Serikali itoe tamko kuwa mwanafunzi akikutwa na simu anafukuzwa shule

Mkuu kumbuka Magufuli alikuwa mwalimu na unajua kabisa sifa kubwa ya mtu kuwa mwalimu hapa Tanzania ni kufeli,sasa unategemea nini kwa watu wa aina hii? last year nilimletea zawadi mwanangu ya computer ndogo from US unaambiwa alipoenda nayo shule ilikuwa heka heka,heka heka ziliisha nilipoamua kuomba uhamisho wa mwanangu kwenda shule nyingine,yaani Kuishi nchi za dunia ya saba ni shida sana
 
 
ukimnyanganya wa kwangu lazima nikupe kipigo bahati mwanangu hasomi shule zenu za bure
 

Wewe kama siyo Mhaya au Mjita au Mnyakyusa ( Wapenda Sifa / Ujivuni usio wa lazima ) basi nakufa kwa Makusudi Ndugu.
 
Dunia ya saba shida kweli kweli,Kwa hiyo mwanafunzi wa kitanzania anatakiwa kukutana na simu au computer akifika chuo kikuu si ndiyo?
Simu ni wakati wa likizo tu , computer ni somo linafundishwa shuleni
 
Wewe kama siyo Mhaya au Mjita au Mnyakyusa ( Wapenda Sifa / Ujivuni usio wa lazima ) basi nakufa kwa Makusudi Ndugu.
wewe ni miongoni wa hao wanaoona mwanagunzi kutumia simu shuleni ni sababu za wao kufeli wakati magufuli anasoma hapakuwa na simu za mkononi na still alifeli
 
Simu ni wakati wa likizo tu , computer ni somo linafundishwa shuleni

Naona bado unazidi tu Kuonyesha ' Udhaifu ' wako wa Kifikra na hasa katika Ujengaji wa Hoja. Kwani huwezi Kunyamaza tu ili utuachie wenye ' Akili ' kubwa tukufundishe jinsi ya Kujenga Hoja zenye Mantiki na Tija ili na Wewe uwe unajifunza na unaokoteza okoteza Kwetu? Yaani hapa umeandika ' Pumba ' tupu na ndiyo unazidi Kutulazimisha tuendelee Kukudharau.
 
Hapo umene kweli
 
Watoto wa siku hizi wameshindikana.
Simu zinazurula huko shuleni Hadi Basi...ukaguzi huwa unafanywa ila mwanafunzi ni mwanafunzi tu.
 
Kwani sasa hivi sheria inasemaje mwanafunzi anapokutwa na simu shuleni?
Kila shule zinatofautiana za serikali hazina mwongozo za private zingine ukikutwa na Simu wanakufukuza shule. Na kwenye joining instruction wanakueleza kabisa kuwa simu Ni marufuku na Kuna baadhi ya vyuo vya kikatoliki vya masomo ya kawaida kabisa vingine havitaki kabisa mwanachuo awe na simu chuoni.
 
Hayo ni mawazo ya watu mnaoishi nchi za ulimwengu wa kumi
Kama umewahi kufanya private sector na watu wa nje Kama wazungu ,wahindi na wamarekani,wajapani na wachina endekeza kisimu chako uone muziki wake.Wengi hawataki kabisa uwe na simu kazini.Unatakiwa uizime kabisa utaiwasha ukimaliza Kazi zao.

Bill gates au Dangote ulishawahi waona popote wakitembea Wana Simu mikononi na Wana chat Kama hivi vitoto vilofa vyanafunzi vya kitanzania vilivyonunuliwa Simu used na Wazazi wao malofa wanaotembelea magari used waliyonunua kwenye majalala ya magari used Japan? Ama kweli maskini akipata hata kasimu mtumba matako hulia mbwata
 
athari za Simu ziko kwenye shule za wasichana mimi niliposoma tulifaulu kwa kiwango cha juu na Simu tulitumia Kama kawaida darasani tu Simu isisikike, pia usilalamike Simu kuibiwa
 
Wanafunzi kuwa na simu ni UJINGA na tunawaharibu watoto.
Asilimia 97 wanazitumia kubetia, kuwasiliana na wapenzi, na kuangalia porno. Asilimia 2 wanazitumia kwa matumizi yote kusomea na kufanyia ujinga na asilimia 1 ndo wanatumia kwa matumizi sahihi tu.
Sasa ni lipi jema tuwaachie simu kwa ajili ya hiyo asilimia 3 hasa asilimia 1 wanao stahili au tuwapokonye kuwanusuru asilimia 97!?
Nasema hivo kwa sababu nimewahi kufundisha kwa kipindi fulani, shida sisi african hatujafika hatua ya wenzetu wazungu kuwa na self limit tusiige wazungu please tutawapoteza vijana wetu. Kuna watoto unakuta anaomba ruhusa anaondoka boda inakuja inambeba unajiuliza hii boda ilijuaje ka anaondoka huyu mtoto???
Sababu za kufanya vibaya kwenye mitihani zipo nyingi zimesababishwa na wazazi na mfumo wa uchumi kwa ujumla 35% walimu 20% Serikali 30% mtoto 15%
How! Inahitaji uzi maalum.
 
Upo sahihi.
 
Sijui wenzangu, mimi watoto wangu wanafunzi wote wanasimu za smart.
Zinawasaidi kwenye masomo yao.
Tena nawawekea bando la mwezi mzima na wanafanya vizuri Darasani.
Simu zinawasaidia hata kujifunza Lugha mbalimbali kwani Kuna App za kufasili Lugha mabalimbali.
Siwezi kuwachelewesha wanangu kwenye teknolojia kwa sababu ya Sera za nchi masikini.
Mwanafunzi anajufunza Somo la Hesabu vizuri zaidi kwenye App za Simu kuliko hata anavyofundishwa na baadhi ya walimu wetu.
Kinachotakiwa ni kuwaeleza namna na wakati mzuri ya kutumia simu.
 
Hadi dakika hii nafanya kazi na Washington based organization na tunahata whatsApp group,social media tunazitumia kufikisha ujumbe kwa wadau wewtu
 
Tupe mrejesho wa maendeleo ya dogo,Bado anamiliki simu au simu unaimiliki wewe yeye anatumia tu muda wa kujifunza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…