Serikali iwe moja na iitwe Zanzibar, capital iwe ZNZ Town kama ilivokuwa 1700s

Serikali iwe moja na iitwe Zanzibar, capital iwe ZNZ Town kama ilivokuwa 1700s

Uoni hata aibu, eti Tanganyika ni mali ya Zanzibar!!!
Vichekesho vitupu unaleta hapa JF.
Mlidhani kujitawala ni jambo la mchezo eeh.
Mtaendelea kuwa chini ya utawala wa Tanganyika au Oman maisha yenu yote.
 
LumumbDar,

hukuwahi kuusikia ule msemo wa kiswhaili usemao WAJINGA NDIO WALIWAO, nadhani umepata jawabu lako rasmi hapo

Soon baada tu ya kuondokana na nyinyi znz will shine again.

Unasikia na uiweke emaill hii................MIMI BINAFSI NINAAHIDI NA ISHALLAH NITATIMIZA AHADI YANGU, KUPELEKA MABUKU NA KALAMU NA PENSELI KWA SKULI ZOTE ZA ZANZIBAR NA KULEPEKA VYANDARUWA KWA KILA KITANDA CHA KILA HOSPITAL ZANZIBAR NZIMA. kwani zanzibar kuna watu wengapi?????

utasema kwanini hupeleki sasahivi? sasa hivi mushkila mkubwa sana kuisimia znz, si unajuwa matekeo tu ya mitihani anatokea mchaga mmoja pale wizara ya elimu anasema wazanzibari wamekopia kwanini wafanye vivuri sana katika mitihani...stupid fellows running ur system.

sasa mimi ni mtu wa kaiwada tu, wapo jamaa wamefanya ZANZIBAR FOUNDATION ....sasa ina 3 billion US$, pesa hizo vipo standby, uvunjike muungano tu kazi ya kuijenga zanzibar upya itaanza, kama muungano haukuvunjika, ndio tuseme hypothetically speaking ndio dola iitwe zanzibar pia tutasaidia zanzibar yetu.

ahasante
 
Tanganyika ,Tanganyika
Nakupenda kwa moyo wote.
Nchi yangu Tanganyika nilalapo nakuwaza wewe.
.................................

Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums
 
Stroke

hii ni historia mambo leo, ni historia katika pilitical system na mawimbi na dira ya watu wanaotaka kujujuwa na kujuwa ukweli wao kama ulivo. Nimeliona kundi la historia huko lakii nahisi mada hii inagusa zaidi siasa ya leo zaidi.

kitu ambacho ustadh wangu na wenzako munajaribu kukipiga chenga nikwamba

1. utumwa ulifutwa rasmi duniani, kwahivo kurejea haiwezekani

2. Oman ilipinduliwa zanzibar, kwahivo kurejea tena east afrika haiwezekani

3. Fukwe za Tnganyika zilikodishwa kwa mjerumani na nyaraka zipo na hakuna nyaraka zisemazo funkwe hizo hadi mile 10 ndani ya tanganyika zimegaiwa kwa watanganyika. Kwahivo nafasi ya zanzibar kuzidai fukwe hizo ipo nani haki yao kwahvo hakuna sheria itakayoweza kulippinga hilo, dodoma hawatothubutu kusema lolote wala kufanya lolote. no choice

sijui umefahamu hilo kuna nyaraka za kodi, sasa hemu nihesabie 10 mile kutoka bandarini itakuwa hadi wapi??????

Ndio maana tanganyika wameharamisha muungano kujadiliwa, wanajuwa hilo na wana uhakika nalo, kuwa wataloooz fukwe nzima kuzini hadi tanga juu huko. kwasababu anytime muungano ukivunika tu, tutakwenda UN kuidai sehemu yetu.....

ahsante
 
Msingida

Mwalimu Nyerere ndie aliyekudhulumuni na kukunyimeni nchi yenu.

Alipofanya muungano wa makubaliano na sio wa katika, akaiuwa serikali ya tanganyika, au akaivisha ngozi ya serikali ya Muungano. akawaacha watanganyika katika mataa.

