Serikali iwe moja na iitwe Zanzibar, capital iwe ZNZ Town kama ilivokuwa 1700s

Serikali iwe moja na iitwe Zanzibar, capital iwe ZNZ Town kama ilivokuwa 1700s

Highlander

Ahsante sana kwa nasaha na kauli zako njema. Nakushukuru sana kwa kutoa ahadi hiyo ya kuweza kunipa kiwanja cha kujenga msikiti mbeya. Na nakuahidi kwamba nitaitikia wito wako, muda ukifikia nitawasiliana na wewe.

Ninahakika kwamba wewe ni mkiristo mwema na msomaji mzuri wa bibilia kwahivo unajuwa wazi kwamba uislamu ni dini ya mitume wote waliomo ndani ya bibilia akiwemo Yesu mwenyewe. Pia ninajuwa unajuwa kwamba Mtume wetu Muhammad SAW katajwa kwa jina katika Songs of solomon 5:16 hebu funguwa ikiwa hukuliona jina Muhammad nitakuonesha.

Dini ni chaguo la mtu na hakuna mtu nayewekea gunduki kulazimishwa kutembea uchi au kuvaa kiheshima au kukatazwa kuingia msikitini au kanisani. Ni chaguo binafsi.

Labda kinachowatisha wazanzibari zaidi ni kuona idadi ya makanisa yanayojengwa huko hayana proportional balance na idadi ya wakiristo walioko zanzibar.

Ahsante

Ni kweli mimi ni mkristo ingawa sijaenda kanisani kwa muda sasa. Utakapokuwa tayari kutaka kiwanja cha Msikiti Mbeya nipe PM humu ujue sitanii. Uislamu umejengwa juu ya msingi wa dini ya Kiyahudi ya Judaism ndiyo maana mitume wote waliopo katika Biblia wanapokelewa na dini ya Kiislamu. Waislamu wanafuata torati ya musa kwa sababu hiyo; wanavaa bargashia kwa sababu hiyo, wanavaa kanzu kwa sababu hiyo, hakuna kuvaa viatu msikitini kwa sababu hiyo. Wakristo wanawakubali mitume wote hao ambao waislamu wanawakubali. Tunaunganishwa na torati ya Musa. Waislamu wanapokea mafundisho mengi ya Kristo, ingawa si yote. Kwa hiyo tunaunganishwa pia na hayo machache katika Kristo ambayo Waislam wanayapokea. Tatizo ni kwamba Wakristo wanamkataa Mtume Muhammad (SAW). Mgogoro wetu upo hapo. Lakini mimi sipendi kuuita mgogoro kwa sababu kila mtu anatakiwa kuwa huru kuamini anavyotaka.

Tukiwapa watu wetu uhuru wa imani, tukawapa wahubiri wa pande zote uhuru wa kuuza mawazo pasipo kubeza, kutukana, kudharau mitazamo ya watu wengine nchi yetu haina tatizo. Tazama upumbavu wa kupita kwenye majumba ya ibada kubeza dini za watu wengine linakotupeleka!
 
kwa bahati mbaya nyerere alikabishiwa tangayika ambayo coastal strip ni sehemu waliokodishwa wajerumani na serikali ya zanaibar. nyerere alilijuwa hilo ndio akalazimisha muungano
 
baba wenu wa taifa

ni cheo cha roman katoliki hicho

nyerere kapewa kutokea itali kwa kuuwezesha ukatoliki kuitawala tanganyika
 
baba wenu wa taifa

ni cheo cha roman katoliki hicho

nyerere kapewa kutokea itali kwa kuuwezesha ukatoliki kuitawala tanganyika

s'alykum sheikh...?
Naona unaharisha mdomoni,mana mineno yako kama umekurupukia kwenye shimo la choo,au majini yameshapanda?mana nasikia ukisoma sana yale mavitabu unakuwa sakara
 
Lidaku

s'alykum sheikh...?
Naona unaharisha mdomoni,mana mineno yako kama umekurupukia kwenye shimo la choo,au majini yameshapanda?mana nasikia ukisoma sana yale mavitabu unakuwa sakara

nakushukuru kwa mara nyengine, una uhuru wako wa kutowa maoni na kusema utakavo

kwani kila ukweli ni lazima uujuwe au uukuballi wewe?

kwa sisi wa znz, tumajuwa nyerere alivotufanyia niyinyi watanganyika munajifanya hamuoni, shauri lenu
 
nyie watu mbona hamueleweki mara mnataka kujitenga mara mnataka nchi moja lakini jina liwe zanzibar na makao makuu yawe zanzibar ok ebu tuachane na hizo hadhithi zako tuje kwenye hoja ukizungumzia zanzibar kabla ya mwaka 1886, mimi nitapenda uzungumzie zanzibar kabla ya mwaka 100 ilikuwaje? na kama tukirudi kwenye hizo historia zako basi hata iringa wana dola yao iliyokuwa inaongozwa na mkwawa. cha msingi ni kujua tanganyika ilipata uhuru ikiwa na mipaka ipi na zanzibar ilifanya mapinduzi na kupata uhuru ikiwa na mipaka ipi, pia hatuwezi kuwa watumwa wa historia coz waliofanya maamuzi ya kugawa mipaka wakati huo ni binadamu kama mimi na wewe na walifanya hivyo kwa utashi na faida yao na sisi tuna uhuru wa kufanya maamuzi yetu sasa kwa faida yetu hata tukiamua tuigawe na zipatikane nchi 3 ndani ya tanzania
 
Sisi tunakataa ukoloni wa aina zote, hatukatai ukoloni wa Wajerumani na waingereza tuu ili kuuthibitisha ukoloni wa waarabu, yaonekana wewe una ajenda ya kuukataa ukoloni wa waingereza na wajerumani ili uturudishie ukoloni wa Waarabu ambao ni mbovu kuliko huo ukoloni wa waingereza, tunakataa ukoloni wa aina zote na
 
Fikira mbadala na yenye mshiko wa kihistoria! Usilopenda kulitaja ni kwa jinsi ya wapogoro na wazaramo walivyopigana kishujaa kukataa utawala huo wa kipwani, na hapa sijazungumzia mashujaa kama wale wa kule Iringa, Unyanyembe, Usukumani na Uchagani na hata hapo karibu na Zanzibar kwa Wazigua/Usambarani!

Kama ni dola ndiye kitambulizi cha utaifa basi pengine tungekwenda ndani ya historia tuangalie ni dola gani ilikuwa kubwa zaidi kabla ya ukoloni ndio tuibebeshe utaifa wetu, taifa moja, serikali mmoja.

Hutoipata zaidi ya Zinjibar, oppss siku hizi Zanzibar, katika Afrika.
 
Tena kwa kuwakumbusha tu, wasioijuwa maana Zanzibar, ile "bar", herufi tatu za mwiso, ina maana ya bara na si visiwa.

Hilo jina muafaka na la asili kabisa ya hii nchi.

cc. Bin Faza
 
Back
Top Bottom