Serikali inunue Magari ya idara zote za Halmashauri ili kuleta tija na Ufanisi Nchini

Serikali inunue Magari ya idara zote za Halmashauri ili kuleta tija na Ufanisi Nchini

mkamanga original

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2015
Posts
637
Reaction score
663
Muundo wa Halmashauri zetu zina idara 12 na vitengo 6. Hivyo kufanya jumla ya wakuu wa idara na vitengo kuwa 18 . Kabla ya kuondoka watalaam wa Maji kwenda RUWASA Halmashauri ilikuwa na wakuu wa idara na vitengo 19.

Idara zilizopo katika Halmashauri ni idara ya Elimu Msingi, Idara ya elimu Sekondari, Idara ya utumishi na utawala, Idara ya Mipango na ufuatiliaji, Idara ya Ujenzi, Idara ya Kilimo na umwagiliaji, Idara ya mifugo na Uvuvi, Idara ya Ardhi na Maliasili(ijapokuwa wameshahamia wizarani),Idara ya Afya , Idara ya usafi na mazingira, Idara ya Fedha. Vitengo ni Kitengo cha uchaguzi, kitengo cha manunuzi, kitengo cha ukaguzi wa ndani, kitengo sheria, kitengo cha Tehama, na Kitengo cha Nyuki.

Kimsingi wakuu wa idara na vitengo katika Halmashauri ndio wanao unda timu ya usimamizi wa Halmashauri ( CMT- Council management team). Wakuu wa idara na vitengo wanafanya kazi chini ya Mkurugenzi, Mkurugenzi wa Halmashauri ndio mwenyekiti wa CMTs .Timu hii ndio inayosimamia shughuri za kila siku za Halmashauri , kila mkuu wa idara na vitengo anajukumu la kusimamia watumishi wa chini yake kwa kuhakikisha anawafikia wadau wake waliopo chini kabisa, ikiwa ni pamoja na wananchi .

Wakuu wa idara na vitengo wote wana hadhi sawa, kwa maana ya stahiki zao na katika usimamizi .Tofauti ipo katika utekelezaji wa Majukumu na uzito wa majukumu.

Tumeona serikali kupitia waziri mkuu akikabidhi magari kwa wakuu wa idara ya elimu Msingi, Magari hayo yatasaidia katika ufuatiliaji wa shughuri za elimu katika Halmashauri. Nitoe pongezi za dhati kwa serikali kwa kuliona hilo.

Lakini ushauri wangu kwa serikali ni wakuu idara walio wengi hawana magari ,hivyo inawawia vigumu sana katika kutekeleza majukumu yao ya kila Siku . Kuwaachia Halmashauri wanunue magari kwa ajili ya matumizi ya idara na vitengo imekuwa changamoto kubwa. Ziko idara ambazo ukifanya sensa Leo kati ya Halmashauri 185 utakuta karibu 95% ya idara hizo hazina magari pamoja na umuhimu wake .Mfano tu idara ya ujenzi ambayo ndio wasimamizi miradi ya maendeleo hawana magari kabisa fanyeni sensa muone . wahandisi wa halmashauri matokeo yake wanafanya kazi ya usimamizi wa miradi kwa Simu,Siku hizi serikali inapeleka fedha moja kwa moja kwenye mashule,waandisi wakisha waandalia BOQ walimu na kuwakabidhi basi hawana uwezo wa kwenda site kwenda kufanya ufuatiliaji ,ndio maana miradi mingi baada ya miaka 2 utakuta sakafu imetifuka ,madarasa yamebaki vumbi tu, kwa sababu ya usimamizi hafifu. Utakuta Halmashauri ina magari 4 , mweka hazina atumie hilo hilo kwenye mapato, afisa elimu atumie hilo hilo kwenye elimu , afisa kilimo atumie hilohilo, Afisa mipango atumie hilo hilo katika kukusanyia takwimu mbalimbali za miradi. Afisa maendekeo ya Jamii atumie hill hill kwenda kugawa fedha za Tasaf .Gari ambalo linakuwa nzima muda wote ni la Mkurugenzi tu, mengine yote hayatengenezwi.