Sisi wazanzibari japo kuwa serikali yetu haitambulikani lakini bado tunayo serikali yetu.

ahsante
 
...ka Zanzibar kadogo..!! eti ndo tugawane sawa kwa sawa...? no way...come back Tanganyika please i miss you ssooo muchi....
 
Najuwa kujitawala si mchezo ndio maana Tanganyika iko hohe hahe pamojana kwamba 60% ya ardhi yake bado binadamu hakuwahi kuweka mguu, pamoja na kwamba kuna rivers, lakes around tanganyika, pamoja na kwamba mvua zipo kila msimu, Tanganyika inauwezo wa kuilisha Afrika nzima ikiwa itaitumia ardhi yake kwa kilimo lakini bado tanganyika kuna njaa na hata ilipata ukame siku za mkapa......kujitawala is not a joke.

kazi yenu kuiibia serikali tu, kila kiongozi ni billionaire ...mali asili dhahabu na almasi ni nani anayejuwa zinapelekwa wapi? magogo na mbao ni nani anayejuwa zinapelekwa wapi na ni nani nayeshughulikia?

Air tanzania,Uda na raiways zimekufa, u are so funny but arrogant drunkards, yaani kwa mujibu wa population ya tanganyika vipi vyanzo vya usafiri zife? kwasababu kujiongoza is not a joke......

Wewe sema utakavo na watanganyika wenzako waseme watakalo lakini labda ndio muungano usivunjike milele, lakini siku ukivunjika tu na hata iwe kesho basi you are loosing big time. eneo la znz ambalo mjerumani amelikodi litarudi, na mutaanza kulipia kodi kwa serikali ya znz kwa mali zenu pale

Mutaona nini maana ya kuwa landlocked country
 
Gefu

Ni nani alomtuma Mwalimu Nyerere afanye Muunganio na zanzibar?

Ni nani alomtuma Mwalimu Nyerere Alifute taifa la Tangayika kwa kutumia kichaka cha Muungano?

Kwanini Watanganyika mundaendelea kukubali Nchi yenu kuwa behind the scene?

Ikiwa mulikubali kuungana na zanzibar kwa sababu zozote zile shauri lenu ......sasa kila kitu kigaiwe sawa sawa ....mafuta yenu, dhahabu na almasi yenu, copper na gas, na mapato ya TRA na Central Bank yenu, ndio mara nyengine mutashika adabu yenu na kujuwa munataka nini na nini ndio muhimu kwa Mtanganyika wa kwaida.

Ikiwa hamuwezi wachieni ngazi, zanzibar haina haja ya muungano na tanganyika

ahsante
 
hivi ni nani huyo kiongozi shupavu wa Zenj Empire aliye kuwa akiishi Zanzibar Town?
Sp
 
Nyinyi wote unabishana upumbavu kwasababu maelezo yenu yanaonyesha wote nindugu hivi unafikiri watu watanga na wa mwambao wote mtawagawa kwamba hizo mile 10 ziwe ni sehemu ya Zanzibar, vipi kuhusu wale walio more than 10miles hawana haki ya kutumia bahari ile? Sijui ni lini binadamu watakuja kujitambua kama wao ni kitu kimoja?

Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums
 
Dean

Huwezi kuwa na uhakika kwasababu wanaohusika kukueleza wewe ukweli wamekudanganya ili kupata maslahi yao binafsi ya kukutawalaeni kama wanyama pori tu

Angalia na hizi sasa, kumbuka tu ramani za duni azilichorwa na wazungu na sio sisi

9k=


attachment haionekani
 
We BinFaza mtu muungwana sana. Nimekupenda sana. Labda nikuombe niongezee jambo dogo hapo kwenye kauli yako. Zanzibar kuna watu wana mashaka sisi Watanganyika tunataka kuwaharibia mila yenu ya Uislamu. Mimi nakwambia hakuna mtu ana makusudi ya kuaribu uislamu Zanzibar. Njia mtu anayochagua kumwabudu Mungu ni ya kwake binafsi.

