanawajibika kwa umma. CCM has nothing to do with wagombea wake waliochaguliwa. Hili somo nililitoa katika bandiko hili... The Doctrine ya Mwanasiasa Kuwa Maarufu Kuliko Chama!-Ni "Utumishi wa Watu VS Utumishi wa Chama!.
Vivyo kwa Spika, jukumu la chama cha siasa, ni kututeulia tuu mgombea, akiisha chukua fumu ya kugombea Uspika na kupitishwa, jukumu la chama cha siasa, linaishia hapo, sasa anakuwa ni mgombea wa Uspika wa umma, anachaguliwa na wabunge wa Bunge la JMT, hata kama wabunge wote ni wa CCM, Spika anayechaguliwa sio Spika wa CCM, ni Spika wa Bunge la JMT, hata kama atachaguliwa na wabunge wa CCM tuu, bado atahesabiwa amechaguliwa na Bunge la JMT, hata kama wabunge wote 100% watakuwa ni wana CCM, lakini atahesabiwa amechaguliwa na Bunge la JMT na sio Bunge la CCM, na baada ya Spika kuchaguliwa, anakuwa ni Spika wa Bunge la JMT na sio Spika wa CCM, na anawajibika kwa Bunge la JMT na sio kwa CCM, hivyo siku anajiuzulu, anajiuzulu kwa Bunge la JMT na sio kujiuzulu CCM.
Ni kutokana na hilo ndo maana hata anapolazimika kujiuzulu, mwenye haki ya kupata BARUA ni Chama kwa sababu ndicho kilimtuma akagombee na sio Katibu wa Bunge!! Kama ataandika na nakala kwa Katibu wa Bunge, well and good, Ibara ya 149(1)(c) INAMLAZIMISHA kutoa TAARIFA (na sio barua) kwenye bunge!!

Lakini kwavile suala la Spika lina public interest, ndipo kupitia barua ya kujiuzulu, Chama kitautaarifu umma kwa kutoa TAARIFA kwamba XYZ amejiuzulu! Na Katibu wa Bunge nae kwavile atakuwa amearifiwa kuhusu kujiuzulu kwa Spika, awe alipewa nakala ya barua au taarifa, nae atakachofanya ni kutoa TAARIFA kwa umma kwamba XYZ amejiuzulu Uspika!!

Unaanzaje kwa mfano, kuanza kupeleka barua kwa Katibu wa Bunge, and assume Katibu wa Bunge anakubali kujiuzulu kwako wakati aliyekutuma ukagombee Uspika ni chama?!
Hapa you are wrong my friend, Spika ni Spika wa Bunge la JMT na sio Spika wa CCM, anawajibika kwa Bunge na sio kwa chama, hivyo akijuzulu uspika, anaandika kwa Bunge na sio kwa Chama!.

Kwavile ameupata Uspika kutokana na kudhaminiwa na chama kuwa mbunge, kisha akadhaminiwa tena kugombea Uspika, kama angajiuzulu uanachama wa CCM, hivyo kupoteza ubunge na uspika, hapo sasa ndio angeandika barua kwenye plain paper, sio headed paper ya Bunge, kumtaarifu Katibu Mkuu wa CCM kuwa amejitoa CCM, hivyo kutokana na kujitoa huko, amepoteza ubunge na Uspika, then hapo ndipo CCM ingekuwa right kulitaarifu Bunge, kuwa mwanachama wetu XYZ aliyekuwa mbunge na Spika, amejivua uanachama hivyo nafasi ya ubunge na spika zipo wazi. Au kama angafukuzwa uanachama wa CCM na hivyo kupoteza ubunge, na uspika, kutokana na vikao vya CCM, hapo ingekuwa sawa kwa CCM kuliarifu Bunge.

Naomba kuchukua fursa hii kukumbushia kuwa shurti la mgombea kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba, kama nilivyo eleza hapa. Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.
Mgombea akiishachaguliwa anakuwa ni mtumishi wa umma, kitendo cha chama cha siasa, kumfukuza uanachama na hivyo kupoteza utumishi wake wa umma, ni kukifanya chama kupora mamlaka ya umma!.
Katiba ni ya umma, inapata mamlaka yake kutokana na umma, mgombea anaechaguliwa na umma, anawezaje kupoteza uongozi wa umma kwa kutimuliwa uanachama wa kakikundi fulani ka watu kanakoitwa chama?. Nani zaidi kati ya chama na umma?. This is wrong!.
P.
 
Back
Top Bottom