Waziri mkuu aziagize kila wizara ihakikishe inanunua magari kwa ajili ya wakuu wa idara wao waliopo kwenye Halmashauri, wananchi wanakosa baadhi ya huduma kwa sababu tu maafisa wanashindwa kuwafikia na kutatua changamoto zao. Serikali inaagiza tu maafisa wasikae ofisini, huku vijijini hao maafisa wanaendaje , wakodi yebo au boda boda.

Mama Ummy Mwalimu saidia hili, mwenzako Jaffor alishindwa kabisa hapo tamisemi kuwa mbunifu wa kuzitafutia ufumbuzi changamoto za Halmashauri kazi yake maneno mengi utekelezaji sifuri, Alikuwa amekosa ubunifu . Mshauri Rais kule wizara ya ujenzi kuna magari mengi ya miradi ya wahisani ambayo imephase out, chukueni hayo pelekeni Halmashauri, Bandarini kuna magari mengi ambayo wamiliki wake wameshindwa kuyagomboa chukueni hayo pelekeni Halmashauri. Mtakuwa mmezisaidia Halmashauri kuwafikia wananchi kwa wakati.Wizara ya tamisemi ndio wizara ambayo IPO jirani na wananchi, hivyo wapewe magari, au vile vyanzo ambavyo vilichukuliwa virudishwe Halmashauri
 
Hapo ulipoandika mhandisi anamkabidhi mwalimu BoQ wanakabidhiana wakiwa wapi?? Kama ni ofisini kwa mhandisi he mwalimu anafikaje ofisini kwa mhandisi??Kama ni shuleni mhansi kafikaje shuleni, wote hao ni maafisa kwa nafasi take hivyo suala la usafiri libalance kotekote
 
Ahsante kwa elimu nzuri ila sijaona idara ya fedha, mipango na biashara hao wanasimama wapi.
 
Hapo ulipoandika mhandisi anamkabidhi mwalimu BoQ wanakabidhiana wakiwa wapi?? Kama ni ofisini kwa mhandisi he mwalimu anafikaje ofisini kwa mhandisi??Kama ni shuleni mhansi kafikaje shuleni, wote hao ni maafisa kwa nafasi take hivyo suala la usafiri libalance kotekote
Kwan kwa sasa kuna mtumishi wa serikali mpaka amefikia kuwa mkuu wa idara hajawa na gari lake binafsi labda kama ametoka chuoni anakabidhiwa idara.
 
Magari ni mzigo kwa walipa kodi.Watumishi wapewe misamaha ya kodi waingize magari binafsi Ili kupunguza ulazima wa manunuzi ya magari
Kutumia magari binafsi kwenye shughuri za serikali ,serikali ilishatoa maelekezo ,lakini inascourage kwa sababu kuna utararibu umewekwa wa kuchukua mafuta ya serikali na kutia kwenye magari binafsi. Unaweza sababisha hoja za ukaguzi, kama utaendekezwa sana, kwa sababu sasa wanaaweza kutumia mwanya huo kutumia mafuta ya serikali kwa shughuri zao binafsi
 
Hapo ulipoandika mhandisi anamkabidhi mwalimu BoQ wanakabidhiana wakiwa wapi?? Kama ni ofisini kwa mhandisi he mwalimu anafikaje ofisini kwa mhandisi??Kama ni shuleni mhansi kafikaje shuleni, wote hao ni maafisa kwa nafasi take hivyo suala la usafiri libalance kotekote
Mwalimu ndio anayekuja ofisin iwe kwa pikipiki au baiskeli.Mwalimu anaweza kuwa afisa lakini asiwe kiongozi kwa miundo ya utumishi was umma. Mkuu wa Idara ni kiongozi lakini mwalimu sio kiongozi kwa mujibu wa muundo uliopo wa utumishi wa umma . mtumishi wa umma anaweza kuwa afisa lakini asiwe kiongozi. Kiongozi yeyote anakuwa kwenye daraja la mshahara LSSE kwa maana ya Leaders Scale of Salary , lakini wengine wote pamoja na hao walimu uliowataja mishahara yao in tgs au tgts. Uikisikia mtumishi analipwa LSSE ni above 3M
 