Njoen hata kwetu Mbeya Faza, achana an hii pwani ya Dar es Salaam na Kilwa; njoo uone kama tutawakataza kujenga misikiti. Mimi mwenyewe hapa nitakupatia kiwanja ujenge msikiti. Njia ambayo mtu anachagua kumwabudu Mungu ni ya kwake binafsi mradi isiingilie uhuru wa wengine kuchagua aina ya ibada wanataka.

Jengeni misikiti hata milioni moja mkitaka--jengeni ardhini, kwenye rooftops, au popote mnapotaka, mradi nanyi mnikubalie kujenga makanisa au hata mabanda ya vinyamkera popote nataka. Njoooooni!!!



Wananchi Wezangu,

Nami leo ninapenda kutowa maoni yangu, ingawaje sidhani kwamba jaji Warioba na kundi lake watayasikia maoni haya.

Kwanza ningependa kuyapa uzito maoni yangu kwa kuweka hii map ya Zanzibar ya mwaka 1886, kabla ya mile 10 za fukwe ya Tanganyika na Kenya kukodishwa kwa miaka 99 kwa wajerumani na waingereza.

Kabla ya wazungu kuifanya ramani hii, tanganyika ilikuwa ni sehemu ya Zanzibar, mjerumani ikaipora sehemu hiyo na kuifanya koloni lake.

Mimi ninaamini moyoni kwamba sisi wazanaibari na watanganyika ni wamoja kidamu na tulikuwa raia wa nchi moja, sulatanate of zanzibar,

Kwa mtazamo huo na tufanye tu nchi moja lakini iitwe zanzibar na capital city yake iwe znz town, na musiseme znz town ni mji mdogo kuwa capital, kwani dodoma hakuna kitu chochote cha kuifanya iwe capital ya tz, hata airport hakuna.

Tujikombowe kutoka makucha ya wakoloni na turejeeni katika asili yetu ya Dola ya zanzibar

Ahsanteni

EAFR1886.gif
 
Sasa fundishaneni huu ujinga kwenye 'skuli' halafu ndio mtajua kazi ya Dr. Ndalichako ni kusahihisha au kubalansisha
 
Gefu

Ni nani alomtuma Mwalimu Nyerere afanye Muunganio na zanzibar?

Ni nani alomtuma Mwalimu Nyerere Alifute taifa la Tangayika kwa kutumia kichaka cha Muungano?

Kwanini Watanganyika mundaendelea kukubali Nchi yenu kuwa behind the scene?

Ikiwa mulikubali kuungana na zanzibar kwa sababu zozote zile shauri lenu ......sasa kila kitu kigaiwe sawa sawa ....mafuta yenu, dhahabu na almasi yenu, copper na gas, na mapato ya TRA na Central Bank yenu, ndio mara nyengine mutashika adabu yenu na kujuwa munataka nini na nini ndio muhimu kwa Mtanganyika wa kwaida.

Ikiwa hamuwezi wachieni ngazi, zanzibar haina haja ya muungano na tanganyika

ahsante


aaaaaaah?!! nimekusifia sasa hivi alaf yuleyule binfaza kageuka tena kusema huu utumbo? mi nilikuona mtu wa maana; muelewa.... hii nini unasema sasa. huna msimamo, au? we siumetaka serekali moja sasa hivi hapa? sasa hii ya kuachia ngazi imeanzaje tena! aaaah! huna maana kabisa kumbe....
 
Highlander

Ahsante sana kwa nasaha na kauli zako njema. Nakushukuru sana kwa kutoa ahadi hiyo ya kuweza kunipa kiwanja cha kujenga msikiti mbeya. Na nakuahidi kwamba nitaitikia wito wako, muda ukifikia nitawasiliana na wewe.

Ninahakika kwamba wewe ni mkiristo mwema na msomaji mzuri wa bibilia kwahivo unajuwa wazi kwamba uislamu ni dini ya mitume wote waliomo ndani ya bibilia akiwemo Yesu mwenyewe. Pia ninajuwa unajuwa kwamba Mtume wetu Muhammad SAW katajwa kwa jina katika Songs of solomon 5:16 hebu funguwa ikiwa hukuliona jina Muhammad nitakuonesha.

