Serikali inunue Magari ya idara zote za Halmashauri ili kuleta tija na Ufanisi Nchini

Serikali inunue Magari ya idara zote za Halmashauri ili kuleta tija na Ufanisi Nchini

Mbona viongozi wengine waandamizi wa serikali (mawaziri, wakuu wa wakala na idara kubwa n.k.) utumia magari ya serikali kwa shughuli zao binafsi? Waziri anavyoenda kanisani au msikitini kwa gari la serikali, hiyo siyo shughuli binafsi?

Kama alivyosema mdau hapo juu, nami nakubali kabisa haya magari ni mzigo mkubwa sana kwa serikali. Nilishawahi kusema humu kwamba tunapaswa kuwa na ‘government car pools’ kubwa katika kila wilaya, idara na taasisi yenye magari ya aina (size, space, power etc.) tofauti tofauti kukidhi mahitaji husika ya matumizi. Pesa itakayookolewa ikaongezee bajeti za kuboresha usafirishaji na usafiri wa umma. Wakuu wa idara na taasisi watakuwa na options za kutumia magari yao binafsi (kwa kupata misamaha ya kodi na incentives zingine) ama usafiri wa umma kwa shughuli za kutimiza wajibu wao.
Ndugu inaonyesha unaishi sanaa mjini, Kuna wilaya za ajabu kwenye miundo mbinu ndugu huku public transport inatoka asubuhi na kurudi jioni na ni gari MOJA tu, bro umefika wilaya kama Songwe, Kilolo, Momba, Mburu??

#YNWA
 
Sioni umuhimu wa Afisa Elimu kupewa gari kwa ajili ya kufuatilia masuala ya Elimu wakati mwalimu anayefundisha anatembea kilometa kadhaa kufika kituoni....ningetamani sana serikali ichukue hayo mabilioni iwanunulie walimu pikipiki ili iwe rahisi kwao kufika vituoni maana kuna shule zinaweza maliza mwaka mzima hazijawahi kumuona Afisa Elimu amekanyaga hapo unless kuna tatizo ndipo aende hapo ......
Maafisa elimu hawaendi kwasababu Hawana magari.

#YNWA
 
Sawa mkuu lakini Kama issue Ni kutatua changamoto za wananchi Hawa wote wapo kwenye utekeleaji kwaio hatuitaki double standard Kama watapewa izo gari wakuu was idara basi na hao wakuu was shule wapewe
kama injinia ni mmoja hajapewa itakuwa walimu wakuu 200, labda kuwe na mradi kama waratibu
 
Maada Kama hizi nazipenda Sana mtoa maada big up great thinker
 
Ila hii nchi Kuna watu wanaoishi kama malaika,elimu masters au bachelor Ila salary million 3 bado marupurupu mengine na anapewa usafiri,wakati huo sisi tusio maafisa pamoja na masters zetu we are still under laki 7.
Hii Ni dharau kubwa na ndo maana molari wa kazi unapungua.ni ujinga mkubwa sana.
Sikia bro USIACHE NDOTO yako ifee..
Komaa sanaa bro.

Niliajiriwa 2013 na diploma kama Afisa katani.

Nilijiona bado sina elimu na ile nafasi sio yangu, 2014/November nikarudi chuo na na October/2019 nikamaliza masters (niliunga)

Ajira ya diploma yangu sikuielewa.

Kurudi nikakomaa na kuhamishiwa bomani, kwasasa ni mkuu wa Idara mtarajiwa (nasubiri recategorization).

Na wakati huohuo natafuta channel nitoke halmashauri niende taasisi zinazozalisha kama TRA, NSSF, PSPF na kwengine nikawe giant huko.

Nilichojiapia na maisha yangu, SIWEZI KUACHA NDOTO ZANGU ZIFE.

Napambana hasa kutafuta connection, kwani huko juu hawastaafu? Basi nahitaji hizo nafasi.

Mungu ni mwema, nilivyoajiriwa nilikua tofauti na wenzangu kijijini.

Wao walikuwa wanawaza kulima, kuoa, kuzaa mi nikasema "Nina Miaka mi5 ya kwenda Shule nikitoka huko nije kutafuta hela"

Kuingia chuo nilikua bahili hasa kwa ajili ya ndoto zangu na kusema kweli zimetimia kiasi japo nasonga mbele.

Huwa napenda sanaa KUWAPA moyo watumishi kama nyie mnaoteseka na elimu zenu vijijini huko kwamba USIKATE TAMAA, VIZINGITI NI VINGI NA TRUST ME VITAPITIKA NA NIMEVIPITA KWA MSAADA WA WATU NA KUKOMAA MWENYEWE.

TUENDELEE KUPAMBANA.

SEE YOU IN THE UN, AU, SADC OFFICE AS A BIG MANAGER..!!!

#YNWA
 
Kwa nini serikali hainunui sasa hayo magari wakati ni muhimu? Bajeti za mafuta ziwe za makusanyo ya ndani kwa Halmashauri husika
 
Ndugu inaonyesha unaishi sanaa mjini, Kuna wilaya za ajabu kwenye miundo mbinu ndugu huku public transport inatoka asubuhi na kurudi jioni na ni gari MOJA tu, bro umefika wilaya kama Songwe, Kilolo, Momba, Mburu??

#YNWA
Ndiyo maana nimesema pesa itakayookolewa iboreshe barabara na usafiri wa umma. Hivyo it’s a process.
 
Back
Top Bottom