Ahsante kwa elimu nzuri ila sijaona idara ya fedha, mipango na biashara hao wanasimama wapi.
Zipo soma vizuri hapo juu,ila biashara sio idara wala kitengo.biashara ipo chini ya idara ya fedha na ndio maana inaitwa idara ya fedha na biashara na mkuu wake wa idara ni mwekahazina
 
Kutumia magari binafsi kwenye shughuri za serikali ,serikali ilishatoa maelekezo ,lakini inascourage kwa sababu kuna utararibu umewekwa wa kuchukua mafuta ya serikali na kutia kwenye magari binafsi. Unaweza sababisha hoja za ukaguzi, kama utaendekezwa sana, kwa sababu sasa wanaaweza kutumia mwanya huo kutumia mafuta ya serikali kwa shughuri zao binafsi
Mbona viongozi wengine waandamizi wa serikali (mawaziri, wakuu wa wakala na idara kubwa n.k.) utumia magari ya serikali kwa shughuli zao binafsi? Waziri anavyoenda kanisani au msikitini kwa gari la serikali, hiyo siyo shughuli binafsi?

Kama alivyosema mdau hapo juu, nami nakubali kabisa haya magari ni mzigo mkubwa sana kwa serikali. Nilishawahi kusema humu kwamba tunapaswa kuwa na ‘government car pools’ kubwa katika kila wilaya, idara na taasisi yenye magari ya aina (size, space, power etc.) tofauti tofauti kukidhi mahitaji husika ya matumizi. Pesa itakayookolewa ikaongezee bajeti za kuboresha usafirishaji na usafiri wa umma. Wakuu wa idara na taasisi watakuwa na options za kutumia magari yao binafsi (kwa kupata misamaha ya kodi na incentives zingine) ama usafiri wa umma kwa shughuli za kutimiza wajibu wao.
 
Kwan kwa sasa kuna mtumishi wa serikali mpaka amefikia kuwa mkuu wa idara hajawa na gari lake binafsi labda kama ametoka chuoni anakabidhiwa idara.
Mhhh, wapo wengi tu ,zamani ilikuwa unaweza kaa miaka 4 unapata ukuu wa idara lakini siku hizi ni ngumu mpaka ufike afisa mwandamizi ni miaka 10
 
Mbona viongozi wengine waandamizi wa serikali (mawaziri, wakuu wa wakala na idara kubwa n.k.) utumia magari ya serikali kwa shughuli zao binafsi? Waziri anavyoenda kanisani au msikitini kwa gari la serikali, hiyo siyo shughuli binafsi?

Kama alivyosema mdau hapo juu, nami nakubali kabisa haya magari ni mzigo mkubwa sana kwa serikali. Nilishawahi kusema humu kwamba tunapaswa kuwa na ‘government car pools’ kubwa katika kila wilaya, idara na taasisi yenye magari ya aina (size, space, power etc.) tofauti tofauti kukidhi mahitaji husika ya matumizi. Pesa itakayookolewa ikaongezee bajeti za kuboresha usafirishaji na usafiri wa umma. Wakuu wa idara na taasisi watakuwa na options za kutumia magari yao binafsi (kwa kupata misamaha ya kodi na incentives zingine) ama usafiri wa umma kwa shughuli za kutimiza wajibu wao.
Hujanielewa, nimezungumzia watumishi kutumia magari binafsi kwa shughuri za serikali na sijazungumzia watumishi kutumia magari ya serikali kwa shughuri binafsi, kwa viongozi wamegawanyika kwa makundi tofauti na stahiki zao zinatofautiana ,mfano mkuu wa idara analipwa 16M za fenicha kila baada ya miaka 5 ,lakini wapo viongozi wengine kila baada ya miaka 3,
 