Dini ni chaguo la mtu na hakuna mtu nayewekea gunduki kulazimishwa kutembea uchi au kuvaa kiheshima au kukatazwa kuingia msikitini au kanisani. Ni chaguo binafsi.

Labda kinachowatisha wazanzibari zaidi ni kuona idadi ya makanisa yanayojengwa huko hayana proportional balance na idadi ya wakiristo walioko zanzibar.

Ahsante
 
Highlander,

katika kujibu swala ujuwe kuna nafasi ya muulizaji na kuna nafasi muulizwa, swala linajibika kwa mujibu lilivoulizwa, ikiwa mtu anaanza kufanya kejeli na kafsha fulani inabidi tufanye ile kazi....SAMAKI MKAANGE KWA MAFUTA YAKE
 
Highlander,

katika kujibu swala ujuwe kuna nafasi ya muulizaji na kuna nafasi muulizwa, swala linajibika kwa mujibu lilivoulizwa, ikiwa mtu anaanza kufanya kejeli na kafsha fulani inabidi tufanye ile kazi....SAMAKI MKAANGE KWA MAFUTA YAKE

Mi nadhani hoja yako ya mwanzo niliielewa. Nilikuwa nataka tuelekee sasa kwenye utata unaozusha hizi chuki baina yetu. Mgogoro uliopo katikati yetu una sura kama tatu hivi kubwa BinFaza.

Tatizo la kwanza ni tatizo la elimu: si kila mmoja katika hizi nchi zetu amesoma akapata digrii za mahusiano ya kimataifa, ili kujua umuhimu wa kuungana. Hilo ni tatizo la elimu ambalo lipo kila upande wa Muungano wetu. Kwa hiyo ni vizuri wale wanaojua hata kuweka hizi ramani na uhalisia wa udugu wetu wa damu kama wewe tuwasaidie wale wasioelewa haya mambo. Ingawa nakubaliana kuna majibu tunayatoa humu kwa hasira tu. Naomba unisamehe kwa kusema huna maana. Umenielewesha vizuri kwa nini umemjibu yule mchangiaji hovyo pale.

Tatizo la Pili linaloleta mgogoro baina yetu ni la kiuchumi. Umaskini uliopo bara na visiwani unalazimisha watu kushika mchawi. Wanadhani umaskini umeletwa na Muungano. Na hili si kweli pia. Umaskini haujaletwa na Muungano. Umaskini umeletwa na uendeshaji mbovu wa uchumi katika nchi zetu. Tunahitaji kushikama kubadili watu wanaoendesha uchumi wetu tuweke watakao ondosha hizi njaa na umaskini wa kutupa. Tatizo si Muungano, tatizo ni usimamizi na uendeshaji wa uchumi wetu.

Tatizo la tatu ni Dini. Wanzanibari wana mashaka tunataka kuwaharibia dini yao kule. Hili ndilo ambalo nilitaka kujadili nawe kwa maneno haya: Zanzibar kuna watu wana mashaka sisi Watanganyika tunataka kuwaharibia mila yenu ya Uislamu. Mimi nakwambia hakuna mtu ana makusudi ya kuaribu uislamu Zanzibar. Njia mtu anayochagua kumwabudu Mungu ni ya kwake binafsi.

Njoen hata kwetu Mbeya Faza, achana an hii pwani ya Dar es Salaam na Kilwa; njoo uone kama tutawakataza kujenga misikiti. Mimi mwenyewe hapa nitakupatia kiwanja ujenge msikiti. Njia ambayo mtu anachagua kumwabudu Mungu ni ya kwake binafsi mradi isiingilie uhuru wa wengine kuchagua aina ya ibada wanataka.

Jengeni misikiti hata milioni moja mkitaka--jengeni ardhini, kwenye rooftops, au popote mnapotaka, mradi nanyi mnikubalie kujenga makanisa au hata mabanda ya vinyamkera popote nataka. Njoooooni!!!

Hebu mimi na wewe tujadili hili sasa... tunafanyaje nalo?
 
Back
Top Bottom