Serikali inavyo piga marufuku shamrashamra za Pasaka, hawakuona kelele mule Bungeni?

Yaani serikali inahangaishana na watu kwenye mambo ya imani.
Ndo maana msibani watu hula sasa sijui iliwakamata kwa nini
Hata siku hizi misibani kuna miziki watu wanaburudika kujiliwaza, target ya wauzuliaji misibani ni kuhakikisha wanaenda kuwapa tumaini wafiwa kwa kuwafariji sambamba na kuwaondolea majonzi kujisahaulisha na yaliyotokea

Na ndio maana waislam msiba wao haudumu, kwasababu hakuna point ya kuendelea kutumia muda mwingi kumfikiria mfu
 
Mambo mengine serikali ituache
 

Sasa mle bungeni si mjengoni? Hizo kelele zilipigwa ndani ya bunge au mitaani?
 
Serikali ituache kidogo kwa hili
Viongozi wa serikali wanatambua kuwa baadhi ya watanzania walikuwa hawampendi mtu huyu. Walitakiwa wajiulize kwa nini, kisha wao wajirekebishe kwa kuepuka matendo yaliyosababisha wasimpende. Kutoa maagizo kama haya, ni kulazimisha watu wote wampende, na zaidi sana kuingilia imani za watu. Hilo haliwezekani. Th 17/03/2021 msiba ulipotangazwa, kuna watu walikesha wakinywa pombe. Sijui walikuwa wakinywa kwa furaha au kwa majonzi. Kilangila.
 
Serikali ituache kidogo tusherekee na kupata pisi kali
 
Hivi wakristu tumekuwa wadhaifu kiasi hiki kwamba Magufuli ni muhimu kuliko ufufuo wa bwana YESU?
 
Unaweza kuchinja ka mbuzi kako ukaja kukamatwa kuwa unasherekea msiba.
Tunakukamata, na ka mbuzi tunabeba kama tunaenda kutupa. Tukifika sehemu tunaangalia kama hakuna watu wanaotutazama tunagawana tunapeleka majumbani kwetu. Na ndiyo utajua kumbe maendeleo yana vyama.
 
Nafikiri kule ukaguzi wa vyeti haukufanyika, hivi kati ya tukio la pasaka ambalo kwa imani ya kikiristo linaashiria kufufuka kwa mwokozi wa ulimwengu Yesu Kristo na tukio la kumwombolezea magufuli, lipi ni tukio kubwa linalopaswa kupewa kipaumbele...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…