tramadol
JF-Expert Member
- Oct 10, 2015
- 5,383
- 4,323
Muda wote tunategemea mvua za msimu katika kilimo chetu na mvua zenyewe zimekuwa zinabadilika badilika sana kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa duniani yaani climate change.
Serikali ingewekeza sana katika sekta hii ya kilimo hasa kilimo cha umwagiliaji kwa kujenga miundombinu yake imesaidia sana kufanya kilimo cha uhakika kuliko kilimo hiki cha kutegemea mvua za msimu.
Nchi ya Tanzania imebarikiwa sana kuwa vyanzo vya maji vya kutosha kila sehemu hivyo maji si tatizo kabisa.
Ardhi ya Tanzania kila kitu ikakubali ukilima kwahiyo sekta hii ingesaidia sana kuwainua watanzania kiuchumi kwa kuuza ndani na nje ya nchi mazao mbalimbali yenye ubora unaofaa kitaifa na kimataifa.
Nchi kama Japani wameweza kujenga miundombinu ya umwagiliaji katika ardhi kidogo waliyokuwa nayo na wanaitumia vizuri sana kuilisha Japani na hata kuuza nje na pia kutoa misaada ktk majanga ya kiasili yakitokea.
Waziri mwenye dhamana na sekta ya kilimo angalia jinsi ya kuboresha kilimo cha umwagiliaji,pembejeo bora, wataalamu kutumika ipasavyo wa SUA, masoko bora ya mazao nk.