Kwan kwa sasa kuna mtumishi wa serikali mpaka amefikia kuwa mkuu wa idara hajawa na gari lake binafsi labda kama ametoka chuoni anakabidhiwa idara.
Sasa gari lake binafsi ndiyo alitumie kwenda nalo site?
 
Mkuu umesahau Idara ya Maendeleo ya Jamii.
Halafu kuhusu TASAF wao wana magari yao ,TASAF ni kitengo siku hizi.
 
Muundo wa Halmashauri zetu zina idara 12 na vitengo 6. Hivyo kufanya jumla ya wakuu wa idara na vitengo kuwa 18 . Kabla ya kuondoka watalaam wa Maji kwenda RUWASA Halmashauri ilikuwa na wakuu wa idara na vitengo 19.

Idara zilizopo katika Halmashauri ni idara ya Elimu Msingi, Idara ya elimu Sekondari, Idara ya utumishi na utawala, Idara ya Mipango na ufuatiliaji, Idara ya Ujenzi, Idara ya Kilimo na umwagiliaji, Idara ya mifugo na Uvuvi, Idara ya Ardhi na Maliasili(ijapokuwa wameshahamia wizarani),Idara ya Afya , Idara ya usafi na mazingira, Idara ya Fedha. Vitengo ni Kitengo cha uchaguzi, kitengo cha manunuzi, kitengo cha ukaguzi wa ndani, kitengo sheria, kitengo cha Tehama, na Kitengo cha Nyuki.

Kimsingi wakuu wa idara na vitengo katika Halmashauri ndio wanao unda timu ya usimamizi wa Halmashauri ( CMT- Council management team). Wakuu wa idara na vitengo wanafanya kazi chini ya Mkurugenzi, Mkurugenzi wa Halmashauri ndio mwenyekiti wa CMTs .Timu hii ndio inayosimamia shughuri za kila siku za Halmashauri , kila mkuu wa idara na vitengo anajukumu la kusimamia watumishi wa chini yake kwa kuhakikisha anawafikia wadau wake waliopo chini kabisa, ikiwa ni pamoja na wananchi .

Wakuu wa idara na vitengo wote wana hadhi sawa, kwa maana ya stahiki zao na katika usimamizi .Tofauti ipo katika utekelezaji wa Majukumu na uzito wa majukumu.

Tumeona serikali kupitia waziri mkuu akikabidhi magari kwa wakuu wa idara ya elimu Msingi, Magari hayo yatasaidia katika ufuatiliaji wa shughuri za elimu katika Halmashauri. Nitoe pongezi za dhati kwa serikali kwa kuliona hilo.

Lakini ushauri wangu kwa serikali ni wakuu idara walio wengi hawana magari ,hivyo inawawia vigumu sana katika kutekeleza majukumu yao ya kila Siku . Kuwaachia Halmashauri wanunue magari kwa ajili ya matumizi ya idara na vitengo imekuwa changamoto kubwa. Ziko idara ambazo ukifanya sensa Leo kati ya Halmashauri 185 utakuta karibu 95% ya idara hizo hazina magari pamoja na umuhimu wake .Mfano tu idara ya ujenzi ambayo ndio wasimamizi miradi ya maendeleo hawana magari kabisa fanyeni sensa muone . wahandisi wa halmashauri matokeo yake wanafanya kazi ya usimamizi wa miradi kwa Simu,Siku hizi serikali inapeleka fedha moja kwa moja kwenye mashule,waandisi wakisha waandalia BOQ walimu na kuwakabidhi basi hawana uwezo wa kwenda site kwenda kufanya ufuatiliaji ,ndio maana miradi mingi baada ya miaka 2 utakuta sakafu imetifuka ,madarasa yamebaki vumbi tu, kwa sababu ya usimamizi hafifu. Utakuta Halmashauri ina magari 4 , mweka hazina atumie hilo hilo kwenye mapato, afisa elimu atumie hilo hilo kwenye elimu , afisa kilimo atumie hilohilo, Afisa mipango atumie hilo hilo katika kukusanyia takwimu mbalimbali za miradi. Afisa maendekeo ya Jamii atumie hill hill kwenda kugawa fedha za Tasaf .Gari ambalo linakuwa nzima muda wote ni la Mkurugenzi tu, mengine yote hayatengenezwi.

