Serikali isitishe kulipa mishahara watumishi walioamua kurudi tena masomoni ni upotevu mkubwa wa pesa tena wengine wanahama fani kabisa.

Acha roho mbaya, tena kama hujui SERIKALI inatakiwa kumsomesha, yaani kulipia ada na accomodations
 
Mkuu Wacha roho ya korosho. Kuongeza maarifa ni haki ya kila binadamu. Kuna wataalam wengi serikali inawatumia na haikowasomesha.

Mawazo ya kikomunisti haya!
 
Yaani huyu hana akili na ndio maana muajiriwa yeyote yule anapoajiriwa kuna mkataba wanaingia na kwenye mkataba kuna muajiriwa kujiendeleza huku akigharamiwa na mwajiri wake.
Ila watu mama hawa ndio wakipata vyeo wanawakandamiza walio chini yake. Imagine huyu anaionea huruma pesa ya serikali amabyo inatumia kuwajengea uwezo wataalamu wake je cku akipata cheo afu ndio inatakiwa awalipe watu posho zao ataweza kweli?

WEWE CHAMAA UNA ROHO MBAYA YA KICHAWI MAANA YAKE WEWE NI MCHAWI
 
Acha roho mbaya, tena kama hujui SERIKALI inatakiwa kumsomesha, yaani kulipia ada na accomodations
Yaani waache kuwapa mikopo freshers wampe pesa huyu mtumishi ambaye kwa hiyari yake katakankwenda kusoma? Na ikumbukwe kipindi anaenda kusoma hakuna anachokiingizia taifa faida.

Kama watumishi elfu 5 wote wameenda kusoma unadhani ni kiasi gani cha pesa kinapotea bure?
 
Sio uchawi ni uhalisia , kama watumishi zaidi ya elfu 5 au 10 wote wapo masomoni unadhani ni kiasi gani cha pesa kinapotea bure?

Wewe umeamua kujiendeleza basi pambana na hali yako.
 
Sio uchawi ni uhalisia , kama watumishi zaidi ya elfu 5 au 10 wote wapo masomoni unadhani ni kiasi gani cha pesa kinapotea bure?

Wewe umeamua kujiendeleza basi pambana na hali yako.
Je kati ya mtumishi ambaye yupo kwenye ajira na mwanachuo anayepewa mkopo mwisho wa siku anakosa ajira ni wapi serikali inapata hasara?
 
yaani kuwasomesha wananchi wako ili kuongeza ufanisi kazini ni hasara?
 
Huna akili ww sisi kama chama tawala tunakuamuru kufuta uzi wako mara moja ni upotofu kwa umma WACHA MAMA YETU AUPIGE MWINGI
 
Imagine mtu km huyu ndio boss sasa ofisini kwenu..roho kubwaa ovyoooo!
 
Ndugu yangu hii haitasaidia wewe jobless kupata Ajira,labda toa ushauri serikali iwauwe watumishi wote hapo ndo utapata Ajira.

Sheria zinamtaka mwajiri kumsomesha mtumishi pale anapotaka kujipendeleza kielimu,mfano sera ya elimu ya Sasa inataka mwalimu wa sekondari awe na elimu ya chuo kikuu(digrii) Sasa mimi mwalimu wa diploma in secondary Education mwajiri wangu anifikuze au anipe Muda wa kwenda kusoma!?
 
Chai
 
I bet utakuwa na chembechembe za uchawi ndani yako
 
Duh, hii ni changamoto kweli kusoma ni muhimu Kwa Sababu Dunia inabadilika Kila siku Sasa mtumishi asipoenda kusoma maarifa mapya atayapataje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…