Waziri mkuu aziagize kila wizara ihakikishe inanunua magari kwa ajili ya wakuu wa idara wao waliopo kwenye Halmashauri, wananchi wanakosa baadhi ya huduma kwa sababu tu maafisa wanashindwa kuwafikia na kutatua changamoto zao. Serikali inaagiza tu maafisa wasikae ofisini, huku vijijini hao maafisa wanaendaje , wakodi yebo au boda boda.

Mama Ummy Mwalimu saidia hili, mwenzako Jaffor alishindwa kabisa hapo tamisemi kuwa mbunifu wa kuzitafutia ufumbuzi changamoto za Halmashauri kazi yake maneno mengi utekelezaji sifuri, Alikuwa amekosa ubunifu . Mshauri Rais kule wizara ya ujenzi kuna magari mengi ya miradi ya wahisani ambayo imephase out, chukueni hayo pelekeni Halmashauri, Bandarini kuna magari mengi ambayo wamiliki wake wameshindwa kuyagomboa chukueni hayo pelekeni Halmashauri. Mtakuwa mmezisaidia Halmashauri kuwafikia wananchi kwa wakati.Wizara ya tamisemi ndio wizara ambayo IPO jirani na wananchi, hivyo wapewe magari, au vile vyanzo ambavyo vilichukuliwa virudishwe Halmashauri
Uko sahihi kabisa na umeandika ukweli kabisa, na suluhisho ni serikali kupata pesa za kutosha ili kukiza hayo mahitaji, ila sehemu wanayokosea ni kuwavuruga Wafanya biashara, hawa watu ndio wenye uwezo wa kutengeneza pesa ili serikali iweze kupata kodi nyingi, Serikali ikiwaheshimu na kuwajali hayo matatizo yataisha.
 
Hujanielewa, nimezungumzia watumishi kutumia magari binafsi kwa shughuri za serikali na sijazungumzia watumishi kutumia magari ya serikali kwa shughuri binafsi, kwa viongozi wamegawanyika kwa makundi tofauti na stahiki zao zinatofautiana ,mfano mkuu wa idara analipwa 16M za fenicha kila baada ya miaka 5 ,lakini wapo viongozi wengine kila baada ya miaka 3,
Nilikuelewa.

Mimi nimezungumzia jambo hili kwa upana wake zaidi. Kwamba kama kuna audit query kwenye kuweka mafuta kwenye gari binafsi kwa kuwa kuna mstari mwembamba katika kueleza matumizi ya mafuta hayo kwa shughuli binafsi na shughuli za serikali, kwanini kusiwe na tatizo kwa upande wa matumizi ya mafuta ya serikali yaliyowekwa kwenye magari ya serikali pale yanapotumika kwenye shughuli binafsi?
 
Ila hii nchi Kuna watu wanaoishi kama malaika,elimu masters au bachelor Ila salary million 3 bado marupurupu mengine na anapewa usafiri,wakati huo sisi tusio maafisa pamoja na masters zetu we are still under laki 7.
Hii Ni dharau kubwa na ndo maana molari wa kazi unapungua.ni ujinga mkubwa sana.
 
Back
Top Bottom